• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Mkuu wa mkoa wa Singida, Dkt. Binilith Mahenge amewahamasisha wananchi wote kulima zao la alizeti pamoja na mazao mengine kwa kadri wanavyoweza. Dkt Mahenge ametoa wito huo leo Alhamisi Januari 27, 2022 alipofanya ziara ya kukagua miradi ya ujenzi wa bar

Posted on: January 27th, 2022

Na hemedi Munga

tehama@irambadc.go.tz

Singida – Iramba. Mkuu wa mkoa wa Singida, Dkt. Binilith Mahenge amewahamasisha wananchi wote kulima zao la alizeti pamoja na mazao mengine kwa kadri wanavyoweza.

Dkt Mahenge ametoa wito huo leo Alhamisi Januari 27, 2022 alipofanya ziara ya kukagua miradi ya ujenzi wa barabara katika kata ya Urughu wilayani Iramba.

“Ndugu zangu huu ni msimu wa kilimo kila mmoja afanye kazi kwa sababu barabara zinajengwa ili msafirishe mazao yenu.” Alihamasisha Dkt Mahenge

Aidha, aliongeza kuwa kwa mara ya kwanza serikali ya Mheshimiwa Rais Samia imeweka ruzuku katika mbegu ya alizeti ambapo ukienda dukani na kuambiwa mfuko wa mbegu ya alizeti unauzwa mfano wa Tsh 7000 basi mwananchi atachangi Tsh 3500 na serikali kumuongezea Tsh 3500.

“Haijawahi kutokea mkoa wa Singida tumepewa tani 465 zenye thamani ya takribani Tsh 3 bilioni, hivyo niwashawishi ndugu zangu twendeni tukalime.” Alihamasisha Mkuu wa Mkoa

Pia aliwaeleza kuwa katika kampeni ya mkoa kulima zao la alizeti bado haijafunga milango kwa mkulima mabaye anahitaji kulima zao la mtama, mahindi, pamba na mazao mengineyo kulingana na uwezo wao na utashi.

Halikadhalika, Dkt Mahenge alitumia fursa hiyo kuwahimiza wananchi kuwapeleka watoto ambao wamefaulu shule kwa sababu elimu ndio urithi wao utakao wakomboa katika maisha haya.

“Ndugu zangu niwaombe mpeleke watoto shuleni kwa sababu shule zimeishafunguliwa zikiwa na madarasa yakutosha, madawati yakutosha na  walimu wakutosha.”

Alifafanua kuwa elimu ndio ufunguo utakaomkomboa mwanafunzi na kuweza kujiajiri na pindi atakapopewa fedha anaweza kufanya biashara kwa ufanisi.

Awali akielezea hali ya barabara katika kata ya Urughu wilayani Iramba Mkuu wa wilaya hiyo, Suleiman Mwenda alionesha furaha yake kwa wananchi hao baada ya kuona kuwa kero walizowasilisha kwake kipindi alipofika kusikiza kero zimetatuliwa.

“Ndugu zangu ni baada ya miezi minne tangu muwasilishe kero ya barabara kwangu na serikali ya awamu ya sita chini ya Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan imewatimizia ujenzi wa barabara na leo Mkuu wa mkoa amekuja kuzikagua.” Alisema Mwenda

Kwa upande wake diwani wa kata ya Urughu wilayani hapo, Simon Tyosela akamuomba Mkuu huyo wa mkoa  kuwafikishia salamu zao za pongezi na shukrani  kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan kwa kuwatatulia kero ya barabara.

“Mkuu wa mkoa tunashukuru sana kwa kufika kwako hapa tunaomba utufikishie salamu kwa Rais wetu Samia Suluhu Hassan kwa sababu hajawahi kufika huku lakini ametujali sana maana wilaya ya Iramba inakata 20 lakini katika kata yetu ametupatia takribani Tsh 1.5 bilioni ukilinganisha na kata nyingine.” Alisema Tyosela

Naye mmoja wa wananchi wa kijiji cha Urughu wilayani hapo, Mohammed Salehe alimshukuru mkuu huyo wa mkoa kwa kuwatembelea na kumuomba afike hapo mara kwa mara.

Salehe alisema kuwa serikali hii ni nzuri kwa sababu inaleta maendeleo katika kata yao.

MWISHO

Tangazo

  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI June 05, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • DC MWENDA ATEMBELEA MRADI WA UJENZI WA SHULE MPYA YA SEKONDARI YA AMALI KITUKUTU

    May 08, 2025
  • KAMATI YA FEDHA, UONGOZI NA MIPANGO YA HALMASHAURI YA WILAYA YA IRAMBA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO

    May 06, 2025
  • DC MWENDA ATOA WITO KWA WALIMU WA SHULE ZA MSINGI KUIMARISHA UFUNDISHAJI KWA MADARASA YA MITIHANI

    May 06, 2025
  • JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI WILAYANI IRAMBA LATOA ELIMU YA KINGA DHIDI MAJANGA YA MOTO KWA MADIWANI NA WANANCHI

    May 02, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.