• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba Monica Samweli aizawadia Jumuiya ya Maji Nguvumali Pikipiki

Posted on: June 24th, 2021

Hemedi Munga Irambadc

irambadc@singida.go.tz

Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba Monica Samweli ameitunuku pikipiki Jumuiya ya Maji ya kijiji cha Nguvu Mali kata ya Ndago Wilayani Iramba Mkoa wa Singida.

Monica ameitunuku pikipiki hiyo leo June 24, 2021 katika hafla fupi iliyofanyika ukumbi Mkubwa wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba mjini Kiomboi.

Akiongea na Jumuiya za maji katika hafya hiyo, Monica amewataka wanajumuiya hizo kutumia mafunzo mbalimbali waliyoyapata kuhakikisha wanasimama imara kutoa huduma ya maji katika maeneo yao.

“Niziagize kamati zote za maji kuacha migongano ya kimaslahi na kujikita kutoa huduma ya maji kwa wananchi waliopo katika maeneo yao “ amesisitiza Monica

Katika hatua nyingine amezitaka Kamati za maji kujiamini na kuwa waadilifu katika kutekeleza miradi ya maji iliyopo katika maeneo yao ili kumtua mama ndoo ya maji kichwani kwa kupata maji safi na salama kwa wakati.

Akiongea na jumuiya hizo, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo, Linno Mwageni ameziagiza kamati zote za maji wilayani humo kupanda miti na kusafisha eneo lolote lililochimbwa kisima cha maji.

“Niziagize Jumuiya za Maji kuhakikisha sehemu zilizochimbwa visima mita 60 za kila upande toka katika eneo hilo zinakua safi na zimepandwa miti rafiki” ameagiza Mwageni na kuongeza kuwa

“ Jumuiya za maji zinawajubu wa kuhakikisha zinalinda na kutunza miundombinu na vyanzo vya maji katika maeneo yao.”

Aidha amemuagiza meneja wa Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) wilayani humo kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora ya maji kupitia miradi inayotekelezwa ngazi zote.

Pia ameitaka RUWASA kuwa na utaratibu wa kutoa zawadi kwa jumuiya zinazofuata kanuni na taratibu za uendeshaji wa jumuiya hizo, hivyo zikaweza kutoa huduma bora na kuikuza miradi hiyo.

Akitoa tarifa fupi ya hali ya upatikanaji wa huduma ya maji safi na salama  kwa wananchi, Meneja wa  Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) wilayani humo, Ezra Mwacha amesema kuwa upatikanaji wa maji kwa wananchi umefikia asilimia 59.6 kupitia visima virefu na vifupi na kufanikiwa kujenga skimu 32 zinazotoa hudama ya maji katika vijiji mbalimbali.

Mwacha amesema RUWASA ilipokea 1.3 bilioni kwa mwaka wa fedha uliopita kwa ajili ya miradi ya maji na kufanikiwa kukamilisha mradi wa maji Ujungu, Mgela, Kyalosangi na Songambele.

Pia amesama kwa mwaka wa fedha unaofuata RUWASA imepanga kutekeleza miradi 10, tayari vibali vya utekelezaji wa miradi hiyo kwa kijiji cha Maluga, Kisiriri na Zinziligi vimeishapatikana na kazi inaendelea.

Kufuatia utekelezaji majukumu mzuri kwa uwazi na kwa kuzingatia kanuni na taratibu za uendeshaji wa jumuiya za maji, Mwacha ameizawadia Jumuiya ya Maji Nguvu Mali pikipiki aina ya TVS yenye namba za usajili STL 9283 yenye thamani ya shilingi milioni 3.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Jumuiya ya Maji Nguvu Mali, Kristina Msengi ameishukuru RUWASA kwa kuwapatia zawadi ya pikipiki ambayo itatatua changamoto ya kuwafikia wateja wao kusoma mita na kufanya ukarabati.

Pia amezitaka jumuiya nyingine kufanya kazi kwa ufanisi, uaminifu, uadilifu, uwazi na ushindani wa kujitoa kuitumikia jamii yao.

MWISHO


Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba Monica Samweli akiwa na Meneja wa Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) Ezra Mwacha kulia kwake na kushoto ni Mwenyekiti wa Kamati ya Huduma za Jamii ya Halmashauri hiyo Peter John wakifuatilia mada ya Usimamizi wa miradi na utoaji wa taarifa, uendashaji wa Matengenezo wa Mitambo katika utoaji wa huduma za maji na Usimamizi wa fedha na ujuzi wa utunzaji wa vitabu. Picha na Hemedi Munga

Baadhi ya wanajumuiya za maji wakifuatilia kwa makini mada ya Usimamizi wa miradi na utoaji wa taarifa, uendashaji wa Matengenezo wa Mitambo katika utoaji wa huduma za maji na Usimamizi wa fedha na ujuzi wa utunzaji wa vitabu. Picha na Hemedi Munga

Pikipiki alioyoitoa Meneja wa Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) Ezra Mwacha, kuizawadia Jumuiya ya Maji Nguvu Mali pikipiki aina ya TVS yenye namba za usajili STL 9283 yenye thamani ya shilingi milioni 3. Picha na Hemedi Munga

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • KIDATO CHA KWANZA KURIPOTI SHULE January 13, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • MAAFISA ELIMU KATA 136 MKOANI SINGIDA WAPATIWA MAFUNZO KUHUSU USIMAMIZI WA SHULE NA UJAZAJI TAKWIMU KATIKA MFUMO WA "SIS"

    March 24, 2025
  • DC MWENDA AWASISITIZA WALIPA KODI KUFANYA MAKADIRIO YA KODI KABLA YA MACHI 31, 2025

    March 20, 2025
  • DC MWENDA NA WAZIRI MWIGULU NCHEMBA WACHANGIA JUMLA YA MADAWATI 98 SHULE YA MSINGI MSANSAO ILIYOPO KATA YA MTEKENTE

    March 10, 2025
  • WALIMU WAKUU 108 WA SHULE ZA MSINGI NA MAAFISA ELIMU KATA 20 WILAYANI IRAMBA WAPEWA MAFUNZO ENDELEVU YA USIMAMIZI WA UFUNDISHAJI NA UJIFUNZAJI FANISI KUPITIA JUMUIYA ZA KUJIFUNZA ZA WALIMU WAKUU NA MAAFISA ELIMU KATA

    March 19, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.