• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Comments |
Iramba District Council
Iramba District Council

The United Republic of Tanzania Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Iramba District Council

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Mkuu wa mkoa wa Singida Mhe. Dkt Rehema Nchimbi ameongoza maadhimisho ya siku ya mtoto Afrika yaliyofanyika kijiji cha Doromoni kata ya Tulya Tarafa ya Kisiriri wilaya ya Iramba Mkoa wa Singida

Posted on: June 16th, 2018

Mkuu wa mkoa wa Singida Mhe. Dkt Rehema Nchimbi ameongoza maadhimisho ya siku ya mtoto Afrika yaliyofanyika kijiji cha Doromoni kata ya Tulya Tarafa ya Kisiriri wilaya ya Iramba Mkoa wa Singida leo tarehe 16/06/2018.

 Dkt Rehema Nchimbi ameungana na Mkuu wa wilaya ya Iramba Mhe. Emmanuel Luhahula, Mkurugenzi mtendajiwa Halmashauri ya wilaya ya Iramba Mwl Linno Mwageni, viongozi wa mkoa wa Singida, viongozi wa Halmashauri ya wilaya ya Iramba na wananchi kuadhimisha siku ya mtoto Afrika.

 Chimbuko la Maadhimisho haya ni Azimio lililopitishwa na uliokuwa Umoja wa Nchi Huru za Afrika mwaka 1990 kwa lengo la kuwakumbuka watoto wa kitongoji cha Soweto nchini Afrika ya Kusini waliouawa tarehe 16 Juni, 1976 kutokana na ubaguzi warangi. Watoto hao walikuwa wakidai haki zao za kutobaguliwa pamoja na haki nyingine za   kibinadamu ikiwemo haki ya kupata elimu bora na hivyo kupinga mifumo ya elimu ya kibaguzi. Kufuatia tukio hili, Umoja wa Nchi Huru za Afrika iliazimia kuwa tarehe 16 Juni ya kila mwaka iwe Siku ya Mtoto wa Afrika.

 Dkt. Nchimbiakizungumza kwenye maadhimisho hayo amesema maadhimisho ya mtoto afrika ni fursa ya kutathimini utekelezaji wa Sera za Taifa zinazohusu maendeleo ya mtoto kwa kuwapatia huduma stahiki ikiwa ni pamoja na afya, elimu, ulinzi na   malezi bora ili wawe tunu ya taifa na familia kwa ujumla, Kauli mbiu ikiwa UCHUMI WA VIWANDA TUSIMUACHE MTOTO NYUMA. Elimu bora utegemea afya bora yake (Miwani ni Tiba). 

Aidha Dkt. Nchimbi amewataka wazazi kuwajali na kuwapenda watoto wao kwani waliwaleta duniani kwa mapenzi yao wenyewe yawapasa kuwalea na kuwakinga na ukatili wa kijinsia. Ameongeza kwa kusema wazazi wanawajibika kikamilifu katika kuhakikisha watoto wao wanapata elimu, kuwalinda na ukatili wa kijinsia pamoja na kupinga ndoa za utotoni ambazo zinawakatisha watoto masomo.

 Katika sherehe yamaadhimisho ya mtoto Afrika, pia Dkt Nchimbi amezindua upimaji wa macho na chanjo ya mtoto pamoja na kuchangia Shilingi laki moja (100,000) ili watoto wapimwe macho na miwani

 Vile vile Dkt Nchimbi amegiza shule zote za sekondari mkoani Singida kulima heka moja ya alizeti, kuandaa bwawa la samaki, kujenga na kukarabati chumba kimoja cha maabara na ameahidi kutoa zawadi ya pikipiki kwa shule nne zitakazo ongeza ufaulu mkoani singida.

Announcements

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU January 02, 2026
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI June 05, 2025
  • View All

Latest News

  • MAONESHO YA MATUMIZI YA PEMBEJEO ZA KILIMO (MBEGU, MBOLEA NA VIUATILIFU) HALMASHAURI YA WILAYA YA IRAMBA DISEMBA 29-30, 2025

    December 28, 2025
  • HERI YA SIKUKUU YA KRISMASI NA MWAKA MPYA 2026

    December 25, 2025
  • DC MWENDA AWATAKA WALIMU IRAMBA KUONGEZA UBUNIFU NA BIDII KUINUA UFAULU

    December 09, 2025
  • HERI YA MIAKA 64 YA UHURU WA TANZANIA BARA

    December 09, 2025
  • View All

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
More Videos

Quick Links

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Related Links

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    KIOMBOI, IRAMBA

    Postal Address: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Telephone: 026 - 2532253

    Mobile: 026 - 2533001

    Email: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.