• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dkt. Rehema Nchimbi amewaapisha Wazee Wapya wa Baraza la Ardhi na Nyumba wilaya ya Iramba. Picha na Hemedi Munga

Posted on: January 16th, 2020

Hemedi Munga, Irambadc

tehama@irambadc.go.tz

Iramba. Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dkt. Rehema Nchimbi amewaapisha Wazee Wapya wa Baraza la Ardhi na Nyumba wilaya ya Iramba ambapo watahudumia kwa kipindi cha miaka mitatu.

Tukio la kuwaapisha Wazee hao limefanyika leo   Alhamisi Januari 16, 2020 katika ukumbi wa Mkuu wa Wilaya hiyo.

Wazee wa nne wa Baraza hilo ambao wameapishwa leo ni Agness Mbazi, Ainess Shimba, Omari Hassan na Fanuel Kiula kuchukuwa nafasi ya Paulo Sankey, Joram Masenga na Elimamba Lula ambao wamemaliza muda wao.

Dkt, Nchimbi amewaambia Wazee hao kuwa thamani ya kiapo chao ni kudhihirisha matunda na matokeo ya utumishi wao kwa wananchi.

Huku akiwataka kuthamini ardhi kwani kufanya mambo kinyume na maadili ardhini sio tu kunaikosea ardhi ispokuwa ni kulifanyia kosa Taifa kwa kuwa linajengwa na Ardhi.

“Tanzania bila ardhi haiwezi kuwepo, Mataifa makubwa ni Ardhi,” alisisitiza Dkt Nchimbi

Mkuu huyo amefafanuwa kuwa ardhi ni uchumi wa mtu mmoja mmoja na Taifa ambapo Tanzania ya viwanda haiwezi kuwepo pasipo ardhi.

Aidha amewaomba Wazee  hao kutumia muda mwingi kutoa elimu kwa watendaji wa kata, walimu wa shule wanazoweza kuzifikia na wananchi kwa ujumla ili kujenga uwelewa wa pamoja.

“Mwiba hutokea ulipoingilia, nanyi Baraza la Ardhi mkikaa salama mtatatuwa migogoro ya ardhi kwa kuwa mnajuwa namna ilivyoanza,” amesema Dkt, Nchimbi

Pia amewataka kuepuka rushwa na kupindisha haki wakati wakiwahudumia wananchi huku akiwahimiza kuwa mfano wa kuingwa , kujifunzia nakuwa namba moja kimkoa.

Kwa upande wake Katibu Tawala wa Mkoa huo, Dkt. Angelina Lutambi amewataka Wazee hao kufahamu kuwa kuna migogoro mingi wanayopaswa kuitatuwa kwa hekima zao.

“ Mlipo apishwa mmekabidhiwa jukumu zito na nikiwatazama ninawaona mmejaa hekima,” amesema Dkt, Lutambi

Amewafafanulia kuwa mwananchi anapofika kwao anamatumaini kupata haki kwa kutumia miiko ya katiba, sheria na vigezo vinavyotumika kwa uwadilifu.

“ Tunaweka imani kwenu kuwa maamuzi mtakayoyatoa katika Baraza la Ardhi hayata iletea serikali picha mbaya wala mabango pindi viongozi wakitaifa watakapotembelea wilayani Iramba,” amesisitiza Lutambi

Naye Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Emmanuel Luhahula amewataka Wazee hao kutambuwa kuwa wanalojukumu la kuhudumia wilaya ya Iramba na Mkalama.

Pia amewaagiza kutenda haki pindi watakapokuwa wakiwahudumia wananchi .

“ Haki huinuwa Taifa, mtakapo haribu haki, mtasababisha wananchi kuichukia serikali,” amesema Luhahula

 

Awali Mwenyekiti wa Baraza la Ardhi wa Halmashauri hiyo  , Baraka Shuma amesema Wazee wa Baraza ni kiungo muhimu na nisehemu ya Baraza.

“Baraza limekamilika na sasa tupo tayari kuwahudumia wanachi,” amesema Shuma

Waliohudhuria tukio hilo la kuapishwa Wazee wa Baraza wameonesha kuwa na imani na Baraza hilo kwa kuwa lina kiongozi wa dini ambaye ni mjumbe katika Baraza.                                                                                                                      

Wazee Wapya wa Baraza la Ardhi na Nyumba wilaya ya Iramba ambao wameapishwa leo Alhamisi 16, 2020 na Dkt, Rehema Nchimbi Mkuu wa Mkoa wa Singida. Picha na Hemedi Munga                                                                                     

Mmoja wa Wazee Wapya wa Baraza la Ardhi na Nyumba wilaya ya Iramba akiapa mbele ya Dkt, Rehema Nchimbi Mkuu wa Mkoa wa Singida. Picha na Hemedi Munga                                                                                                                    

Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dkt. Rehema Nchimbi akiwa katika picha ya pamoja na Wazee wa Baraza la Ardhi walioapishwa jeo Alhamisi Januari 16, 2020 kushoto kwake ni Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Emmanuel Luhahula na Kulia kwa Dkt, Nchimbi ni Katibu Tawala wa Mkoa wa Singida, Dkt. Angelina Lutambi. Picha na Hemedi Munga                                                                                                                                                                                                                                       

Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dkt. Rehema Nchimbi akiwa katika picha ya pamoja na Wazee wa Baraza la Ardhi walioapishwa jeo Alhamisi Januari 16, 2020 pamoja na viongozi malimbali wa dini. Picha na Hemedi Munga                                    

Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dkt. Rehema Nchimbi akiwa katika picha ya pamoja na Wazee wa Baraza la Ardhi walioapishwa jeo Alhamisi Januari 16, 2020 pamoja na waku wa Idara Mbalimbali za Halmashauri ya Wilaya ya Iramba. Picha na Hemedi Munga

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • KIDATO CHA KWANZA KURIPOTI SHULE January 13, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • MAAFISA ELIMU KATA 136 MKOANI SINGIDA WAPATIWA MAFUNZO KUHUSU USIMAMIZI WA SHULE NA UJAZAJI TAKWIMU KATIKA MFUMO WA "SIS"

    March 24, 2025
  • DC MWENDA AWASISITIZA WALIPA KODI KUFANYA MAKADIRIO YA KODI KABLA YA MACHI 31, 2025

    March 20, 2025
  • DC MWENDA NA WAZIRI MWIGULU NCHEMBA WACHANGIA JUMLA YA MADAWATI 98 SHULE YA MSINGI MSANSAO ILIYOPO KATA YA MTEKENTE

    March 10, 2025
  • WALIMU WAKUU 108 WA SHULE ZA MSINGI NA MAAFISA ELIMU KATA 20 WILAYANI IRAMBA WAPEWA MAFUNZO ENDELEVU YA USIMAMIZI WA UFUNDISHAJI NA UJIFUNZAJI FANISI KUPITIA JUMUIYA ZA KUJIFUNZA ZA WALIMU WAKUU NA MAAFISA ELIMU KATA

    March 19, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.