• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Comments |
Iramba District Council
Iramba District Council

The United Republic of Tanzania Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Iramba District Council

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dkt Rehema Nchimbi kushoto akimkabidhi Mwenge wa Uhuru Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Aggrey Mwandri kulia. Picha na Hemedi Munga

Posted on: August 26th, 2019

Hemedi Munga, IrambaDC

tehema@singidadc.go.tz

Iramba – Singida. Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dkt. Rehema Nchimbi ameukabidhi Mwenge wa Uhuru 2019, kwa Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Aggrey Mwandri   leo Agosti 26, 2019 Mgongoro mpakani mwa  Singida na Tabora.

Akikabidhi Mwenge huo, Dkt. Nchimbi amemueleza Mkuu wa Mkoa wa Tabora  kuwa mwenge wa Uhuru,  unawaka,  unameremeta,  na kwa heshima zote za kumuwakilisha Rais Jonh Pombe Magufuli pamoja na itifaki yote ya mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa 2019  ipo  salama.

Akitoa taarifa fupi ya mbio za Mwenge wa Uhuru, Dkt. Nchimbi amesema kuwa Mwenge wa Uhuru umekimbizwa kwa siku saba sawa na kilometa   804.8  katika Halmashauri saba  za mkoa wa Singida huku ukiwa umepitia jumla ya miradi 46.

Miradi ambayo inahusu sekta ya elimu, afya, mazingira, maji, utawala bora, kilimo, ushirika, biashara, elimu ya mpiga kura, program za mapambano dhidi ya dawa za kulevya, malaria, rushwa na UkIMWI. Aliongeza Nchimbi

Akieleza suluhisho la  vijana walio maliza JKT wa oparesheni Magufuli, oparesheni  Kikwete na oparesheni nyinginezo Mkoani Singida  amewataka vijana kuchukua mizinga ili wafuge nyuki wajipatie kipato kizuri  na waachane na ukataji wa miti  unaoharibu mazingira.

Ameyasema hayo mbele ya mkimbiza mwenge kitafa, Ndugu Mzee Ali ukiwa ni mkakati wa pili unaoitwa achia shoka kamata  mzinga ulioanzishwa mkoani Singida kwa lengo la kuachana na ukataji wa miti kwa ajili ya kuchoma mkaa kutafuta kipato.

“Tumesema waachie shoka wakamate mzinga, ukiwa na mizinga ukifuga nyuki, unatunza mazingira ambayo ni vyanzo vya maji.” Alisema nchimbi

Mkakati wapili unakuja baada ya kufanikwa kwa mkakati wakwanza uliotabulika kama mshahara wangu uko wapi wenye lengo la kuhakikisha kuwa watumishi wa umma wanaona mishahara yao na kumpenda muajiri wao.

Mkakati huo ulizinduliwa na mbio za mwenge wa Uhuru Kitaifa mwaka  2018 na watumishi wameweza kuonesha mishahara yao kupitia kilimo,ufugaji, ufundi, uvuvi, ujasiriamali na mambo mengine na kuweza kuwa na miradi inayowawezesha kuwaajiri wengine.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Aggrey Mwandri amekiri kuupokea Mwenge wa Uhuru 2019 na kuahidi kuulinda Mwenge wa Uhuru pamoja na wakimbiza mwenge kitafa kwa siku zote watakazokuwa Mkoani Tabora.

Announcements

  • TANGAZO KUHUSU UJIO WA MADAKTARI BINGWA HOSPITALI YA WILAYA YA IRAMBA-KIOMBOI February 20, 2026
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU January 02, 2026
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • View All

Latest News

  • MAONESHO YA MATUMIZI YA PEMBEJEO ZA KILIMO (MBEGU, MBOLEA NA VIUATILIFU) HALMASHAURI YA WILAYA YA IRAMBA DISEMBA 29-30, 2025

    December 28, 2025
  • HERI YA SIKUKUU YA KRISMASI NA MWAKA MPYA 2026

    December 25, 2025
  • DC MWENDA AWATAKA WALIMU IRAMBA KUONGEZA UBUNIFU NA BIDII KUINUA UFAULU

    December 09, 2025
  • HERI YA MIAKA 64 YA UHURU WA TANZANIA BARA

    December 09, 2025
  • View All

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
More Videos

Quick Links

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Related Links

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    KIOMBOI, IRAMBA

    Postal Address: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Telephone: 026 - 2532253

    Mobile: 026 - 2533001

    Email: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.