• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba Mwl. Linno Mwageni amekabidhi vifaa vya michezo kwa timu za sekondari Wilayani Iramba mkoa wa Singida. Vifaa hivyo vya michezo vimetolewa na kampuni ya Coca-Cola Katika shule za sekondari 23.

Posted on: August 27th, 2018

Walimu wakuu kwa kushirikiana na walimu wao wa michezo wa shule za sekondari zipatazo23 katika Halmashauri ya Wilaya ya Iramba, wamepokea vifaa mbali mbali vya michezo kutoka katika kampuni ya vinywaji baridi nchini Coca cola.

Zoezi hilo limeweza kufanyika katika ukumbi mdogo wa mikutano uliopo katika Ofisi za Halmashauri ya Wilaya ya Iramba na kuhudhuriwa na walimu wakuu na wengine kuwakilishwa na walimu wao wa michezo, nakupokea jezi 36 za mpira wa miguu pamoja na mpira wa kikapu.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba Mwl. Linno Mwagenia ameshukuru kampuni ya Coca-Cola kwa kutoa zawadi hizi za michezo. Ameongeza kusema zawadi hizo zitafanikisha jitihada za kuendelea kuibua vipaji vya wachezaji chipukizi wa michezo ya soka mpira na kikapu. alisisitiza kuwa sekta ya michezo inazidi kukua ambapo hivi sasa lengo lake sio burudani bali ni biashara kubwa. 

Kwa mujibu wa Mwakilishi wa Kampuni ya Coca cola Mkoa wa Singida Ndg. Benjamin Daud ambaye ameudhuria katika ufanyikaji wa zoezi hilo Wilayani hapa, amesema kwamba zoezi hili hufanyika kila mwaka kwa ushirikiano wa Maafisa Elimu Michezo na Utamaduni katika wilaya hii. Aliongeza kusema kampuni ya Coca-Cola inajivunia kuhamasisha michezo katika Wilaya ya Iramba kwa kutoa vifaa vyamichezo katika shule  23 za sekondari. “naamini vipaji vingi vinaibuliwa na vitaendelea kuibuliwa baada ya kutoa vifaa vya michezo” alisema Ndg. Benjamin.

Ndg.Benjamin alisema kwamba wameweza kugawa kwa kila shule za elimu sekondari wilayani Iramba Jezi za mpira wa Miguu 18 na mpira wa Kikapu 18 jumla yake 36 pamoja na Mpira wa miguu mmoja na wa kikapu mmoja kwa kila shule za sekondari zipatazo 23 Wilayani hapa.

Lengo haswa la ugawaji wa vifaa vya michezo kwa shule hizo za sekondari Ndg. Benjamin ameeleza kwamba ni kukuza na kuendeleza vipaji vya wanafunzi mbali mbali katika shule hizo za sekondari pamoja na kampuni hiyo kuweza kuwa karibu na jamii.

Nao walimu wa shule hizo za sekondari waliweza kuishukuru kampuni hiyo ya vinywaji vya Coca cola kwa kusema kwamba, imesaidia kukuza vipaji vya wanafunzi wao pamoja na mazingira ya wanafunzi hao kupenda zaidi masomo.  

Vifaa hivyo vya michezo kwa wanafunzi wa shule za sekondari hutumika katika mashindano mbali mbali yakiwemo mashindano ya UMISETA pamoja na Copa Coca cola.


Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba Mwl. Linno Mwageni akiwa kwenye picha ya pamoja na Mwakilishi wa Kampuni ya Coca cola Mkoa wa Singida Ndg. Benjamin Daud, Walimu wakuu na walimu wa michezo wa shule za sekondari baada ya kukabidhi vifaa vya michezo kwa timu za sekondari Wilayani Iramba mkoa wa Singida. 

Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA IRAMBA November 03, 2023
  • KUITWA KAZINI November 29, 2023
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2018 HALMASHAURI YA WILAYA IRAMBA January 05, 2019
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA KIDATO CHA PILI (FTNA) 2018 January 05, 2019
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • Wajumbe wa Kamati ya Fedha, Utawala na Mipango ya Halmashauri ya Wilaya ya Iramba wamefanya ziara ya Ukaguzi wa Miradi mbalimbali ya Maendeleo inayotekelezwa Wilayani Iramba

    October 24, 2023
  • RAIS DKT. SAMIA AHITIMISHA ZIARA YAKE MKOANI SINGIDA KWA KISHINDO, WANANCHI WAMSHUKURU KWA MIRADI YA MAENDELEO

    October 17, 2023
  • MKUU wa Mkoa wa Singida Peter Serukamba amepokea rasmi Mbio za Mwenge wa Uhuru kutoka Mkoani Tabora na aliyekabidhi ni Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Balozi Batlida Briani.

    September 22, 2023
  • MKIMBIZA Mwenge wa Uhuru Kitaifa, Abdalla Shaibu Kaim amewataka Watanzania kuhakikisha wanakemea vitendo vya rushwa kwa maelezo kuwa rushwa inakwamisha maendeleo ya Mkoa pamoja na Taifa kwa ujumla

    September 22, 2023
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.