• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Comments |
Iramba District Council
Iramba District Council

The United Republic of Tanzania Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Iramba District Council

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

MKUU WA WILAYA IRAMBA AONGOZA KIKAO CHA TATHMINI YA MKATABA WA LISHE “JIONGEZE TUWAVUSHE SALAMA ROBO YA TATU YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025

Posted on: May 20th, 2025

MKUU WA WILAYA IRAMBA AONGOZA KIKAO CHA TATHMINI YA MKATABA WA LISHE “JIONGEZE TUWAVUSHE SALAMA ROBO YA TATU YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025


Iramba, Singida – Mei 20, 2025


Mkuu wa Wilaya ya Iramba mkoani Singida, Suleiman Yusuph Mwenda, ameongoza kikao cha tathmini ya mkataba wa lishe wa Jiongeze Tuwavushe Salama katika ngazi ya wilaya kwa robo ya tatu ya mwaka wa fedha 2024/2025 kuanzia Januari hadi Machi 2025. Kikao hicho kimefanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba.


Akizungumza katika kikao hicho, DC Mwenda amesisitiza umuhimu wa kuendelea kuwekeza katika lishe bora kwa watoto, akieleza kuwa afya njema ya watoto ndiyo msingi wa taifa lenye watu wenye tija na uchumi imara. Ameeleza kuwa lishe bora ni msingi wa maendeleo ya mtu binafsi na ya taifa kwa ujumla.


“Tunapozungumzia lishe, tunazungumzia uwekezaji wa moja kwa moja katika rasilimali watu. Taifa letu linahitaji watu wenye afya bora ili waweze kushiriki kikamilifu katika uzalishaji na kulisaidia taifa kuepuka kuwa na wategemezi wengi,” alisema DC Mwenda.


Aidha, Mkuu huyo wa Wilaya amewakumbusha wajumbe kuwa suala la lishe ni ajenda ya kitaifa inayopewa kipaumbele na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan. Ameeleza kuwa maagizo ya Rais kuhusu lishe yanapaswa kutekelezwa kwa ufanisi mkubwa kwa kuwa na mikakati endelevu katika ngazi zote za utawala.


Kikao hicho kilihusisha maafisa kutoka idara mbalimbali, wadau wa afya na lishe, waliopo katika Wilaya ya Iramba, ambao kwa pamoja walieleza dhamira ya pamoja katika kuhakikisha lishe bora inakuwa sehemu ya ajenda ya maendeleo ya wilaya.


Mwisho wa kikao, wajumbe walikubaliana kuongeza jitihada katika kutoa elimu ya lishe kwa jamii na kufuatilia utekelezaji wa mikakati ya lishe kwa watoto na wajawazito ili kufikia malengo ya kitaifa ya kuwa na taifa lenye afya bora na uchumi imara.

Announcements

  • TANGAZO KUHUSU UJIO WA MADAKTARI BINGWA HOSPITALI YA WILAYA YA IRAMBA-KIOMBOI February 20, 2026
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU January 02, 2026
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • View All

Latest News

  • MAONESHO YA MATUMIZI YA PEMBEJEO ZA KILIMO (MBEGU, MBOLEA NA VIUATILIFU) HALMASHAURI YA WILAYA YA IRAMBA DISEMBA 29-30, 2025

    December 28, 2025
  • HERI YA SIKUKUU YA KRISMASI NA MWAKA MPYA 2026

    December 25, 2025
  • DC MWENDA AWATAKA WALIMU IRAMBA KUONGEZA UBUNIFU NA BIDII KUINUA UFAULU

    December 09, 2025
  • HERI YA MIAKA 64 YA UHURU WA TANZANIA BARA

    December 09, 2025
  • View All

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
More Videos

Quick Links

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Related Links

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    KIOMBOI, IRAMBA

    Postal Address: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Telephone: 026 - 2532253

    Mobile: 026 - 2533001

    Email: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.