• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba, Samwel Shillah amekipa siku 90 kikosi kazi cha Corparation Sole Surperitandents kukamilisha ujenzi wa kituo cha Afya Shelui.

Posted on: May 17th, 2020

Hemedi Munga, Irambadc

tehama@irambadc.go.tz

Iramba. Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba, Samwel Shillah amekipa siku 90 kikosi kazi cha Corparation Sole Surperitandents kukamilisha ujenzi wa kituo cha Afya Shelui.

Shillah ametoa agizo hilo mwishoni mwa wiki hii alipotembelea Kata ya Shelui akiwa na kamati ya Fedha, Mipango na Utawala wa Halmashuri ya Wilaya ya Iramba.

“Fedha tunazo, hivyo tunawaomba wenzetu wa kikosi kazi kumaliza kazi hii kwa wakati kwani hakuna kikwazo chochote,” ameagiza Shillah na kuongeza

“Tunataka baada ya muda mchache wananchi waone matokeo ya ujenzi wa Kituo cha Afya Shelui na kupata huduma za Afya.”

Shillah amefafanua kuwa Mhe, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Magufuli akishatoa fedha anataka aone matokeo kwa haraka.

“Mhe, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Magufuli akisha toa pesa, msifikirie kua hayupo hapa, ulipo tupo” amesisitiza Shillah

Halikadhalika, amewataka Wataalamu kuhakikisha wanafika eneo la mradi wa kituo cha Afya Shelui kuona mwenendo wa kazi kila siku.

Pia, amemtahadharisha Mganga Mkuu wa Zahanati ya Shelui, Alex Mpweku kuwa makini na mtulivu katika mradi huu.

“Asilimia 90% Mganga wa Zahanati ya Shelui ujenzi huu upo chini yako, hakikisha unapoandika kitu au kupitisha pesa yoyote umesoma kuanzia neno la kwanza hadi la mwisho na unapoona kua umechoka usifanye kazi hii,” amesisitiza Shillah na kuongeza

“Ninakuomba uwe mtulivu katika mradi huu, ili mwisho wa siku uweze kufika mbali maana mradi huu unaweza kukupandisha  au kukushusha cheo.”

Amemtaka Mganga huyo kufaham kuwa changamoto zitakua nyingi pamoja na  maelekezo mbalimbali kutoka kwa viongozi mbalimbali.

“Angalia mliyokubaliana, tembea kwenye mstari, mtu akitaka kubadilisha neno mwambie alete kwa maandishi ili kesho na keshokutwa unatoa nyaraka, lakini mimi nikija na kukwambia vunja hapa na ukavunja, fahamu kuwa gerezani utakwenda peke yako maana kazi za serikali zinafanyika kwa maandishi,” amesisitiza Shillah

Katika hatua nyingine,Makamu Mwenyekiti huyo amewataka Wanakamati wa ujenzi wa kituo cha Afya Shelui kuenedelea kushirikiana katika ujezi huo ili uende kwa haraka nakufanikisha kukamilisha kituo hicho ili kiweze kutoa huduma kwa wananchi.

 

Mapema akiwasilisha taarifa ya ujenzi wa kituo hicho, Mganga Mkuu wa Zahanati ya Shelui, Alex Mpweku amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Magufuli kwa kutoa Tshs 400milioni za kujenga kituo cha Afya Shelui.

Pia, amemshukuru Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo, Linno Mwageni kwa kukubali kuchangia Tshs 32.1milioni ili kuhakikisha mradi huu unakamilika kwa wakati huku ukitumia jumla ya Tshs 400.38milioni chini ya Kikosi kazi cha Corparation Sole Surperitandents.

Mpweku amebainisha kuwa Kikosi Kazi kilianza rasmi kazi Mei 01, 2020 kwa kusafisha eneo ambalo yatajengwa majengo matano na kwa sasa kipo katika hatua ya ufyatuaji wa tofari.

 

Mpaka mradi unakamilika majengo matano yanatarajiwa kujengwa ambayo ni jengo la mama na mtoto, jengo la upasuaji (theater), nyumba ya mtumishi, jengo la kufulia (laundry), jengo la kuhifadhia maiti(mortuary) na jengo la maabara (laboratory).

Akichangia maoni Diwani wa kata ya Shelui na Mjumbe wa Kamati ya Fedha, Mipango na Utawala, Omary Kinota amewakumbusha Wanakamati wa ujenzi huo kuhakikisha wanavaa barakoa ili kuhakikisha wanajilinda na maambukizi ya homa kali ya mapafu inayosababishwa na virusi vya corona.

Kinota amemtahadharisha Injinia wa Halmashauri hiyo kuwa makini na ardhi ya Shelui.

“Nikuombe Injinia kuhakikisha unafuata maelekezo yanayotakiwa, ardhi ya Shelui sio salama na sio rafiki kwa majengo, hivyo tukilemaa tukaamini kuwa ni sawasawa na sehemu nyingine kwa kweli tutapata hasara,” amefafanua Kinota

MWISHO

Diwani wa kata ya Shelui na Mjumbe wa Kamati ya Fedha, Mipango na Utawala wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba, Omary Kinota (JB) akimtahadharisha Injinia wa Ujenzi wa Kituo cha Afya Shelui kua makini na ardhi ya Shelui. Picha na Hemedi Munga

Mganga Mkuu wa Zahanati ya Shelui, Alex Mpweku akisoma taarifa fupi ya ujenzi wa kituo cha Afya Shelui mbele ya Kamati ya Fedha, Mipango na Utawala. Picha na Hemedi Munga

Wajumbe wa kamati ya ujenzi wa kituo cha Afya Shelui wakisikiliza kwa makini maagizo ya Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba, Samwel Shillah alipofanya ziara akiwa na Kamati ya Fedha, Mipango na Utawala kata ya Shelui kuangalia maendeleo ya ujenzi wa kituo cha Afya Shelui. Picha na Hemedi Munga


Tangazo

  • WAHI NAFASI YA AJIRA August 19, 2021
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2018 HALMASHAURI YA WILAYA IRAMBA January 05, 2019
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA KIDATO CHA PILI (FTNA) 2018 January 05, 2019
  • TANGAZO LA KULIPA KODI YA ARDHI. February 26, 2018
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • DC MWENDA AONGOZA ZOEZI LA UPANDAJI MITI WAPANDA MITI 3500 KATA YA MGONGO

    March 09, 2023
  • PIKIPIKI SITA ZAKABIDHIWA KWA WATENDAJI WA KATA.

    March 09, 2023
  • MAADHIMISHO YA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI WILAYANI IRAMBA

    March 08, 2023
  • ZIARA YA WAH MADIWANI WAJUMBE WA KAMATI YA FEDHA, MIPANGO NA UTAWALA KUTEMBELEA NA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO TAREHE 23 JANUARI, 2023

    January 23, 2023
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.