• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Comments |
Iramba District Council
Iramba District Council

The United Republic of Tanzania Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Iramba District Council

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba mkoni Singida, Mhandisi Michael Matomora amesikiliza na kutatua changamoto ya kulipa kodi ya vibanda iliyodaiwa kuwa kubwa na wafanyabiashara wa mji mdogo Kiomboi.

Posted on: January 8th, 2022

Na Hemedi Munga

tehama@irambadc.go.tz

Singida - Iramba. Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba mkoni Singida, Mhandisi Michael Matomora amesikiliza na kutatua changamoto ya kulipa kodi ya vibanda iliyodaiwa kuwa kubwa na wafanyabiashara wa mji mdogo Kiomboi.

Matomora ametatua changamoto hiyo mwishoni mwa juma hili alipokutana na wafanyabiashara hao katika ukumbi Mkubwa wa Halmashauri hiyo mjini hapa.

Akiongea katika kikao hicho Mkurugenzi huyo, amewataka wafanyabiashara hao kulipa kodi ili Halmashauri iweze kukusanya mapato na kufikisha miundombinu mbalimbali katika soko na stendi.

“Ndugu zangu wafanyabiashara ni lazima tufahamu kuwa kulipa kodi ni lazima, hivyo nilazima tukubaliane kodi ya kizalendo ambayo kila mmoja kuanzaia leo baada ya kikao hichi atakwenda kulipia kodi ya kibanda anachomiliki kilichopo katika eneo la Serikali.” Alisema Matomora na kuongeza kuwa

“Siwezi kukubali kuwa na soko chafu kiasi hicho, hivyo tumeanza kuweka umeme na miundombinu mingine itafuata mpaka pawe pazuri na rafiki pakufanyia biashara muda wote.”

Katika kikao hicho wamakubaliana kila mwenye kibanda kulipia kiasi cha Tsh 10000 kila mwisho ya mwezi ukilinganisha na Tsh 20000 iliyokuwa ikilipwa kabla ya kikao hicho.

“Mimi naridhia kuanzia Februari mosi, 2022 mkalipie Tsh 10000 kila tarehe ya mwisho wa mwezi, hivyo vibanda vyote wamiliki wake waende wakalipe kodi kwa sababu sitaki kusikia mfanyabiashara anatengeneza deni sinta weza mvumilia.” Alisistiza

Aidha amewataka wafanyabiashara hao kwenda kulipa madeni amabayo wamekwisha yatengeneza katika mfumo wa mapato kwa kuwa hakuna namna wa kuyafuta madeni hayo ispokuwa ni kwa kulipa madeni.

Alifafanua kuwa kiwango cha Tsh 10000 ni kiwango kidogo ambacho mfanyabiashara anaweza kulipa kodi hiyo huku akiweka utaratibu mzuri wa kulipa deni.

Awali akiongea katika kikao hicho Afisa Biashara wa Halmashauri hiyo, Prosper Banzi aliwapongeza wafanyabiashara hao kwa sababu wamekuwa na subira dhidi ya mgogoro huo uliodaiwa kuwapo kwa muda mrefu.

“Hongereni sana kwa uvumilivu, hali hii inatujengea taswira mpya ya kulitekeleza jukumu la kulipa kodi ya vibanda kwa wakati kwa sababu sasa ni kodi ambayo mmeipanga wenyewe.” Alisema Banzi

Kwa upande wake mmoja wa wafanyabiashara hao, Omari Haruna alishukuru kwa kiwango cha Tsh 10000 na kuahidi kuwa maamuzi hayo yaliofikiwa katika kikao hicho itakuwa ni sababu ya kuendelea kurekebisha vibanda vingine ili Halmashauri ipate mapato mengi.

“Kwa kweli wastani wa kodi hii ninauhakika wafanyabiashara hawa watalipia na kuendeleza vibanda ambavyo vilikuwa ni magofu kutengenezwa kuwa safi na tayari kwa kuvilipia kodi.” Alisema Haruna

Naye mmoja wa wamiliki wa vibanda vya sokoni, Winjuka Msangulo alimshukuru Mkurugenzi huyo kwa makubaliano ambayo wameyafikia na kuahidi kuwa sasa watakuwa tayari kulipia kodi hiyo.

Aidha alisema kuwa watakuwa ni mabalozi watakofikisha ujumbe wa kulipia kodi ya vibanda kwa wamiliki wote ambao hawakufanikwa kufika katika kiako hicho.

“Nikuombe Mkurugenzi kwa wafanyakazi wako kuwa makini pale mteja anapokuja lipia deni lake apate bili iliokuwa sahihi kulingana na deni lake.” Aliomba

MWISHO

Announcements

  • TANGAZO KUHUSU UJIO WA MADAKTARI BINGWA HOSPITALI YA WILAYA YA IRAMBA-KIOMBOI February 20, 2026
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU January 02, 2026
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • View All

Latest News

  • MAONESHO YA MATUMIZI YA PEMBEJEO ZA KILIMO (MBEGU, MBOLEA NA VIUATILIFU) HALMASHAURI YA WILAYA YA IRAMBA DISEMBA 29-30, 2025

    December 28, 2025
  • HERI YA SIKUKUU YA KRISMASI NA MWAKA MPYA 2026

    December 25, 2025
  • DC MWENDA AWATAKA WALIMU IRAMBA KUONGEZA UBUNIFU NA BIDII KUINUA UFAULU

    December 09, 2025
  • HERI YA MIAKA 64 YA UHURU WA TANZANIA BARA

    December 09, 2025
  • View All

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
More Videos

Quick Links

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Related Links

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    KIOMBOI, IRAMBA

    Postal Address: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Telephone: 026 - 2532253

    Mobile: 026 - 2533001

    Email: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.