• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

MKUU WA WILAYA IRAMBA AONGOZA KIKAO CHA TATHMINI YA MKATABA WA LISHE “JIONGEZE TUWAVUSHE SALAMA ROBO YA TATU YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025

Posted on: May 20th, 2025

MKUU WA WILAYA IRAMBA AONGOZA KIKAO CHA TATHMINI YA MKATABA WA LISHE “JIONGEZE TUWAVUSHE SALAMA ROBO YA TATU YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025


Iramba, Singida – Mei 20, 2025


Mkuu wa Wilaya ya Iramba mkoani Singida, Suleiman Yusuph Mwenda, ameongoza kikao cha tathmini ya mkataba wa lishe wa Jiongeze Tuwavushe Salama katika ngazi ya wilaya kwa robo ya tatu ya mwaka wa fedha 2024/2025 kuanzia Januari hadi Machi 2025. Kikao hicho kimefanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba.


Akizungumza katika kikao hicho, DC Mwenda amesisitiza umuhimu wa kuendelea kuwekeza katika lishe bora kwa watoto, akieleza kuwa afya njema ya watoto ndiyo msingi wa taifa lenye watu wenye tija na uchumi imara. Ameeleza kuwa lishe bora ni msingi wa maendeleo ya mtu binafsi na ya taifa kwa ujumla.


“Tunapozungumzia lishe, tunazungumzia uwekezaji wa moja kwa moja katika rasilimali watu. Taifa letu linahitaji watu wenye afya bora ili waweze kushiriki kikamilifu katika uzalishaji na kulisaidia taifa kuepuka kuwa na wategemezi wengi,” alisema DC Mwenda.


Aidha, Mkuu huyo wa Wilaya amewakumbusha wajumbe kuwa suala la lishe ni ajenda ya kitaifa inayopewa kipaumbele na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan. Ameeleza kuwa maagizo ya Rais kuhusu lishe yanapaswa kutekelezwa kwa ufanisi mkubwa kwa kuwa na mikakati endelevu katika ngazi zote za utawala.


Kikao hicho kilihusisha maafisa kutoka idara mbalimbali, wadau wa afya na lishe, waliopo katika Wilaya ya Iramba, ambao kwa pamoja walieleza dhamira ya pamoja katika kuhakikisha lishe bora inakuwa sehemu ya ajenda ya maendeleo ya wilaya.


Mwisho wa kikao, wajumbe walikubaliana kuongeza jitihada katika kutoa elimu ya lishe kwa jamii na kufuatilia utekelezaji wa mikakati ya lishe kwa watoto na wajawazito ili kufikia malengo ya kitaifa ya kuwa na taifa lenye afya bora na uchumi imara.

Tangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA MADIWANI KUJADILI NA KUPOKEA TAARIFA YA CAG MWAKA WA FEDHA 2023/2024 TAREHE 18, JUNI 2025 June 16, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI June 05, 2025
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • SERIKALI YAWAHIMIZA WAFUGAJI MKOANI SINGIDA KULINDA MIFUGO KUPITIA CHANJO NA UTAMBUZI

    July 08, 2025
  • HERI YA SIKUKUU YA SABASABA 2025

    July 07, 2025
  • TRA IRAMBA YAVUKA MALENGO YA UKUSANYAJI KODI KWA ASILIMIA 130, YAWASHUKURU WALIPAKODI

    July 01, 2025
  • DC MWENDA AKABIDHI SPIKA KWA MAAFISA MAENDELEO YA JAMII IRAMBA

    July 01, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.