• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Mhe, Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Emmanuel luhahula amefanya ziara kata ya Ndulungu Tarafa ya Ndago leo tarehe 19/03/2019

Posted on: March 19th, 2019

Mhe, Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Emmanuel Luhahula,

 amefanya ziara leo tarehe 19.03.2019 katika Tarafa ya

 Ndago kata ya Ndulungu.


 Mhe, Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Emmanuel Luhahula,

akihutubia katika mkutano wa hadhara amemuagiza

 Kaimu OCD Mkuu wa Kituo cha Polisi Ndago,

Rashidi Mchonvu kuwakamata wale wote waliouza

 na walionunua Gala la Ushirika nakubomoa nyumba

 iliyojengwa katika kiwanja cha serikali.

“Nimetengeneza tume kwenye Wilaya kuangalia na

 kuhakiki mali za Ushirika, Ndulungu Gala la

Ushirika mmeliuza, Gala la Ushirika limeliwa,

 haya ni maelekezo wala sio ombi, Kaimu OCD

 kamata wote waliouza hilo Gala pamoja na

 aliyenunua Gala, na eneo la kiwanja libaki

 wazi kwenye Ushirika, sitaki maelezo katika

 hilo, wote wawajibike, hatuwezi tukachezea mali

 za Ushirika na nipate taarifa kabla sijamaliza

 ziara yangu kwenye Tarafa hii, hao watu

wamekwisha kamatwa wote na nimepita

nimeangalia sehemu zingine wamejenga ibomolewe

 hiyo nyumba, hatuwezi tukachezea maeneo

 ya serikali, sio tu la Ushirika na kama

 kuna mtu yuko kwenye eneo la serikali

  amevamia lazima aondoke,” amesema.


Mhe, Mkuu wa Wilaya, Emmanuel Luhahula

 amemuagiza Afisa Tarafa, Gerege Kingu,

kuwashirikisha wazazi na kuwaelemisha maana

 halisi ya Elimu bila malipo na kuhakikisha

 watoto wote wanakwenda shule na wanakula chakula.

“Simamieni suala la utoro na hakikisheni watoto

wote wanakwenda shule, hakikisheni watoto wote

wanakula chakula shuleni, watoto lazima wale

 sio ombi kwenye vijiji vyote,

ninatumia mamlaka kuagiza hili

 na sio ombi watoto lazima wale. Hakikisheni

 wananchi mnatunza chakula, kulima mazao

 mengine yanayokabiliana na hali hii,

mwenye mfugo avune na kununua chakula maana

 ni fedhea sana familia kukosa chakula.

Tusimamieni nidhamu, kuheshimiana viongozi

 wote wa serikali na hakikisheni mnatekeleza wajibu

 wenu kwa kufanya kazi,” amesema


Mhe, Mkuu wa Wilaya amewaambia wananchi kua

 tumejipanga kusajili watoto 20,000 wenye umri

 chini ya miaka mitano ili wapate vyeti vya kuzaliwa,

 mpaka sasa tumekwisha sajili zaidi ya watoto 11,000.

“Simamieni upatikanaji wa cheti cha kuzaliwa na

 hakikisheni mnakitunza maana ukipoteza utalazimika

 kutoa garama kukipata ofisi ya Mkuu wa Wilaya.

Amewaomba viongozi kusimamia ugawaji wa

vitambulisho vya mjasiriamali ili viishe, kufanya

 hivyo tutakua tunaunga mkono juhudi za Mh Rais,

Daktari John Joseph Magufuli,” amesema

Mhe, Mkuu wa Wilaya amewaambia wananchi kua

 Ndulungu bila Rushwa inawezekana na huo ndio

 ulinzi na usalama, kwa hivyo wenyeviti wa kamati

 ya Ulinzi na Usalama kuanzia ngazi ya kijiji hadi

 wilayani kusimamia kutokomeza rushwa.


Naye Mkuu wa Takukuru Wilaya ya Iramba,

 Pachal Lufungulo amewaelimisha wananchi kua

 rushwa ni kitu chochote mtu anapewa ili atekeleze

 jambo fulani kwa upendeleo, rushwa ni adui wa haki,

 rushwa ni kosa la jinai, rushwa ni dhambi na kuwataka

 wananchi watakapo ombwa rushwa watoe taarifa

Takukuru, Polisi au kwa Mkuu wa Wilaya.

Mhe, Mkuu wa Wilaya amewaomba wenyeviti wa

vitongoji wote na mabalozi kusimamia na kuimarisha

 madaftari ya wageni ili kuahakikisha tunatokomeza

uhamiaji haram.


Akizungumza kwenye mkutano huo kaimu Kamanda

 wa Uhamiaji, Insepekta Collins Soka, amesema

Mhamiaji haramu ni raia wa kigeni anayeingia

 nchini na kuendelea kuishi nchini bila kufuata

 taratibu na sharia za uhamiaji, au anayeingia

 nchini kwa mujibu wa sharia za uhamiaji lakini

 akaendelea kuishi nchini kinyume na sharia,

kanuni na taratibu.


“Amewataka wananchi kutoa taarifa kwenye ofisi

za Uhamiaji, kituo cha Polisi, au serikali za mitaa

 pindi unapohisi kuwepo wahamiaji haramu mahali

 popote. Ushiriki wako katika kuwafichua wahamiaji

 haramu ni muhimu sana katika kuimarisha ulinzi,

usalama na maendeleo ya nchi,” amesema

Naye Luhende Masangwa mkazi wa Makungi

 kijiji cha kipuma Kata ya Ndulungu, amemshukuru

 Mkuu wa Wilaya, Emmanuel Luhahula kwa ziara

 yake iliyoweza kuwazindulia jengo la shule shikizi

 na kuahidi kuja kulifungua mwaka huu.


Rozi John mkazi wa Makungi kijiji cha kipuma Kata

 ya Ndulungu, amefurahi ujio wa Mkuu wa Wilaya,

 Emmanuel Luhahula katika ziara yake kwani utasaidia

 kuharakisha ujenzi wa shule shikizi iishe haraka

 na watoto watu kusomea karibu.

Habari na Hemedi Munga.

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • KIDATO CHA KWANZA KURIPOTI SHULE January 13, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • MAAFISA ELIMU KATA 136 MKOANI SINGIDA WAPATIWA MAFUNZO KUHUSU USIMAMIZI WA SHULE NA UJAZAJI TAKWIMU KATIKA MFUMO WA "SIS"

    March 24, 2025
  • DC MWENDA AWASISITIZA WALIPA KODI KUFANYA MAKADIRIO YA KODI KABLA YA MACHI 31, 2025

    March 20, 2025
  • DC MWENDA NA WAZIRI MWIGULU NCHEMBA WACHANGIA JUMLA YA MADAWATI 98 SHULE YA MSINGI MSANSAO ILIYOPO KATA YA MTEKENTE

    March 10, 2025
  • WALIMU WAKUU 108 WA SHULE ZA MSINGI NA MAAFISA ELIMU KATA 20 WILAYANI IRAMBA WAPEWA MAFUNZO ENDELEVU YA USIMAMIZI WA UFUNDISHAJI NA UJIFUNZAJI FANISI KUPITIA JUMUIYA ZA KUJIFUNZA ZA WALIMU WAKUU NA MAAFISA ELIMU KATA

    March 19, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.