• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba. Linno Mwageni azifunda jumuiya za maji vijijini.

Posted on: July 13th, 2020

Hemedi Munga, Irambadc

ded.irambadc@singida.go.tz

Iramba. Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba Mkoani Singida, Linno Mwageni amewataka Wenyeviti wa bodi za maji, Wawakilishi wa Wanawake katika bodi za maji, Wahasibu wa jumuiya na Makatibu wa Jumuiya kutoa huduma bora ya maji katika maeneo yao ili jamii iweze kunufaika na huduma hiyo.

Mwageni ameyasema hayo mwishoni mwa wiki wakati alipokua akiongea na wajumbe hao katika kikao kazi cha Mkutano Mkuu wa Nusu Mwaka wa Wakala wa  Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (  RUWASA) uliofanyika katika  ukumbi mkubwa wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba mjini hapa.

“Niwaombe wajumbe kutoa huduma za maji zilizokua bora zitakazo mnufaisha mwananchi kwa sababu yeye ndio mlengwa aliyesogezewa huduma za maji vijijini,” amesema Mwageni na kuongeza kuwa

 

“Mnajukumu kubwa la kuhakikisha mnasimamia kanuni na taratibu za uanzishaji na uendelezaji wa jumuiya za maji vijijini kwa lengo lakutoa haduma bora na sio kuathiri jumuiya hizo.”

Amewataka Wenyeviti wa vijiji na Watendaji wa kata kusimamia Jumuiya za maji ili kuziba mianya ya kuvujisha fedha na kuwa kila fedha itakayopatikana ipelekwe benki.

“Mkilitekeleza hilo mtasaidia fedha zinazopatikana kuendelea kupanua mradi wa jumuiya na kuweza kuwafikia wananchi mahala ambapo mradi ulikua haujafika,” ametilia mkazo Mwageni

 

Kwa upande wake Afisa Tawala wa Wilaya hiyo, Dijovison Ntangeki ambaye alimuwakilisha Mkuu wa Wilaya hiyo, Emmanuel Luhahula katika hotuba yake amesema Serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli itaendelea kuwekeza ujenzi wa miradi ya maji vijijini kwa kuwashirikisha wananchi kuibua, kupanga, kutekeleza, kusimamia na kuendesha miradi hiyo pindi itapokamilika.

“Ndugu zangu Wajumbe fahamuni kuwa ni kosa kisheria kwa chombo chochote kinachotaka kutoa huduma ya maji vijijini pasipo kusajiliwa kwa mujibu wa sheria namba 5 ya 2019 inayomtaka mwendeshaji kupata leseni ya kutekeleza jukumu hilo, hivyo hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi ya mtu au chombo hicho,” amesema Ntangeki kwa niaba ya Mkuu huyo

Akitoa taarifa fupi ya utekelezaji wa sheria mpya ya uundaji wa jumuiya za maji vijijini, Meneja wa Maji wa Wilaya hiyo,Mhandisi Ezra Macha amesema jumuiya 14 zimeisha kamilisha taratibu za uhuishaji huku vijiji vitatu vya Meli, Nselembwe na Nguvumali vikiwa katika hatua za ukamilishaji wa taratibu za usajili.

Macha amewaambia wajumbe hao kuwa fedha za jumuiya zitabaki kuwa za jumuiya kwa kufuata sheria hii ambayo imeingiza wataalam katika bodi ya maji ili kuongeza uwajibikaji na utaalam katika kusimamia jumuiya za maji ngazi ya jamii ili ziwe endelevu zenye ufanisi na upatikanaji wa fedha.

Naye mmoja wa washiriki wa Mkutano huo toka kata ya Mukulu Wilayani hapo, Eliya Sauti amewaomba viongozi wa RUWASA kufika vijijini mara kwa mara kwa lengo la kuendelea kutoa elimu ya mabadiliko ya sheria hiyo.

MWISHO

Meneja wa Maji Wilayani Iramba, Mhandisi Ezra Macha akizihakikishia jumuiya za maji kuwa fedha za jumuiya zitabaki kuwa za jumuiya kwa kufuata sheria Na 5 ya mwaka 2019 ambayo imeingiza wataalam katika bodi ya maji ili kuongeza uwajibikaji na utaalam katika kusimamia jumuiya za maji ngazi ya jamii ili ziwe endelevu zenye ufanisi na upatikanaji wa fedha. Picha na Hemedi Munga

Afisa Tawala wa Wilaya ya Iramba, Dijovison Ntangeki akigawa vyeti kwa jumuiya za maji vijijini zilizokwisha kamilisha usaji kwa mujibu wa Sheria Na, 5 ya mwaka 2019. Picha na Hemedi Munga

Wenyeviti wa bodi za maji, Wawakilishi wa Wanawake katika bodi za maji, Wahasibu wa jumuiya na Makatibu wa Jumuiya wakifuatilia maelekezo mbalimbali toka kwa wataalam namna ya kuziendesha jumuiya zao kifanisi. Picha na Hemedi Munga


Tangazo

  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI June 05, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • DC MWENDA ATEMBELEA MRADI WA UJENZI WA SHULE MPYA YA SEKONDARI YA AMALI KITUKUTU

    May 08, 2025
  • KAMATI YA FEDHA, UONGOZI NA MIPANGO YA HALMASHAURI YA WILAYA YA IRAMBA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO

    May 06, 2025
  • DC MWENDA ATOA WITO KWA WALIMU WA SHULE ZA MSINGI KUIMARISHA UFUNDISHAJI KWA MADARASA YA MITIHANI

    May 06, 2025
  • JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI WILAYANI IRAMBA LATOA ELIMU YA KINGA DHIDI MAJANGA YA MOTO KWA MADIWANI NA WANANCHI

    May 02, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.