• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba awafunda viongonzi wa Vijiji, Mitaa na Vitongoji walioapishwa leo . Picha na Hemedi Munga

Posted on: November 30th, 2019

By Hemedi Munga, Irambadc

tehama@irambadc.go.tz

Iramba. Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba, Linno Mwageni amefungua rasmi zoezi la kuwaapisha viongozi waliochaguliwa katika uchaguzi wa serikali za mitaa.

Mwageni amefugua uapishaji huo leo Jumamosi Novemba 30, 2019 kata ya Shelui Tarafa ya Shelui Wilayani humo.

Ambapo wenyeviti wa vijiji, wenyeviti wa vitongoji, wajumbe mchanganyiko na wajumbe kundi la wanawake wameapishwa kiapo cha uaminifu na kile cha utii na uadilifu.

 Katika ufunguzi huo Mwageni amewaambia viongozi walioapishwa kuwa wanatakiwa kuainisha rasilimali, fursa zilizopo na changamoto ndani  ya kitongoji na namna ya kutumia rasilimali zilizopo kutatua changamoto zao ambapo ndio utekelezaji wa ugatuaji wa madaraka ulioboreshwa unaotaka mipango yote ya maendeleo kila watu wanaanza kujipanga kadri wanavyoishi.

Huku akiwataka wawe viongozi wenye kuhamasisha shughuli za maendeleo kwa sababu itasaidia kupatikana  ajira kwa vijana wetu.

“ Msiwe viongozi wa kubeza shughuli za maendeleo mkawe viongozi wa kuhamasisha shughuli za maendeleo” alisisitiza Mwageni

 

Hata hivyo Mwageni amewakataza viongozi hao kuingia mikataba na wawekezaji waliopo katika maeneo yao  bila kushirikisha uwongozi wa wilaya ili uweze kuwasaidia kuingia mikataba yenye tija.

Amewataka viongozi hao kusimamia makusanyo ya serikali za vijiji na kuhakikisha pesa zinakwenda benki katika akaunti za vijiji.

Akiwaapisha viongozi hao Hakimu wa Mahakama ya Mwanzo Shelui, Egdius Byabajuka amewataka kuwa waaminifu, watiifu na waadilifu wa majukumu yao huku akiwakataza kuvunja ndoa za wananchi wao kwa kuwa chombo chenye mamlaka ya kuvunja ndoa ni mahakama na sio wao.

Naye msimamizi wa uchaguzi jimbo la Iramba Magharibi, Salumu Sefu amewaagiza wasimamizi wasaidizi ngazi ya kata kusimamia zoezi la makabidhiano kati ya viongozi walioapishwa na wale waliomaliza muda wao ili waanze kazi mara moja kwa kuwa tayari wameishaapishwa.

Kwa upande wake Afisa wa kuzuwia na kupambana na rushwa wilayani humo  (TAKUKURU ), Benjamini Masyaga  amewaelimisha viongozi hao kujiepusha na vitendo vya rushwa huku akiwataka kuwa mtsari wa mbele kutoa taarifa kila wanapoona viashiria vya rushwa katika jamii yao.

Aidha amewataka kufahamu miradi na pesa yoyote inayoletwa katika vijiji vyao kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo na kuwataka kusoma mapato na matumizi.

Uapishaji huo umefanyika katika kata ya Shelui, Mgongo, Ntwike, Tulya  na Mtoa kwa tarafa ya Shelui wakati tarafa ya Ndago umefanika katika kata ya Mukulu, Ndago, Mbelekese na Kaselya.

Huku ukitarajiwa kuendelea jumapili kwa kata zilizobakia katika tarafa ya Shelui na ndago na kuhitimishwa siku ya juma tatu katika tarafa ya Kisiriri na Kinampanda.

Uchaguzi wa serikali za Mitaa ulifanyika Novemba 24, 2019 na kutangazwa  matokeo ya uchaguzi huo na Waziri wa Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Selemani Jaffo ambapo Chama cha Mapindizi (CCM) kiliibuka na ushindi wakishindo kwenye vijiji, mitaa na vitongoji.                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                           

Afisa wa Kuzuwia na kupambana na rushwa (TAKUKURU), Benjamini Masyaga  akiwaelimisha viongonzi wa Vijiji, Mitaa na Vitongoji walioapishwa leo kujiepusha na rushwa na kutoa taarifa ya viashiria vya rushwa TAKUKURU. Picha na Hemedi Munga                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                        

Baadhi ya viongonzi wa Vijiji, Mitaa na Vitongoji wakiapa kiapo cha uaminifu na kile cha utii na uadilifu mbele ya Hakimu wa Mahakama ya Mwanzo Shelui, Egdius Byabajuka. Picha na Hemedi Munga                                                                  

Picha ya pamoja kati ya viongonzi wa Vijiji, Mitaa na Vitongoji na wasimamisi wa uchaguzi ngazi ya wilaya ya Iramba baada ya kuapishwa. Picha na Hemedi Munga

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • KIDATO CHA KWANZA KURIPOTI SHULE January 13, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • MAAFISA ELIMU KATA 136 MKOANI SINGIDA WAPATIWA MAFUNZO KUHUSU USIMAMIZI WA SHULE NA UJAZAJI TAKWIMU KATIKA MFUMO WA "SIS"

    March 24, 2025
  • DC MWENDA AWASISITIZA WALIPA KODI KUFANYA MAKADIRIO YA KODI KABLA YA MACHI 31, 2025

    March 20, 2025
  • DC MWENDA NA WAZIRI MWIGULU NCHEMBA WACHANGIA JUMLA YA MADAWATI 98 SHULE YA MSINGI MSANSAO ILIYOPO KATA YA MTEKENTE

    March 10, 2025
  • WALIMU WAKUU 108 WA SHULE ZA MSINGI NA MAAFISA ELIMU KATA 20 WILAYANI IRAMBA WAPEWA MAFUNZO ENDELEVU YA USIMAMIZI WA UFUNDISHAJI NA UJIFUNZAJI FANISI KUPITIA JUMUIYA ZA KUJIFUNZA ZA WALIMU WAKUU NA MAAFISA ELIMU KATA

    March 19, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.