Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe Hemed Suleiman Abdulla amefungua Kikao Kazi cha 20 cha Maafisa Habari, Mawasiliano, Itifaki na Uhusiano Serikalini katika ukumbi wa Mikutano wa New Amani Hotel Zanzibar.
Akifungua Kikao Kazi cha 20 Mjini Unguja kwa niaba ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe Dkt Hussein Ali Mwinyi, Makamu huyo amewataka Maafisa Habari nchini kutoa mrejesho kwa wananchi kwa kazi zinazotekelezwa na Serikali kuelekea Uchaguzi Mkuu.
" Taarifa za miradi inayotekelezwa na Serikali zote mbili ziwafikie wananchi kwa wakati ili waweze kufanya tathmini ya taarifa za kina za utekelezaji wa miradi ili waweze kufanya maamuzi kuelekea Uchaguzi Mkuu " Amesema Mhe Hemed Suleiman Abdulla.
KIOMBOI, IRAMBA
Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA
Simu: 026 - 2532253
Simu: 026 - 2533001
Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz
Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.