• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

MADIWANI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA IRAMBA, WAOMBWA KUHAMASISHA WANANCHI KUCHANGIA DAMU SALAMA KWA LENGO LA KUONDOA JANGA LA UPUNGUFU WA DAMU SALAMA KATIKA HOSPITALI YA WILAYA HIYO

Posted on: May 1st, 2024

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba Mkoani Singida Michael Matomora, ametoa wito kwa Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba Innocent Msengi pamoja na Waheshimiwa Madiwani kwenda kuwahamasisha Wananchi kuchangia damu kwa hiari kwani kuna hali mbaya katika hospitali ya Wilaya kuwa na upungufu Mkubwa wa damu salama.

Matomora ameyasema hayo kwenye kikao cha Robo ya tatu cha Baraza la Madiwani, kikao kilichofanyika April 30, Mwaka huu katika ukumbi Mkubwa wa Mikutano wa Halmashauri hiyo.

Matomora akieleza zaidi amesema Jamii ndiyo chanzo cha Damu na hakuna chanzo kingine hivyo kuna umuhimu kwa Wananchi kwenda kuchangia Damu kwenye vituo vyetu vya afya na Zahanati kwani Damu hizohizo zitakuja kuwasaidia wao wenyewe pamoja na Wananchi wengine ambao watahitaji huduma ya damu salama.

" Naomba nitoe taarifa ya hali ya damu salama katika Hospitali yetu na vituo  vyetu vya afya kuwa si shwari kwani katika Hospitali yetu ya Wilaya mpaka asubuhi hii  Damu salama iliyopo ni chupa 24 tu na tuna chupa  33 pekee za damu ambazo bado zinafanyiwa uchunguzi "- Amesema.

" Na katika chupa hizo 24 za Damu salama, ina makundi yale manne ya damu A, B, AB na kundi O na haya yana positive na Negative. Damu tuliyonayo ni positive tu. Kundi A tuna chupa 4,peke yake, A+, B+ tuna chupa 3 pekee na O tunazo  chupa 7 pekee" Amefafanua DED Matomora.

Aidha Mkurugenzi huyo amesema kuwa, Damu za kundi la negative hakuna hata moja kwani akipatikana mgonjwa au wagonjwa wanaohitaji makundi ya damu hizo itakuwa ni shida, hivyo wito wangu kwa Wananchi ni kujitolea kwa hiari  kutoa damu ili baadaye iweze kuwasaidia Wa Tanzania.


Tangazo

  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI June 05, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • DC MWENDA ATEMBELEA MRADI WA UJENZI WA SHULE MPYA YA SEKONDARI YA AMALI KITUKUTU

    May 08, 2025
  • KAMATI YA FEDHA, UONGOZI NA MIPANGO YA HALMASHAURI YA WILAYA YA IRAMBA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO

    May 06, 2025
  • DC MWENDA ATOA WITO KWA WALIMU WA SHULE ZA MSINGI KUIMARISHA UFUNDISHAJI KWA MADARASA YA MITIHANI

    May 06, 2025
  • JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI WILAYANI IRAMBA LATOA ELIMU YA KINGA DHIDI MAJANGA YA MOTO KWA MADIWANI NA WANANCHI

    May 02, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.