• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Mkuu wa mkoa wa Singida Mhe : Dkt Rehema Nchimbi amefanya ziara ya kukagua shughuli za uvunaji na uuzaji wa zao la pamba kwenye vijjiji vya mtoa, msai kata ya mtoa tarafa ya Ndago wilayani Iramba leo tarehe 20/06/2019.

Posted on: June 29th, 2019

Mkuu wa mkoa wa Singida Mhe : Dkt Rehema Nchimbi amefanya ziara ya kukagua shughuli za uvunaji na uuzaji wa zao la pamba kwenye vijjiji vya mtoa, msai kata ya mtoa tarafa ya Ndago wilayani Iramba leo tarehe 20/06/2019.

Mkuu wa mkoa wa Singida Mhe: Dkt Rehema Nchimbi aliyeambatana na Mkuu wa Wilaya ya Iramba Mhe. Emmanuel Luhahula, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba Mwl. Linno Mwageni, Viongozi wa Mkoa wa Singida na Viongozi wa Halmashauri ya wilaya ya Iramba wamefanya ziara hiyo katika vijiji vya Msai na Mtoa.

Akizungunza na wananchi wa kata ya Mtoa Dkt Nchimbi amesema nimekuja kujionea zoezi la uvunaji na uuzaji, kama linaenda vizuri na pamba yote inayopokelewa na vyama vya Ushirika ni ile iliyo katika ubora unaohitajika.

Vile vile Dkt Nchimbi ameagiza uongozi kuanzia ngazi ya kijiji hadi wilaya kuhakikisha wanasimamia zoezi la malipo kwa wakulima na kuhakikisha kwamba wanaouza pamba wote wanalipwa hapo hapo na ni marufuku mnunuzi kumkopa mkulima.

Pamoja na wingi huu wa pamba ambao tumezalisha katika wilaya yetu ya Iramba na katika mkoa wetu wa Singida, faraja kubwa tuliyonayo mnunuzi tuliyenaye amesema atanunua pamba yote kilo ni Tshs 1200, Viongozi wote lazima muwe macho na yeyote ambaye atajitokeza kudanganya wakulima lazima kupambana nae, mnunuzi wa pamba ni BioSustain.

Mkuu wa mkoa wa Singida Mhe: Dkt Rehema Nchimbi amewataka wananchi wa wilaya hiyo kuhakikisha wanatumia vizuri fedha wanazozipata kutokana na mauzo ya zao la pamba.

Ameongeza kusema ni vema wakatumia fedha hizo kwa ajili ya kujiletea maendeleo katika familia zao, kununua chakula, kuwapatia mahitaji muhimu watoto wao ili kuwaendeleza kielimu ikiwa ni pamoja na ujenzi wa nyumba bora na za kisasa.

Wakulima ambao walizungumza kwa nyakati tofauti, walitumia fursa hiyo kumshukuru Rais Dkt. John Magufuli kwa kuhamasisha wananchi walime zao la pamba, na kuwagawia pembejeo bure bila gharama yeyote na sasa wameanza kuona mafanikio.

Dkt Nchimbi amewashauri wakulima wa pamba baada ya kuuza pamba fedha zao zilipwe kupitia akaunti za benki au kwa kutumia M-pesa, Airtel Money n.k ili kuwa na usalama wa fedha zao. Aliongeza kusema wakulima walipwe kwa wakati na kwa kuzingatia sheria za ununuzi wa pamba pamoja na usafi na ubora wa pamba. Dkt Nchimbi alisema usafi na ubora wa pamba ni suala ambalo linapewa kipaumbele kikubwa kwa sababu uchafu kwenye pamba unaathiri ubora na sifa ya pamba katika soko la dunia.

Tangazo

  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI June 05, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • DC MWENDA ATEMBELEA MRADI WA UJENZI WA SHULE MPYA YA SEKONDARI YA AMALI KITUKUTU

    May 08, 2025
  • KAMATI YA FEDHA, UONGOZI NA MIPANGO YA HALMASHAURI YA WILAYA YA IRAMBA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO

    May 06, 2025
  • DC MWENDA ATOA WITO KWA WALIMU WA SHULE ZA MSINGI KUIMARISHA UFUNDISHAJI KWA MADARASA YA MITIHANI

    May 06, 2025
  • JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI WILAYANI IRAMBA LATOA ELIMU YA KINGA DHIDI MAJANGA YA MOTO KWA MADIWANI NA WANANCHI

    May 02, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.