• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba, Linno Mwageni amefanya ziara ya kukagua ukamilishaji wa Maabara 9 za kemia zinazokamilishwa katika shule 9 Wilayani Iramba Mkoa wa Singida.

Posted on: July 23rd, 2021

Hemedi Munga Irambadc

irambadc@singida.go.tz

Iramba. Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba, Linno Mwageni amefanya ziara ya kukagua ukamilishaji wa Maabara 9 za kemia zinazokamilishwa katika shule 9 Wilayani Iramba Mkoa wa Singida.

Mwageni amefanya ziara hiyo leo Ijumaa Julai 23, 2021 wakati alipotembelea baahdi ya shule 9 kukagua ukamilishaji wa maabara hizo zilizopo Wilayani hapa.

Akiongea na kamati ya manunuzi ya Shule ya Sekondari Kidaru, Mwageni amezitaka kamati zote za manunuzi katika wilaya hiyo kuwa na tabia ya kujadili miradi ya maendeleo katika vikao vyao vya kiutawala ili iwasaidie kuweza kubaini kwa haraka kama kuna changamoto na kuweza kuitafutia ufumbuzi kwa muda stahiki.

Aidha amewataka viongozi wote ambao katika maeneo yao wanamiradi ya maendeleo wanapokuwa wamepata changamoto ya usafiri wa kusafirishia vifaa vya ujenzi kufika Halmashauri mapema kupata gari litakaloweza kuwarahishia usafirishaji wa vifavaa kupeleka katika maeneo yao ya miradi.

Kwa upande wake Mkuu wa Idara ya Elimu Sekondari, Godfrey Mwanjala amesema kuwa maabara hizo zimekamilika kwa kiwango bora kinachohitajika na tayari Serikali imekwisha leta vifaa vya maabara hizo.

Mwanjala amesema kuwa Serikali kuu ilileta takriban Tst 210 milioni kwa ajili ya ukamilishaji wa maabara za kemia.

Amefafanua kuwa  maabara hizo zimekamilishwa katika shule ya Sekondari New Kiomboi, Sekondari ya Kisiriri, Sekondari ya Kidaru, Sekondari ya Mgongo, Sekondari ya Mukulu, Sekondari ya Mbelekese, Sekondari ya Mtoa, Sekondari ya Ushora na Sekondari ya Kyengege.

Pia ametowa wito kwa walimu wote kuhakikisha wanatumia weledi wao wakisaidiwa na uwepo wa maabara pamoja na vifaa vilivyopo kuhakikisha wanafunzi wananufaika kwa kupata taaluma bora itakayowawezesha kufaulu vizuri katika mitihani yao ya mwisho.

Akiongea na Mwandishi wetu Mkuu wa Shule ya New Kiomboi, Amadeus Kiduu amesema kuwa maabara ipo tayari na itaanza kutumika wakati wowote tokea sasa.

Naye Mwalimu wa shule ya Sekondari Kidaru, Leonard Mgenzi ametumia fursa ya ziara hiyo kuwaomba viongozi kuendelea kutoa elimu kwa kamati zote zinazosimamia miradi mbalmbali ili wapate ujuzi wa kusimamia kwa umakini na usahihi wa miradi hiyo.

MWISHO

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba, Linno Mwageni amefanya ziara ya kukagua ukamilishaji wa Maabara 9 za kemia zinazokamilishwa katika shule 9 Wilayani Iramba Mkoa wa Singida. Kulia ni Mkuu wa Shule ya New Kiomboi na kushoto ni Makamu Mkuu wa Shule ya New Kiomboi, Ndugu Nkololo. Picha na Hemedi Munga

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba, Linno Mwageni akiwa na baadhi ya Wakuu wa Idara pamoja na kamati mbalimbali za moja kati ya shule alizozitembelea wakati wa ziara hiyo. Picha na Hemedi Munga

Moja kati ya Maabara 9 zinazokamilishwa Wilaya ya Iramba Mkoa wa Singida kwa fedha iliyotoka Serikali kuu takribani Tsh 210 milioni. Picha na Hemedi Munga

Moja kati ya Maabara 9 zilizojengwa katika shule 9 Wilayani Iramba Mkoa wa Singida ziko tayari kuanza kutumika kwa kuwa zimekamilka kwa ubora unaohitajika . Picha na Hemedi Munga


Tangazo

  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI June 05, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • DC MWENDA ATEMBELEA MRADI WA UJENZI WA SHULE MPYA YA SEKONDARI YA AMALI KITUKUTU

    May 08, 2025
  • KAMATI YA FEDHA, UONGOZI NA MIPANGO YA HALMASHAURI YA WILAYA YA IRAMBA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO

    May 06, 2025
  • DC MWENDA ATOA WITO KWA WALIMU WA SHULE ZA MSINGI KUIMARISHA UFUNDISHAJI KWA MADARASA YA MITIHANI

    May 06, 2025
  • JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI WILAYANI IRAMBA LATOA ELIMU YA KINGA DHIDI MAJANGA YA MOTO KWA MADIWANI NA WANANCHI

    May 02, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.