• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Comments |
Iramba District Council
Iramba District Council

The United Republic of Tanzania Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Iramba District Council

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba, Linno Mwageni amewaagiza Wamiliki wa Maduka ya Dawa na Maabara za Binaadamu kufuata kanuni, taratibu na miongozo mbalambali ya kutoa huduma hiyo muhimu kwa maisha ya mwanadamu. Picha na Hemedi Munga

Posted on: January 25th, 2020

Hemedi Munga, Irambadc

tehama@irambadc.go.tz

Iramba. Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba, Linno Mwageni amewaagiza Wamiliki wa Maduka ya Dawa na Maabara za Binaadamu kufuata kanuni, taratibu na miongozo mbalambali ya kutoa huduma hiyo muhimu kwa  maisha ya mwanadamu.

Mwageni ameyasema hayo leo Jumamosi Januari 25, 2020 wakati akiongea na Wamiliki hao katika kikao kazi Ukumbi Mkubwa wa Halmashauri hiyo mjni hapa.

“ Kila mmoja anapaswa kufahamu  sheria inayomuongoza kufanya hizi shughuli na hukumu zake,” alisisitiza Mwageni na kuongeza

“ Mnafanya biashara zinazookoa uhai wa binaadamu hivyo mnapaswa kuchukua tahadhari mnapotoa huduma hizo”

Kuchukua tahadhari kunasababisha kuepusha madhara yanayotokana na Wamiliki ambao hawafuati taratibu na kanuni ya kuendesha maduka hayo.

“Ninawaagiza Wamiliki wote wa Maduka ya Dawa na Maabara za Binaadamu kuingia kwenye shughuli hii ili kuisaidia wilaya  kutoa huduma zinazostahiki na si kutoa huduma ili kukuza mtaji,” amesema Mwageni

Vilevile amewatahadharisha Wamiliki hao kuchukua dawa serikalini kuwa ni rahisi kufahamika na nisababu yakufirisika.

Awali akiwasilisha taarifa ya Mganga Mkuu wa Wilaya hiyo, Kaimu Mganga Mkuu Afisa Ustawi wa Jamii, Hapiness Alex amesema duka la dawa muhimu ni miongoni mwa biashara zinazodhibitiwa na kusimamiwa kwa mujibu wa sheria ya Baraza la Famasi.

Wilaya hiyo inajumla ya maduka ya dawa muhimu 121 na maabara 11 katika vijiji, mitaa na vitongoji mbalimbali.

Pia amemuahidi Mkurugenzi huyo kuendeleza usimamizi shirikishi unaolenga kufuatilia huduma zinazotolewa na maduka ya dawa muhimu, uhai wa vibali vya maduka hayo na  utendaji kazi na uhai wa vibali vya maabara za binaadamu.

Tabia hiyo husaidia kujenga uhusiano mzuri na kuimarisha huduma za afya katika vijiji, mitaa na vitongoji vyote.

Naye ndugu Joseph wa Mamlaka  ya Dawa na Vifaa Tiba ameawataka wamiliki hao kutunza nyaraka za manunuzi kutokana na uwepo wa dawa ambazo hazina usajili  na si  salama, hivyo itaturahisishia kuzifahamu  wakati wa ukaguzi na kuwachukulia hatua wanaohusika.

“Ninawaagiza kununua dawa zilizoandikwa majina ya dawa na majina ya kampuni yaliozalisha dawa hizo,” amesema

Akiongea katika kikao hicho Afisa Biashara wa Wilaya hiyo, Prosper Banzi amewataka Wamiliki hao kufuata utaratibu wa kupata leseni na kusoma vizuri masharti yake.

“ Ni bora tuwe na wafanya biashara wachache wanaofuata kanuni, vigezo na masharti ambayo mmewekewa na sekta zote,” amesema

Pia amewaambia kuwa ukaguzi wa leseni unaendelea na hivyo atakayebainika kukiuka sheria ya leseni atapigwa faini.

Akichangia mada mmoja wa Wamiliki wa Maduka kwa niaba ya wengine, Alex Paneras ameuomba uogozi kuwapa ushirikiano mzuri pindi wanapokuja kukagua maana mara nyingi  huwa wanawafikiria kuwa ni vibaka kutokana na tabia na muonekano wao na kuwataka   Wamiliki wenzake kuwa makini.                                                                                                                                                                                                                                                                                           

Afisa Ustawi wa Jamii, Hapiness Alex akiwasilisha taarifa ya Mganga Mkuu inayohusu  Wamiliki wa Maduka ya dawa na Maabara za Binaadamu mbele ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo. Picha na Hemedi Munga                            

                                Wamiliki wa Maduka ya dawa na maabara za Binaadamu wakifuatilia mada mbalimbali zilizowasilishwa katika kikao hicho. Picha na Hemedi Munga


Announcements

  • TANGAZO KUHUSU UJIO WA MADAKTARI BINGWA HOSPITALI YA WILAYA YA IRAMBA-KIOMBOI February 20, 2026
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU January 02, 2026
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • View All

Latest News

  • MAONESHO YA MATUMIZI YA PEMBEJEO ZA KILIMO (MBEGU, MBOLEA NA VIUATILIFU) HALMASHAURI YA WILAYA YA IRAMBA DISEMBA 29-30, 2025

    December 28, 2025
  • HERI YA SIKUKUU YA KRISMASI NA MWAKA MPYA 2026

    December 25, 2025
  • DC MWENDA AWATAKA WALIMU IRAMBA KUONGEZA UBUNIFU NA BIDII KUINUA UFAULU

    December 09, 2025
  • HERI YA MIAKA 64 YA UHURU WA TANZANIA BARA

    December 09, 2025
  • View All

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
More Videos

Quick Links

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Related Links

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    KIOMBOI, IRAMBA

    Postal Address: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Telephone: 026 - 2532253

    Mobile: 026 - 2533001

    Email: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.