• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba, Samwel Shillah amemuagiza Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo, Linno Mwageni kuufunga Mwalo uliopo kati ya Mwalo wa Doromoni na Misri mara moja.

Posted on: May 14th, 2020

Hemedi Munga, Irambadc

tehama@irambadc.go.tz

Iramba. Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba, Samwel Shillah amemuagiza Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo, Linno Mwageni kuufunga Mwalo uliopo kati ya Mwalo wa Doromoni na Misri mara moja.

                                     

Shillah ametoa agizo hilo leo Alhamisi Mei 14, 2020 kando mwa Ziwa Kitangiri Mwalo wa Doromoni alipokuwa katika ziara ya Kamati ya Fedha, Mipango na Utawala ya Halmashauri hiyo.

Akiongea na baadhi ya Wavuvi na Wenyeji waliopo kando ya Ziwa Kitangiri, Shillah amewaomba Wavuvi hao kulinda rasilimali hiyo muhimu inayoweza kukuza uchumi wao huku akiwataka kuchukua tahadhari ya maambukizi ya homa kali ya mapafu inayosababishwa na virusi vya corona.

“Niwaombe tushirikiane kulinda Ziwa hili kwa kuwa ni lakwetu na hatuwezi kufurahia samaki watokao Ziwani ikiwa sisi ni wagonjwa, hivyo lazima tuchukue tahadhari ya covid-19,” amesema Shillah na kuongeza

“ Muhakikishe kila anayefika hapa analipa ushuru kwa sababu ushuru huo ndio unaochangia kuleta maendeleo.”

Halikadhalika, Shillah amewaagiza watendaji wote wa kata Wilayani humo kuhakikisha wanahuisha akaunti za vijiji na kuziwasilisha ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji kwa ajili ya kufanyiwa kazi.

Mapema akiwasilisha maoni yake mjumbe wa Kamati ya Fedha, Mipango na Utawala ya Halmashauri hiyo, Wilfredi Kizanga  Diwani wa Kata ya Tulya. ameikumbusha kamati hiyo kuwa iliahidi kujenga kizimba katika Mwalo wa Doromoni kwa ajili ya kuhifadhi boti na kuwa na wepesi wa kufanya doria.

“Ziwa Kitangiri lina umuhimu mkubwa kwa sababu ni chanzo kizuri cha mapato ya Halmashauri yetu, hivyo ninaiomba kamati hii kuhakikisha inazitatua changamoto zote ili kuongeza tija na mapato,” amesema Kizanga

Akijibu swali la ndugu Juma mmoja wa wenyeji wanaoishi kando ya Ziwa hilo aliyetaka kujua kuwa, wao kama kata au kijiji wananufaika na nini baada ya mapato kupelekwa Halmashauri?


Mwenyekiti wa Kamati ya Fedha, Mipango na Utawala ya Halmashauri hiyo, Innocenti Msengi amesema kuwa kamati hua inajadili na kuweka mikakati inayoinufaisha kata ya Kidaru na nyinginezo Wilayani humo kupitia ushuru unaopatikana baada ya kuuza  samaki wakubwa kwa wanunuzi watokao maeneo ya ndani na nje ya wilaya.

Naye Afisa Uvuvi wa Halmashauri hiyo, Deogratius Isagala amesema kuwa Ziwa Kitangiri ni rasilimali muhimu ya Wilaya ya Iramba kwa sabubu limekuwa na mchango mkubwa wa kuboresha lishe na uchumi wa Wananchi.

Amesema kuwa kumekua na changamoto ya ongezeko la uvuvi haramu katika mialo iliyopo Wilaya  jirani za Kishapu, Meatu na Igunga.

Kamati ya Fedha, Mipango na Utawala ya Halmashauri hiyo, imefanya ziara Ziwa Kitangiri lenye ukubwa wa kilometa za mraba 105 na kumalizia ziara hiyo kata ya Shelui kwenye ujenzi wa kituo cha Afya.

Ujenzi huo ulioanza baada ya kupokea fedha Tshs400 milioni kotoka kwa  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli.

 

Kupitia fedha hizo majengo matano yanatarajiwa kujengwa ambayo ni jengo la mama na mtoto, jengo la upasuaji (theater), nyumba ya mtumishi, jengo la kufulia (laundry), jengo la kuhifadhia maiti(mortuary) na jengo la maabara (laboratory).

MWISHO

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba, Linno Mwageni akiwaagiza wavuvi wote kuhakikisha mgeni yoyote atakayefika Ziwani hapo anasajiliwa ili atambulike anakotoka kwa ajili ya kuchukua tahadhari ya maambukizi ya homa kali ya mapafu inayosababishwa na virusi vya corona. Picha na Hemedi Munga

Waheshimiwa Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba wakiwa wameshika samaki watokao Ziwa Kitangiri walipo fanya ziara Mei 14, 2020 Ziwani Hapo. Wakati kati ni Mh, Ester, nyuma yake ni Mh, Innocenti Msengi na Mbele yake ni Mh, Wilfredi Kizanga Picha na Hemedi Munga

Kaimu Mweka Hazina wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba, Hadhiri Ngayunga alipotembelea Ziwa Kitangiri kukagua ukatishaji wa ushuru utokanao na samaki wa Ziwa hilo. Picha na Hemedi Munga

Mvuvi akiwa na baadhi ya wanunuzi punde baada ya kuwasili toka kuvua katika Ziwa Kitangiri. Picha na Hemedi Munga

Samaki aina ya Pelege waliovuliwa toka Ziwa Kitangiri. Picha na Hemedi Munga


Tangazo

  • WAHI NAFASI YA AJIRA August 19, 2021
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2018 HALMASHAURI YA WILAYA IRAMBA January 05, 2019
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA KIDATO CHA PILI (FTNA) 2018 January 05, 2019
  • TANGAZO LA KULIPA KODI YA ARDHI. February 26, 2018
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • DC MWENDA AONGOZA ZOEZI LA UPANDAJI MITI WAPANDA MITI 3500 KATA YA MGONGO

    March 09, 2023
  • PIKIPIKI SITA ZAKABIDHIWA KWA WATENDAJI WA KATA.

    March 09, 2023
  • MAADHIMISHO YA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI WILAYANI IRAMBA

    March 08, 2023
  • ZIARA YA WAH MADIWANI WAJUMBE WA KAMATI YA FEDHA, MIPANGO NA UTAWALA KUTEMBELEA NA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO TAREHE 23 JANUARI, 2023

    January 23, 2023
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.