• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dkt. Rehema Nchimbi ameipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Iramba kwa kuwa ya kwanza na kutoa mshindi wa kwanza kanda ya kati kwa zao la Mahindi katika kilele cha Maonesho ya Nane Nane mwaka huu.

Posted on: August 8th, 2020

Hemedi Munga, Irambadc

ded.irambadc@singida.go.tz

Dodoma. Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dkt. Rehema Nchimbi ameipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Iramba kwa kuwa ya kwanza na kutoa mshindi wa kwanza kanda ya kati kwa zao la Mahindi katika kilele cha Maonesho ya Nane Nane mwaka huu.

Dkt. Nchimbi ametoa pongezi hizo wakati alipokuwa akiongea na wakulima na wajasiriamali waliohudhuria maonesho hayo katika viwanja vya Nzuguni Jijini Dodoma mwishoni mwa wiki hii.

Akiongea katika hafla hiyo, Dkt. Nchimbi amesema kuwa kuja kwa maonesho ya Nane Nane Jijini Dodoma kumeleta nuru kwa watu wanaoishi katika jiji hilo.

Pia ameonesha kuwa kanda  ya kati ni tajiri kwa kuwa lina madini ya dhahabu na yureniam.

“Tumeombe Mungu na sisi tupate bonge kubwa la dhahabu, inaweza tokea, hivyo kuendelea kuimarisha utajiri wa kanda ya kati na kuifanya kuwa kama ulaya,” amesema Dkt. Nchimbi na kuongeza kuwa

Akiongelea kuhusu kauli mbiu ya Nane Nane mwaka huu isemayo “kwa maendeleo ya kilimo na uvuvi chagua kiongozi bora, Dkt. Nchimbi amesema kuwa kilicho bora huzaa bora, hivyo kilichotufikisha hapa ni uongozi bora na tuna haki ya kumshukuru Mhe, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli.

Halikadhalika Dkt. Nchimbi amewata wataalam walio onesha teknolojia ya magari na mitambo wezeshi kufika katika halmashauri zote za kanda ya kati kwa lengo la kutoa elimu ili teknolojia hiyo iweze kutumiwa na Halmashauri hizo.

“Teknolojia hiyo ni rahisi na garama yake pia ni rahisi, hivyo wakulima wengi wataweza kuitumia kwa urahisi ili wapate mavuno mengi” amesisitiza Dkt. Nchimbi

Pia amewataka wahusika hao kuhakikisha wanafikisha mbegu bora za mifugo katika halmashauri zote na kuwaasa wafygaji kuwa na mifugo michahche yenye ubora badala ya kuwa na mifugo mingi isiokuwa na ubora.

Pia amegiza kila Halmashauri kuwa na shamba la malisho huku akiahidi kuwa Nane Nane kutakuwa na tuzo ya malisho bora.

Kwa upande wake kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba, Jene Ng’ondi amewashukuru wajasiriamali na wakulima wote kwa kuwezesha Halmashauri hiyo kupata ushindi wa Mkulima bora wa zao la Mahindi kwa kanda ya kati na kuifanya Halmashuri hiyo kuwa ya kwanza kati ya Halmashauri saba za Mkoa wa Singida katika maonesho hayo.

 Aidha amewata wakulima hao kuanza maandalizi mapema ya Nane Nane ijayo kwa kuwa mwisho wa Nane  Nane hii ndio mwanzo wa Nane Nane ya mwaka ujao.

Naye mmoja wa wakulima kwa niaba ya Wajasiriamali na Wakulima hao Mgundu,

Yesaya Njolle amesema kuwa wamejifunza kuwa kilimo kinauwezo wa kumtoa Mkulima katika umasikini na kwenda kwenye hali ya kati ya maisha.

Ameongeza kuwa kilimo cha kisasa kwa wakati wa masika na kile cha kiangazi ikiwa masharti yatafuatwa kwa kuzingatia maarifa na weledi walioupata wanaouwezo wakupata mazao msimu wa kipwa na masika.

MWISHO

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba, Jene ng’ondi akiwa na Mshindi wa Kanda ya Kati kwa zao la Mahindi, Yesaya Njolle

pamoja na Wajasiriamali na wakulimwa wengine waliokuwa wakimpongeza katika viwanja vya Nzuguni Jijini Dodoma katika kilele cha Siku ya Nane Nane. Picha na Hemedi Munga

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba, Jene ng’ondi akiwa na Mshindi wa Kanda ya Kati kwa zao la Mahindi, Yesaya Njolle katika viwanja vya Nzuguni Jijini Dodoma siku ya kilele cha Nane Nane. Picha na Hemedi Munga

Tangazo

  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI June 05, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • DC MWENDA ATEMBELEA MRADI WA UJENZI WA SHULE MPYA YA SEKONDARI YA AMALI KITUKUTU

    May 08, 2025
  • KAMATI YA FEDHA, UONGOZI NA MIPANGO YA HALMASHAURI YA WILAYA YA IRAMBA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO

    May 06, 2025
  • DC MWENDA ATOA WITO KWA WALIMU WA SHULE ZA MSINGI KUIMARISHA UFUNDISHAJI KWA MADARASA YA MITIHANI

    May 06, 2025
  • JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI WILAYANI IRAMBA LATOA ELIMU YA KINGA DHIDI MAJANGA YA MOTO KWA MADIWANI NA WANANCHI

    May 02, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.