• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Milioni Moja Laki mbili zachangwa kusaidia ununuzi wa vifaa vya kujikinga na maambukizi ya homa kali ya mapafu inayosababishwa na virusi vya corona.

Posted on: April 28th, 2020

Hemedi Munga, Irambadc

tehama@irambadc.go.tz

Iramba. Wadau mbalimbali wa maendeleo Wilayani Iramba wamechanga Tsh1.2milioni kusaidia ununuzi wa vifaa vya kujikinga na maambukizi ya homa kali ya mapafu inayosababishwa na virusi vya corona.

Mchango huo umetolewa leo Jumanne Aprili 28, 2020 mbele ya Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Emmanuel Luhahula alipokutana na Wadau hao wa maendeleo katika ukumbi Mkubwa wa Halmashauri mjini hapa.

Katika kikao hicho ahadi mbalimbali zimetolewa huku Tsh 6.2milioni zikiahidiwa kutolewa ndani ya siku chache zijazo.

Aidha wadau hao wa maendeleo wametakiwa kulipa pesa hizo kupitia akaunti ya Iramba District Council MIS Deposit 50610000793.

Kufuatia michango hiyo,Mkuu wa Wilaya hiyo, Emmanuel Luhahula amewashukuru Wadau hao wa maendeleo kwa kutoa michango yao ili kuisaidia jamii ya Wanairamba.

Pia, amewataka Wadau hao wa maendeleo kuwa mabalozi wa kuwafikishia taarifa Wafanya biashara wote ili waweze kushiriki kuchangia.

“ Niwaombe wafanya biashara mliopo hapa kufikisha ujumbe kwa wengine maana ninataka wafanya biashara wote wa Iramba washiriki kuchangia,” amesisitiza Luhahula

 

Luhahula amewataka watumishi wa Serikali kuwa waaminifu pindi watakapokua wanakusanya hizo pesa.

 

“Nikigundua Mtumishi wa Serikali amekwenda kuchangisha kwenye duka akapata  elfu ishirini (20,000), au laki moja (100,000) halafu  akazila, Ninakuhakikishia Mkurugenzi Mtendaji kuwa Mtumishi huyo hatokua na kazi,” amesisitiza Luhahula

Kwa upande wake Katibu wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Ibrahimu Mjanaheri amewakumbusha Wadau hao wa maendeleo kutumia nguvu za kiuchumi ili kusaidia kuwalinda wanairamba dhidi ya maambukizi ya virusi vya corona.

“Tuhakikishe tunakua na juhudi za kuiokoa Iramba na Wanyiramba na sisi ambao tuko ndani yake,” amesema Mjanaheri na kuongeza

 

“Ninataka jambo hili tulifanye la kufa na kupona na sio kubembelezana wakati ni jambo ambalo linaweza kupoteza uhai wa watu na tunanguvu za kujiokoa, lazima tujiokoe.”

Akitoa taarifa pufi mbele ya Wadau hao wa maendeleo, Mganga Mkuu wa Halmashauri hiyo, Daktari Hussein Sepoko amesema kuwa watu 170 wamepata mafunzo ya namna ya kupambana na kujikinga na maambukizi ya homa kali ya mapafu inayosababishwa na virusi vya corona kupitia Wizara ya Afya.

Amefafanua kuwa waliopata mafunzo hayo ni wakufunzi 8 ambao waliweza kuwafundisha Watumishi wote wa Idara ya Afya, Waganga Wafawidhi wa Vituo vya Afya, Madereva wote, Wafagiaji na Walinzi wote.

Naye mmoja wa Wadau hao wa maendeleo, Muwakilishi wa Kampuni ya Sun Shine iliyopo kijiji cha Konkilangi Wilayani humo, ameiomba ofisi ya Mkuu wa Wilaya hiyo kuziandikia barua kampuni zote kiwango kinachohitajika kwa ajili ya ununuzi wa vifaa vya kujikinga na maambukizi ya homa kali ya mapafu inayosababishwa na virusi vya corona.

Kikao cha Wadau wa Maendeleo kimefanyika kikiwa na lengo la kuhakikisha wanawailinda wananchi kwa kuwa wao ndio wanaonufaika na wananchi, napindi watakapo ugua watawakosa wateja hao.

Na hii ni kwa sababu  kuwa ugonjwa huu hauchagui cheo cha mtu , awe Mkuu wa Wilaya, masikini, tajiri, msomi au asio msomi, hivyo kila mmoja aguswe na kuona namna atakavyochaingia.

MWISHO

Katibu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilayani Iramba awataka wadau wa maendeleo kutoa nguvu za kiuchumi ili kuisaidia jamii ya Wanyiramba kuepukana na maambukizi ya homa kali ya mapafu inayosababishwa na virusi vya corona. Picha na Hemedi Munga

Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba, Daktari Hussein Sepoko akitoa taarifa kwa Wadau wa Maendeleo namna ya kujikinga na maambukizi ya homa kali inayosababishwa na virusi vya corona. Picha na Hemedi Munga

Katibu Tawala wa Wilaya ya Iramba aliosimama, Pius Songoma akimkaribisha Mkuu wa Wilaya hiyo, Emmanuel Luhahula kufungua kikao cha Wadau wa Maendeleo kujadili namna bora ya kuchangia upatikanaji wa vifaa vya kujikinga na maambukizi ya homa kali ya mapafu inayosababishwa na virusi vya corona. Picha na Hemedi Munga


Tangazo

  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI June 05, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • DC MWENDA ATEMBELEA MRADI WA UJENZI WA SHULE MPYA YA SEKONDARI YA AMALI KITUKUTU

    May 08, 2025
  • KAMATI YA FEDHA, UONGOZI NA MIPANGO YA HALMASHAURI YA WILAYA YA IRAMBA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO

    May 06, 2025
  • DC MWENDA ATOA WITO KWA WALIMU WA SHULE ZA MSINGI KUIMARISHA UFUNDISHAJI KWA MADARASA YA MITIHANI

    May 06, 2025
  • JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI WILAYANI IRAMBA LATOA ELIMU YA KINGA DHIDI MAJANGA YA MOTO KWA MADIWANI NA WANANCHI

    May 02, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.