• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba, Linno Mwageni akisikiliza kero na changamoto mbalimbali za Watumishi wa Makao Makuu ya Halmashauri ya Wilaya ya Iramba Mkoani Singida na kuzitolea majibu. Kulia kwake ni Afisa Utumishi wa Halmashauri

Posted on: January 31st, 2020

Hemedi Munga, Irambadc

tehama@irambadc.go.tz

Iramba. Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba, Linno Mwageni amesikiliza kero na changamoto mbalimbali za watumishi wa Makao Makuu ya Halmashauri ya Wilaya ya Iramba Mkoani Singida na kuzitolea majibu.

Mwageni amezungumza na Watumishi hao katika kikao kilichofanyika leo Ijumaa Januari 31, 2020 katika Ukumbi Mdogo wa Halmashauri hiyo  mjini hapa.

Katika kikao hicho Mwageni  amewataka Wakuu wa Idara na Vitengo   kutenga muda kusikiliza kero na changamoto mbalimbali za watumishi waliopo katika mamlaka zao na kuzitolea majibu huku akiwaamuru kuzifikisha kwake zinaposhindikina  kwa utatuzi zaidi.

Amewasisitiza watumishi hao kutunza nyaraka za serikali na kuto kuwa na kopi au kutoka nazo nje ya Halmashauri hiyo.

“Ninawasisitiza watumishi wenzangu hasa mkirejea sheria inayohusu nyaraka ni makosa kuwa na nyaraka zilizokwisha ingizwa katika utaratibu wa Halmashauri,” amebainisha Mwageni

Pia amekemea taiba ya watumishi kubeba mafaili yao kwani kunachukua  majukumu ya watu, hivyo amemuagiza Afisa Utumishi wa Wilaya hiyo B’hango Lyangwa kushughulika na watu hao kwa mujibu wa taratibu na kanunu za utumishi wa umma.

“Ninakuagiza  Afisa Utumishi kuwachukulia hatua watumishi hao, nanyi mnaohusika na mafaili ni marufuku mtumishi kubeba faili lake,” aliongeza Mwageni

Akiongelea suala la mawasiliano amewakumbusha Watumishi hao  kuwa msemaji  katika Idara au Kitengo ni Mkuu wa Kitengo au Idara na msemaji wa taasisi ni Mkuu wa Taasisi.

Hivyo amekemea Mtumishi yoyote asie kuwa Mkuu wa Idara au Kitengo kutoa taarifa kwani kufanya hivyo ni kutengeneza migogoro.

Hata hivyo amewataka Watumishi hao kuwa makini na magrupu mbalimbali ya mitandao ya kijamii na kuacha tabia ya kufowadi taarifa yoyote usiokua na uhakika nayo.

“ Nimarufuku kutuma barua yoyote kwa njia ya magrupu na haipendezi Mtumishi wa Halmashauri hii kukutwa na makosa ya kimtandao,” amekataza Mwageni

Vile vile amewataka kuwa na tabia ya kuheshimiana, kuthaminiana na kuzibiti hasira, dharau na mihemko yao wakati wakiwahudumia wananchi au wao kwa wao.

Aidha amewaagiza Wakuu wa Idara na Vitengo kufanya tathimini  ya Watumishi waliochini yao kutoa huduma kwa kulinda muda.

Pia amewaagiza Wakuu hao kuweka vibao vinavyotoa taarifa kuwa ni marufuku kupita eneo la Halmashauri ifikapo saa  kumi na mbili jioni, siku za sikukuu na siku za mapumziko.

 

Kufuatia kua karibu na Makao Makuu ya Nchi, Mwageni amewataka Watumishi hao kutumia fursa ya kutumia ardhi kulima mazao mbalimbali na kuyapeleka Dodoma.

Kufanya hivyo kutawawezesha Watumishi hao kukuza uchumi wao kihalali.

Naye Mwenyekiti wa kamati ya kudhibiti Uadilifu katika Halmashauri hiyo, Abraham Mosi amewatahadharisha Watumishi wa Idara ya Elimu Sekondari, Elimu Msingi, Afya , Maliasili na Ardhi na kitengo cha Manunuzi kujiepusha na viashiria vya rushwa.

“Ninawaomba Watumishi wenzangu kujitahidi kua wema na waadilifu wakati wote,” amesisitiza Mosi

Awali akitoa kero yake mbele ya Mkurugenzi huyo, Elieza Kipimo amewaomba Watumishi wenzake kuepuka tabia ya kuuliza posho pindi wanapotakiwa kufanya kazi fulani.

 Naye Mtumishi mwingine kutoka Kitengo cha Manunuzi,  Omari Jumanne amewaomba Watumishi wenzake kuhuisha uhusiano wao kazini hasa pale panapojitokeza matatizo yalio nje ya taratibu za kiutumishi.

 

Pia  Mtumishi kutoka Idara ya Mifugo na Uvuvi, Deogratius Isagala amewaomba Wakuu wa Idara na Vitengo kua na fotokopia na printa katika ofisi zao kwani kufaya hivyo kutasaidia kutunza nyaraka za serikali.

Isagala amemuomba Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo kuwa na siku ya familia au siku ya iramba ( Family day or Iramba day) itakayokusanya Watumishi wote, wale, wanywe wacheze, wabadilishane mawazo na kutambulisha watumishi wapya, kupitia mfumo huo Watumishi wote watafahamiana na kudumisha upendo kati yao.                                                                                                                                                                                                                                               

Watumishi mbalimbali wa Makao Makuu wakisikiliza kwa makini maagizo ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba. Picha na Hemedi Munga                                                                                                                                             


Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • KIDATO CHA KWANZA KURIPOTI SHULE January 13, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • MAAFISA ELIMU KATA 136 MKOANI SINGIDA WAPATIWA MAFUNZO KUHUSU USIMAMIZI WA SHULE NA UJAZAJI TAKWIMU KATIKA MFUMO WA "SIS"

    March 24, 2025
  • DC MWENDA AWASISITIZA WALIPA KODI KUFANYA MAKADIRIO YA KODI KABLA YA MACHI 31, 2025

    March 20, 2025
  • DC MWENDA NA WAZIRI MWIGULU NCHEMBA WACHANGIA JUMLA YA MADAWATI 98 SHULE YA MSINGI MSANSAO ILIYOPO KATA YA MTEKENTE

    March 10, 2025
  • WALIMU WAKUU 108 WA SHULE ZA MSINGI NA MAAFISA ELIMU KATA 20 WILAYANI IRAMBA WAPEWA MAFUNZO ENDELEVU YA USIMAMIZI WA UFUNDISHAJI NA UJIFUNZAJI FANISI KUPITIA JUMUIYA ZA KUJIFUNZA ZA WALIMU WAKUU NA MAAFISA ELIMU KATA

    March 19, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.