• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Mkuu wa Mkoa wa Singida DKt, Rehema Nchimbi amewaagiza Makamanda wa TAKUKURU kuwafuatilia Wanasheria na Mahakimu wanowaumiza wananchi

Posted on: January 23rd, 2021

Hemedi Munga, Irambadc

irambadc@singida.go.tz

Iramba, Mkuu wa Mkoa wa Singida DKt, Rehema Nchimbi amewaagiza Makamanda wa TAKUKURU waliopo katika Wilaya zote za Mkoa wa Singida  kuwafuatilia Wanasheria na Mahakimu umiza  ambao huweka Mahakama zao na kuwafundisha wananchi mambo yasiokua sahihi kwenye mwenendo wa kesi husika.

Dkt, Nchimbi ametoa agizo hilo leo Januari 23, 2021 wakati akiongea na viongozi mbalimbali waliohudhuria  hafla fupi ya kuongoza kuingia katika wiki ya sheria Nchini katika Ukumbi Mkubwa wa Halmashauri Mjini Kiomboi.

‘’  Ndugu viongozi wenzangu, ningependa viongozi  wengine waje kujifunza kwa Makamanda wa TAKUKURU  waliopo Iramba na Mkalama namna mtakavyotokomeza  tatizo  la Mahakimu wanaokiuka sheria  kwa kuwaumiza wananchi wenye mashauri mbalimbali katika mahakama zetu,’’ ameagiza Mkuu  wa Mkoa na kuongeza kuwa

‘’ Tunawajibu wa kuipenda sheria, kuifahamu sheria na kuiishi sheria ili kutokufanya makosa na kufahamu kuwa hakuna mtu aliyekua juu ya sheria, hivyo tuwe na tabia ya kutii sheria bila shuruti.’’

Halikadhalika amewataka Mahakimu kuwa na tabia za kutoa elimu ya sheria na utendaji kazi wake kwa jamii kwa sababu itaifanya jamii kutofanya makosa na kuwa watiifu wa sheria bila shuruti.

Katika hatua nyingine Dkt, Nchimbi amewaagiza Wakuu wa Wilaya zote Mkoa wa Singida kwa kushirikiana na Viongozi wa Dini kulinda barabara zilizopo katika Wilaya zao.

‘’ Ndugu washiriki ! tunafahamu kuwa kwa Mungu hakuna kona ya ajali, hivyo Mahakimu hawa wanatumia barabara hizi ni lazima wawe salama,’’ ametilia mkazo Mkuu wa Mkoa

Katika kuchambua maana ya sheria, Mkuu wa Mkoa, Dkt, Nchimbi amewataka Viongozi hao kutoa elimu kwa jamii inayowazunguka kuwa sheria ipo ndani ya mfumo wa Mwanadamu kwa kuwa kila kiungo  cha Mwanadamu kimekaa kwa kutii sheria.

Awali akitoa maelezo ya utangulizi wakati wa kuingia katika wiki ya sheria Nchini, Hakimu Mkazi Mfawidhi anayeshughulikia Wilaya ya Iramba na Mkalama , Christopher Makwaya amesema kuwa lengo la kukutana katika hafla hii ni kutoa elimu ya shughuli za  Mahakama katika utendaji wa haki.

Akisoma kauli mbiu ya Maadhimisho ya Wiki ya Sheria mwaka 2021 isemayo ‘’ Miaka 100 ya Mahakama Kuu, Mchango wa Mahakama katika kujenga Nchi inayozingatia uhuru, haki, udugu, amani na ustawi wa wananchi 1921 – 2021’’ Hakimu Makwaya amesema kuwa Mahakama ya Wilaya ya Iramba imedhamiria kufanya tathimini na kupokea maoni toka kwa wadau kuhusu utoaji wa huduma ya kimahakama.

‘’ Ndungu zangu niombe tufahamu kuwa sisi viongozi wa umma tunawajibu wa kufanya yaliokua mema kwa sababu jamii inatarajia huduma bora kutoka kwetu’’ amesisitiza Makwaya

Katika kuhakikisha Mahakama inatoa huduma bora kwa jamii, Makama imeboresa utoaji huduma za nakala za hukumu na mienendo ya mashauri iitwayo Posta Mlangoni na huduma ya ufunguaji wa kesi kwa njia ya mtandao iitwayo (electronic filing).

Pia amesema kuwa Mahakama Wilayani humo imefanikiwa kupunguza mashauri kwa kiwango kikubwa kati ya mashauri yaliopokelewa mwaka 2019/ 2020 ni 454 nakufanikiwa kuyasikiliza mashauri 361 na kubakiwa na mashauri 83.

Kwa upande wake mmoja wa washiriki wa hafla hiyo fupi, Afisa Tarafa wa kata ya Shelui, Nicholaus  Makoye amesema kuwa mimba za wanafunzi zitakoma kwa kuitaka jamii kutii sheria bila shuruti  kwa kushirikiana kutoa elimu  na kupambana na watu wasiowatakia mema wanafunzi kwa kuwasababisha  kupata mimba.

Katika kuingia katika wiki ya sheria Nchini zimewasilishwa mada ya ndoa na talaka, mirathi, dhamana, walinzi wa amani, maadili, kesi za jinai na elimu ya uhamiaji.

Uzinduzi wa wiki ya sheria utazinduliwa rasmi Januari 24 na Mhe, Makamu wa Rais, Samia Suluhu  na kilele chake kuhitimishwa Februari 1, 2021 na Mhe, Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli.

Mwisho

Hakimu Mkazi Mfawidhi anayeshughulikia Wilaya ya Iramba na Mkalama, Christopher Makwaya akielezea lengo la kukutana katika hafla ya kuingia katika wiki ya sheria Nchini kuwa ni kutoa elimu ya shughuli za Mahakama katika utendaji wa haki. Picha na Hemedi Munga

Hakimu wa Mahakama ya Mwanzo Wilayani Iramba, Mhe. Rehema Uroki akiwaelezea viongozi mbalimbali waliohudhuria hafla ya kuingia katika wiki ya sheria Nchini mada ya mirathi na umuhimu wa kutoa usia namna unavyosaidia ugawaji wa mirathi. Picha na Hemedi Munga

Mkuu wa Mkoa Dkt, Reheme Nchimbi akiwa na Viongozi mbalimbali pamoja na Waheshimiwa Mahakimu katika picha ya pamoja punde baada ya kuongoza kuingia katika wiki ya sheria Nchini. Picha na Hemedi Munga


Tangazo

  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI June 05, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • AFISA MWANDIKISHAJI JIMBO LA IRAMBA MAGHARIBI AWATAKA WAENDESHA VIFAA VYA BVR NA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI KUFANYA KAZI KWA WELEDI ILI KUFANIKISHA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI

    May 14, 2025
  • KAMATI YA AFYA YA MSINGI (PHC) IRAMBA YAJADILI MIKAKATI YA CHANJO YA POLIO SINDANO YA PILI

    May 09, 2025
  • DC MWENDA ATEMBELEA MRADI WA UJENZI WA SHULE MPYA YA SEKONDARI YA AMALI KITUKUTU

    May 08, 2025
  • KAMATI YA FEDHA, UONGOZI NA MIPANGO YA HALMASHAURI YA WILAYA YA IRAMBA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO

    May 06, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.