• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Mkutano mkuu wa ALAT mkoa wa singida umefanyika leo tarehe 21 Decemba 2018 katika ukumbi wa halmashauri ya wilaya ya Iramba mkoani Singida.

Posted on: December 20th, 2018

Mwenyekiti wa ALAT mkoa wa Singida Mhe. James J. Mkwega ameongoza kikao hicho wilayani Iramba na kujadili mambo mbalimbali yakiwemo msimu wa kilimo, mikakati ya kupokea wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza kwa mwaka 2018/2019, utoaji wa vitambulisho vya wajasiliamali wadogo wadogo na kutembelea na kukagua miradi ya maendeleo iliyopo halmashauri ya wilaya ya Iramba.

Akizungumza kwenye mkutano wa ALAT Mkuu wa wilaya ya Iramba Mhe. Emmanuel Luhahula ambaye ni Mgeni rasmi, amepongeza mkutano wa ALAT kwa kufanya kazi kwa ushirikiano ili kutatua changamoto zilizopo kwenye halmashauri zetu. “Nawapongeza sana wajumbe wa ALAT kwa kazi nzuri mnazozifanya katika kusimamia serikali za mitaa. Natambua juhudi zenu nzuri jinsi mnavyoshiriki kuleta maendeleo katika maeneo yetu kwa kutembelea na kukagua miradi ya maendeleo, endeleeni na utaratibu huu wa kufanya ziara za mara kwa mara za kutembelea na kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo ili kuhakikisha miradi hiyo inatekelezwa kwa kiwango kinachotakiwa”. alisema Mhe. Luhahula

Alisisitiza wajumbe wa ALAT kusimamia kilimo cha mazao ya Alizeti, Pamba na Korosho, katika ngazi ya kijiji na kata ili yawe mazao ya kudumu ya biashara kwa wananchi wa mkoa wa singida. “Mazao yetu ya kimkakati katika mkoa wetu ni Alizeti, Pamba na Korosho. Viwanda tulivonavyo katika mkoa wetu wa singida vinauwezo wa kukamua mbegu za Alizeti tani laki 482, tunazalisha tani laki 260 tu, tuna upungufu mkubwa sana, lazima wananchi walime Alizeti kwa kutumia mbegu tija kwa utaratibu na kanuni bora za kilimo ili kuhakikisha tunapata tani 482. Tukiboresha mazao haya ya kimkakati, tukawa na Pamba, Korosho na Alizeti tutatengeneza mfumo mzuri wa kununua kupitia kwenye ushirika, Halmashauri zetu zitapata ushuru wa kutosha na vyanzo vyetu vitakuwa vimeongezeka”. Alisisitiza Mhe. Luhahula

 Aidha Mhe. Luhahula amezitaka halmashauri ziendelee na ubunifu wa kuibua vyanzo vipya vya mapato ili kuinua kiwango cha ukusanyaji wa mapato katika ngazi ya halmashauri na vyanzo vya mapato viimarishwe na kusimamiwa.

Vile vile Mhe. Luhahula amesisitiza kuhakikisha wananchi wanafanya kazi kwa bidii ili kuendana na kasi ya Mhe. Rais Dkt. John Joseph Pombe Magufuli ya kuipeleka nchi kwenye uchumi wa kati na viwanda. “ALAT hamuwezi kujitenga na serikali kuu katika kutekeleza na kuleta uchumi ambao serikali yetu inataka tufike. Tumeona kazi kubwa ambazo Mhe. Rais Dkt John Joseph Pombe Magufuli anazozifanya kutengeneza viwanda vipya zaidi ya 3066, ujenzi wa Miundombinu ya Barabara na madaraja, Ujenzi wa reli ya mwendo kasi ya stanadard gauge, Ujenzi wa mradi wa umeme wa stieglers gorge, Ununuzi wa ndege 7, Ujenzi na ukarabati wa vituo vya afya na hosipitali, Ujenzi na ukarabati wa nyumba za wakuu wa wilaya na Watumishi, ujenzi na ukarabati wa vyuo, shule za sekondari na msingi, Elimu bila malipo na miradi mingine mingi alisema Mhe. Luhahula

Aliongeza kusema, kila mmoja wetu atambue na atimize wajibu wake ili tuhakikishe tunawasaidia wananchi wetu. “tukawasaidie, tukawasemee, wananchi wetu wakati mwingine wanateswa na Rushwa, Waheshimiwa madiwani ni watu ambao mna nafasi ambazo mnaweza kusimama na kutetea wananchi wenu mahala walipo, ukisimama wewe kidedea mwananchi hawezi kuonewa kule.  Lazima uchumi wa kati umufikie mwananchi. Alisisitiza Mhe. Luhahula.



Wajumbe wa ALAT wakifuatilia majadiliano katika kikao hicho yakiendelea katika wa halmashauri ya wilaya ya Iramba katika ukumbi wa halmashauri.


Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • KIDATO CHA KWANZA KURIPOTI SHULE January 13, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • MAAFISA ELIMU KATA 136 MKOANI SINGIDA WAPATIWA MAFUNZO KUHUSU USIMAMIZI WA SHULE NA UJAZAJI TAKWIMU KATIKA MFUMO WA "SIS"

    March 24, 2025
  • DC MWENDA AWASISITIZA WALIPA KODI KUFANYA MAKADIRIO YA KODI KABLA YA MACHI 31, 2025

    March 20, 2025
  • DC MWENDA NA WAZIRI MWIGULU NCHEMBA WACHANGIA JUMLA YA MADAWATI 98 SHULE YA MSINGI MSANSAO ILIYOPO KATA YA MTEKENTE

    March 10, 2025
  • WALIMU WAKUU 108 WA SHULE ZA MSINGI NA MAAFISA ELIMU KATA 20 WILAYANI IRAMBA WAPEWA MAFUNZO ENDELEVU YA USIMAMIZI WA UFUNDISHAJI NA UJIFUNZAJI FANISI KUPITIA JUMUIYA ZA KUJIFUNZA ZA WALIMU WAKUU NA MAAFISA ELIMU KATA

    March 19, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.