• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba, Samwel Shillah akiwaasa Viongozi kutunza siri wakati wakuwaapisha leo kata ya Ulemo Tarafa ya Kinampanda Wilayani Iramba. Picha na Hemdi Munga

Posted on: December 2nd, 2019

By Hemedi Munga, Irambadc

tehama@irambadc.go.tz

Iramba. Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba, Samweli Shillah  amewaasa viongozi walioapishwa kutunza siri za mambo mbalimbali wanayojadili kabla ya kupitishwa.

 

Shillah ameyasema hayo leo Jumatatu Disemba 2, 2019 wakati wa kuhitimisha zoezi la kuapisha viongozi kata ya ulemo Tarafa ya Kinampanda Wilayani Iramba.

Akiongea katika hadhara hiyo Makamu Mwenyekiti  wa Halmashauri hiyo amewataka viongozi walioapishwa kubadili tabia walizokuwa nazo kabla ya kuchaguliwa nakuwa na tabia nzuri kwa kuwa wao ni viyoo vya jamii inayowazunguka.

“ Ukiwa kiongozi ulevi wa kupindukia haufai maana sisi ni barua tunayosomwa na wananchi  kila siku, lazima tubadilishe tabia zetu,” alisisitiza Shillah

 

Pia amewataka kutimiza majuku yao ipasavyo kwa kuwa wamepewa zamana ya kuongoza wananchi ambao wamewaamini kuwapa nyazifa hizo.

Akiawaapisha viongozi hao, Hakimu Mkazi wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba, Sydney Nindi amewaeleza viongozi hao kuwa waaminifu kuitumikia vyema na kwa moyo thabiti Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kuhakikisha wanatunza siri za majukumu yao.

Nindi amewasisitiza viongozi hao kuwa watiifu na waadilifu wa sheria za Tanzania na Maadili ya Viongozi wa Umma ili kuleta usawa na maendeleo katika jamii zao.

Pia amewakumbusha kuwa kiongozi ni pamoja na kusikiliza maelekezo wanayopewa na viongozi wao ili kuweza kuwaongoza wananchi kwa kuzingatia misingi ya utawala bora.

Kwa upande wake   Kaimu Msimamizi wa Uchaguzi Wilayani humo amewaambia viongozi hao wachape kazi huku akiwabainishia kuwa endapo watakwenda kinyume na maadili, uaminifu na utiifu wa kanuni, taratibu na miongozo, sheria itachukuwa mkondo wake kwa kuwa sheria ni msumeno unaokata kote.

Aidha amewaagiza viongozi hao kuhakikisha wanafunzi wote wa shule za awali, shule za msingi na wale waliochaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza wanakwenda shule huku akiwataka wawachukulie hatuwa wale watakaokiuka maagizo hayo.

Kuziwia  vifo vya akinamama wajawazito na watoto wachanga kwa kuhakikisha wanakuwa na taarifa zao na kuwaelimisha kufika hospitali mapema pindi wapatapo ujauzito.

Viongozi hao wametakiwa kufahamu kuwa serikali inaanzia kwao na sio wilayni, hivyo wameaswa kuhakikisha wanatatua kero za wananchi na sio kusubiria viongozi kutoka wilayani.

Zoezi la kuapisha wenyeviti wa vijiji, vitongoji, wajumbe mchanganyiko na wajumbe kundi la wanawake lilianza Novemba 30, na kuhitimishwa Disemba 2, 2019 ambapo viongozi wakata 20 wameapishwa.                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                  

Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Wilaya ya Iramba, Sydney Nindi kushoto aikwa na Kaimu Msimamizi wa uchaguzi katikaki na kulia ni Aro Jimbo wa Uchaguzi wakati wakuwaapisha viongozi mbalimbali. Picha na Hemedi Munga                     

Baadhi ya viongozi wa vijiji , vitongoji, wajumbe mchanganyiko na wajumbe kundi la wanawake wakiapishwa kuitumikia vyema na kwa moyo thabiti Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Picha na Hemedi Munga                                                   

Baadhi ya viongozi wa vijiji , vitongoji, wajumbe mchanganyiko na wajumbe kundi la wanawake wakiapishwa kuitumikia vyema na kwa moyo thabiti Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Picha na Hemedi Munga                                                   

Hakimu Mkazi wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba, Sydney Nindi akiwaapisa baadhi ya viongozi wa vijiji , vitongoji, wajumbe mchanganyiko na wajumbe kundi la wanawake kuitumikia vyema na kwa moyo thabiti Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Picha na Hemedi Munga


Tangazo

  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI June 05, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • DC MWENDA ATEMBELEA MRADI WA UJENZI WA SHULE MPYA YA SEKONDARI YA AMALI KITUKUTU

    May 08, 2025
  • KAMATI YA FEDHA, UONGOZI NA MIPANGO YA HALMASHAURI YA WILAYA YA IRAMBA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO

    May 06, 2025
  • DC MWENDA ATOA WITO KWA WALIMU WA SHULE ZA MSINGI KUIMARISHA UFUNDISHAJI KWA MADARASA YA MITIHANI

    May 06, 2025
  • JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI WILAYANI IRAMBA LATOA ELIMU YA KINGA DHIDI MAJANGA YA MOTO KWA MADIWANI NA WANANCHI

    May 02, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.