• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba, Linno Mwageni ametekeleza agizo la Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dkt Rehema Nchimbi kwa kununua vifaa vya kuchukua tahadhari ya kujikinga na maambukizi ya homa kali ya mapafu inayosababishwa na virusi vy

Posted on: May 14th, 2020

Hemedi Munga, Irambadc

tehama@irambadc.go.tz

Iramba. Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Emmanuel Luhahula amepokea vifaa vyenye thamani ya zaidi ya Tsh 9.1milioni vya kujikinga na kuchukua tahadhari ya maambukizi ya homa kali ya mapafu inayosababishwa na virusi vya corona kutoka kwa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba na Wadau Wengine.

Luhahula amepokea vifaa hivyo leo Alhamisi Mei 14, 2020 katika hafla fupi iliyofanyika katika viwanja vya ofisi ya Halmashauri hiyo mjini hapa.

Akiongea katika hafla hiyo Mkuu huyo wa Wilaya, amempongeza Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo, Linno Mwageni pamoja na Madiwani wote kwa kununua vifaa vya kuchukua tahadhari na kujikinga na maambukizi ya homa kali inayosababishwa na virusi vya korona.

Amesema Halmashauri hiyo imetoa Tsh 5milioni huku wadau mbalimbali wakijitolea zaidi ya Tsh 4.1milioni.

“Nimshukuru Mkurugenzi Mtendaji Linno Mwageni na   wadau ambao  tulikutana nao Aprili 28 mwaka huu  kujadiliana kuhusu timu ya Karantini ya vijana 35  ambayo inasaidia kutoa elimu pamoja na kushughulikia uchukuaji wa tahadhari ya kujikinga na maambukizi ya homa kali ya mapafu inayosababishwa na virusi vya corona  katika Wilaya yetu ili kuwakinga wananchi wetu”  amesisitiza Luhahula na kuongeza

“Tunashukuru kuambiwa na Mkurugenzi Mtendaji kuwa  tayari wameshanunua  ndoo 63 za kunawia za  kukanyaga,   sabuni pamoja na mavazi rasmi pea 40 za PPE (Personal Protective Equipments) ya kujikinga wakati wakutoa huduma.”

Katika kuendelea kupambana na kuchukua tahadhari ya maambukizi ya homa kali ya mapafu inayosababishwa na virusi vya corona, Waziri wa Katiba na Sheria, Dkt. Mwigulu Nchemba amechangia ndoo 48.

Luhahula amefafanua kua ndoo hizo zilizotolewa na Dkt. Mwigulu Nchemba zimepelekwa katika kila ofisi ya Mtendaji wa kata na ofisi ya kata ya Chama cha Mapinduzi (CCM) wilayani humo.

Halikadhlika, Luhahula amesema kua wameweka utaratibu wa kupima joto watu wanaokuja kwenye msiba kutoka nje ya wilaya hiyo, hivyo endapo atapatikana mmoja wapo ana dalili za ugonjwa huo, nyumba hiyo yenye msiba itawekwa  karantini kwa siku 14.

 Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo, Linno Mwageni amesema kua Halmashauri imetekeleza agizo la  Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Rehema Nchimbi  kuhusu kila Halmashauri kununua vifaa vya kujikinga na ugonjwa wa corona pamoja na kununua vifaa vya kunawia kwa Zahanati 29, vituo vya Afya 4 na Hospitali ya Wilaya.

Naye Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo, Samwel Shillah amesema kuwa tayari wananchi wamekwisha elewa utaratibu wa kupima joto kuwa ni wakawaida.

Utaratibu huo umesaidia mtu kujua hali yake na kuwa eneo analokwenda ni salama kwa ajili ya kuchukua tahadhari ya kujikinga na homa kali ya mapafu inayosababishwa na virusi vya corona.

MWISHO

Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Emmanuel Luhahula akinawa maji yanayotiririka kutoka katika ndoo mojawapo kati ya zilizotolewa na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo, Linno Mwageni. Picha na Hemedi Munga

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba, Linno Mwageni akimkabidhi Kaimu Mganga Mkuu wa Halmashauri hiyo, Dkt. Timothy Sumbe PPE na Sabuni. Picha na Hemedi Munga

Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Emmanuel Luhahula akimshukuru Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo, Linno Mwageni kwa vifaa vya kujikinga na maambukizi ya homa kali ya mapafu inayosababishwa na virusi vya corona alivyomkabidhi. Picha na Hemedi Munga

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba, Linno Mwageni akifafanua namna alivyotekeleza agizo la Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dkt. Rehema Nchimbi. Picha na Hemedi Munga

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • KIDATO CHA KWANZA KURIPOTI SHULE January 13, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • MAAFISA ELIMU KATA 136 MKOANI SINGIDA WAPATIWA MAFUNZO KUHUSU USIMAMIZI WA SHULE NA UJAZAJI TAKWIMU KATIKA MFUMO WA "SIS"

    March 24, 2025
  • DC MWENDA AWASISITIZA WALIPA KODI KUFANYA MAKADIRIO YA KODI KABLA YA MACHI 31, 2025

    March 20, 2025
  • DC MWENDA NA WAZIRI MWIGULU NCHEMBA WACHANGIA JUMLA YA MADAWATI 98 SHULE YA MSINGI MSANSAO ILIYOPO KATA YA MTEKENTE

    March 10, 2025
  • WALIMU WAKUU 108 WA SHULE ZA MSINGI NA MAAFISA ELIMU KATA 20 WILAYANI IRAMBA WAPEWA MAFUNZO ENDELEVU YA USIMAMIZI WA UFUNDISHAJI NA UJIFUNZAJI FANISI KUPITIA JUMUIYA ZA KUJIFUNZA ZA WALIMU WAKUU NA MAAFISA ELIMU KATA

    March 19, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.