• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dkt. Rehema Nchimbi awaasa wanaume kuacha tabia ya kuwapa mimba wanafunzi ili watimize ndoto zao kupitia safari ya utafutaji wa elimu.

Posted on: June 18th, 2020

Hemedi Munga, Irambadc

tehama@irambadc.go.tz

Iramba. Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dkt. Rehema Nchimbi awaasa wanaume kuacha tabia ya kuwapa mimba wanafunzi ili watimize ndoto zao kupitia safari ya utafutaji wa elimu.

Dkt Nchimbi ametoa wito huo leo Juni 18, 2020 wakati wa ziara ya kukagua miradi ya maendeleo Shule ya Sekondari New Kiomboi mjini hapa.

Akiongea na hadhira katika hafla hiyo fupi, Dkt Nchimbi amesema kuwa angependa shule hiyo ingekua na kidato cha tano kutokana na miundombinu yake kuwa mizuri.

“Ndugu zangu natamani wakati ufike sasa Wanaume muache tabia ya kuwapa mimba wasichana ili watimize ndoto zao za maisha kupitia elimu,” amesema Dkt. Nchimbi na kuongeza kuwa

“Ndugu waandishi wa habari ni wakati wenu sasa nanyi mnaweza kutengeneza Makala mbalimbali za kuwaelimisha akina baba kuacha tabia mbaya ya kuwapa wanafunzi wa kike mimba.”

Katika hadhara hiyo, Dkt. Nchimbi ameishukuru Benki ya NMB kutoa vitanda kwa ajili ya bweni la wasichana  ili waweze kujisomea na kupata elimu nyakati za usiku kwa pamoja .

Halikadhalika, Dkt, Nchimbi ameiomba Benki kutoa elimu ya ujasiriamali kwa vijana wanaozunguka maeneo ya shule kutafuta wasichana badala yake wajikite na shughuli za kiuchumi.

“Tuwafundishe watoto wa kiume na wababa kuacha tabia ya kuharibu wasichana, ebu tuwakinge vijana kwa kuwapa elimu ya kuwaweka bize kimaendeleo” amesema Dkt. Nchimbi

Akiongea katika ziara hiyo Meneja wa Kanda ya Kati wa NMB, Nsolo Mlozi amesema kuwa benki ya NMB inarejesha faida kwa jamii, hivyo tumetenga kwa mwaka huu takribani bilioni mbili kwa ajili ya shughuli za maendeleo nchi nzima

“Mhe, Mkuu wa Mkoa katika wilaya ya Iramba pekee Benki ya NMB imetoa zaidi ya Tshs 29milioni kwa ajili ya shughuli za elimu na afya ili kuunga mkono juhudi za Rais wetu Dkt. John Magufuli,” amesema Mlozi na kuongeza kuwa

“Leo hii benki ya NMB imetoa vitanda ambavyo vitawasaidia wasichana katika bweni hili na hivyo kuwakinga na vijana wanaonyemelea wasichicha shuleni kuepuka mimba na kukatisha ndoto zao.”

Hata hivyo, Meneja Mlozi amesema pamoja na vitanda benki ya NMB imeweza kusaidia madawati katika shule mbalimbali za Halmashauri ya Wilaya ya Iramba.

Kwa upande wake Mkuu wa Shule hiyo, Amdeus Kiduu ameishukuru Benki ya NMB kwa msaada wa vitanda katika shule hii ambapo vitasaidia wasichana wanatoka mbali na shule hii kupata malazi.

Naye Dada Mkuu wa wanafunzi katika shule hiyo, Martina John amesma kuwa msaada huo wa vitanda utawafanya waweze kusoma kwa bidii ili kukuza taaluma na kuweza kufaulu mitihani yao kwenda kidato cha tano

Pia, amesema uwepo wa bweni hilo utawapunguzia adha ya umbali mrefu, kuondoa mimba za utotoni na kuongeza muda wa kujisomea kwa pamoja, hivyo kuongeza kiwango cha ufaulu.

MWISHO

Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dkt. Rehema Nchimbi akikabidhiwa madawati na Meneja wa Kanda ya Kati wa NMB, Nsolo Mlozi kwa ajili ya wanafunmzi wa kike katika shule ya Sekonda New Kiomboi. Picha na Hemedi Munga

Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dkt. Rehema Nchimbi akiwa katika picha ya pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Emmanuel Luhahula pamoja na wataalamu mbalimbali na wanafunzi Shule ya Sekondari New Kiomboi. Picha na Hemedi Munga

Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Emmanuel Luhahula wakwanza kushoto akiwa pamoja na wataalamu wa Benki ya NMB katika viwanja vya Shule ya Sekondari New Kiomboi. Picha na Hemedi Munga


Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • KIDATO CHA KWANZA KURIPOTI SHULE January 13, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • MAAFISA ELIMU KATA 136 MKOANI SINGIDA WAPATIWA MAFUNZO KUHUSU USIMAMIZI WA SHULE NA UJAZAJI TAKWIMU KATIKA MFUMO WA "SIS"

    March 24, 2025
  • DC MWENDA AWASISITIZA WALIPA KODI KUFANYA MAKADIRIO YA KODI KABLA YA MACHI 31, 2025

    March 20, 2025
  • DC MWENDA NA WAZIRI MWIGULU NCHEMBA WACHANGIA JUMLA YA MADAWATI 98 SHULE YA MSINGI MSANSAO ILIYOPO KATA YA MTEKENTE

    March 10, 2025
  • WALIMU WAKUU 108 WA SHULE ZA MSINGI NA MAAFISA ELIMU KATA 20 WILAYANI IRAMBA WAPEWA MAFUNZO ENDELEVU YA USIMAMIZI WA UFUNDISHAJI NA UJIFUNZAJI FANISI KUPITIA JUMUIYA ZA KUJIFUNZA ZA WALIMU WAKUU NA MAAFISA ELIMU KATA

    March 19, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.