• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Comments |
Iramba District Council
Iramba District Council

The United Republic of Tanzania Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Iramba District Council

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Maajabu ya Mtemi Shuluwa Kisharita Wilayani Iramba Mkoa wa Singida.

Posted on: October 16th, 2019

By Hemedi Munga, Irambadc

tehama@irambadc.go.tz

Iramba. Mzee Edward Mshogola (76) mkazi wa kitongoji cha Kilundo kata ya New-kiomboi Tarafa ya Kisiriri Wilayani Iramba Mkoa wa Singida Tanzania amemfananisha Mtemi Shuluwa na Mtemi Mkwawa wa Iringa na Mtemi Mirambo wa Urambo Tabora.

Mshogola ameyasema hayo leo Jumatano Oktoba 16, 2019 wakati akiongea na Mwandishi wetu kitongoji cha Kilundo.

Mtemi Shuluwa aliyeishi kijiji cha kisharita kata ya Kinampanda Wilayani Iramba alikua bingwa wa vita za zamani zidi ya maadui zake kutoka maeneo ya Kinampanda, Wembere na Ruruma.

Shuluwa alitumia maarifa na tamaduni kuwaziwia maadui zake wasifike maeneo ya utawala wake.

Akisimulia Mshogola kuwa Shuluwa alikuwa shujaa na mwenye uwezo wa kueleza ujio wa vita.

 

“Shuluwa alikuwa anaota kuwa vita vinakuja kutokea pande ya mashariki au kaskazini”Alongeza Mshogola

Hali hiyo ilimfanya Mtemi Shuluwa kuwaita waganga wa kiutamaduni kufanya Tawile.

Akifafanua maana ya Tawile, Mshogola amesema kuwa walikuwa wakikamata kuku wanampasua kisha wanaangalia adui yuko upande gani.

Maarifa hayo yalimuwezesha Mtemi Shuluwa kufanya madawa ambayo yaliwafanya maadui zake kutoka Kinampanda, Wembere na Ruruma kutoingia kwenye eneo la utawala wake.

Kipindi hicho kulikuwa na uwadui wa wenyewe  kwa wenyewe kutaka kutawala maeneo ambayo mtemi wake atapigwa. Alibainisha Mshogola

Akieleza hatima ya Mtemi Shuluwa, Mshogola amesema Mtemi huyo aliota ndoto na kuwasimulia wajomba zake kuwa “ Mtatawaliwa na mtu mweupe”

Tafsiri na maana ya ndoto hiyo ilikamilika wakati Muingereza alipotuwa katika utawala wa Mtemi Shuluwa huku wakitumia chombo maalumu.

Kwa kuwa maarifa na tamaduni alizozitumia Shuluwa kujificha katika jiwe hilo na kutoonekana na adui yoyote hakuwafanyia wajomba zake walikutwa na Waingereza.

 

Wakiwa katika utawala wa Mtemi Shuluwa, Waingereza waliwakuta wajomba wa Mtemi huyo na kuanza kuwaadhibu wakiwataka wawaoneshe alipojificha Shuluwa.

Mateso na maumivu yaliwafanya wajomba wa Mtemi huyo kuwaonesha Waingereza mahali alipojificha Shuluwa katika jiwe lake mithili ya kiti, Aliongeza Mshogola

Wazungu hao walimkuta Shuluwa katika jiwe mithili ya kiti lililopo Kisharita inayopakana  na kijiji cha Kilundo kata ya New-kiomboi Wilayani Iramba.

Mshogola alisema kuwa Shuluwa alichukuliwa hapo na huenda maarifa na tamaduni zake hakuwachia ukoo wa Shuluwa unaopatikana Kisharita, Kilundo na maeneo mengine wilayani humo.

Announcements

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU January 02, 2026
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI June 05, 2025
  • View All

Latest News

  • SIKU YA UKIMWI DUNIANI DISEMBA 1,2025

    December 01, 2025
  • MAZOEZI YA VIUNGO YA KILA IJUMAA KWA WATUMISHI NA WANANCHI WOTE WA KIOMBOI NA MAENEO YA JIRANI

    November 27, 2025
  • RATIBA YA CHANJO NA UTAMBUZI WA MIFUGO KATA YA KASELYA

    November 25, 2025
  • DC MWENDA AWAPONGEZA WALIMU NA WANAFUNZI WILAYANI IRAMBA KWA MATOKEO MAZURI MTIHANI WA KUHITIMU ELIMU YA MSINGI

    November 24, 2025
  • View All

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
More Videos

Quick Links

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Related Links

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    KIOMBOI, IRAMBA

    Postal Address: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Telephone: 026 - 2532253

    Mobile: 026 - 2533001

    Email: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.