• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Emmanuel Luhahula agawa zawadi kwa wanafunzi 10 waliofaulu vizuri katika mtihani wa kumaliza elimu ya msingi 2020.

Posted on: January 8th, 2021

Hemedi Munga, Irambadc

irambadc@singida.go.tz

Iramba. Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Emmanuel Luhahula amewaagiza Maafisa Elimu Kata kuendelea kusimamia kwa ukaribu shule zilizopo katika kata zao ili kuinua ufaulu wa Wanafunzi katika shule zilipo Wilayani Iramba Mkoa wa Singida.

 

Luhahula ameyasema hayo leo Ijumaa Januari 8, 2021 katika Ukumbi mdogo wa Halmashauri hiyo wakati akigawa zawadi kwa wanafunzi waliofaulu vizuri mtihani wa darasa la saba na kupangiwa shule mbalimbali Nchini.

 

“Tunataka hamasa hii ya ugawaji wa zawadi iwainue wanafunizi wote kitaaluma na kufaulu mitihani yao hatimae kuinua Iramba yetu” amesisitiza Mkuu wa Wilaya

Kufuatia Maafisa Elimu Kata kupata posho ya Madaraka na kugawiwa pikipiki kwa lengo la kufanikisha usimamizi wa shule zilizopo katika kata zao, amewagawia mataili ya pikipiki hizo na kuwaasa kuzitumia pikipiki hizo kuzunguka katika maeneo yao kusimamia taaluma.

“Hakikisheni mnazunguka katika kata zenu na kusimamia yale yote tuliyokubaliana katika kikao cha Wadau wa Elimu Wilayani Iramba.”

Pia amewataka Maafisa Elimu Kata hao kuhakikisha wanakua na utaratibu wa kusikiliza kero za wananchi wanaowazunguka katika kata zao.

Awali akiwasilisha taarifa fupi ya wanafunzi waliofaulu vizuri na kuzawadiwa zawadi zilizoandaliwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo, Afisa Elimu Msingi wa Halmashauri, Chacha Kehogo amesema kuwa wanatoa zawadi kwa wanafunzi waliofaulu vizuri na kuwapatia Maafisa Elimu Kata vitendea kazi kwa lengo la kuhakikisha wanasimamia taaluma kwa ukaribu katika kata zao.

“Tumetoa mataili 40 kwa Maafisa Elimu Kata ili kuwawezesha kuzunguka na kufuatilia taaluma katika shule zao,” amesema Kehogo na kuongeza kuwa

“Ufaulu mzuri walioupata wanafunzi 10 katika mtihani wa kumaliza elimu ya msingi 2020 umewawezeshesha wanafunzi hao kupangiwa shule nzuri Nchini.”

Kehogo amebainisha kuwa mwanafunzi Raphael Maganza amepangiwa Tabora Boys, Benedict Isaya amepangiwa Kibaha, Vailet Jackosn amepangiwa Tabora Girls, Gwakisa Mwakijungu amepangiwa Mzumbe na Sixbert Sabigoro amepangiwa Ilboru.

Wakati Yunusu Swalehe amepangiwa Iyunga Technical, Mary Mkumbo amepangiwa Msalato, Benson Makule amepangiwa Ifunda Technical, Gift Kileo amepangiwa Mtwara Technical na Saada  Mnyinga amepangiwa Balangdalalu.

Akiongea na Mwandishi wetu mmoja wa wanafunzi waliopewa zawadi kwa niaba ya wenzake Gift Kileo amewashukuru viongozi wa Wilaya ya Iramba kwa kufanikisha zoezi la utoaji wa zawadi ambazo zitasabisha Wanafunzi hao wafikie ndoto zao.

“Kwa kweli tunashukuru kupata zawadi hizi na kwa shule tulizopangiwa tunamatumani makubwa ndoto zetu zitatimia” amesema Kileo na kuongeza kuwa

“Ninaamini zawadi hizi tulizopewa zitatusaidia katika masomo yetu huko tuendako.”

Kwa upande wake mmoja wa wazazi waliohudhuria hafla hiyo fupi, Vaileti     Mbigu amewaasa wazazi wenzake kuwalea na kuwatunza wanafunzi waliopo katika shule mbalimbali ili waweze kutimiza ndoto zao.

“Niwaombe wazazi wenzangu tuwatunze na kuwaelekeza watoto wetu vizuri wanapokua katika hatua mbalimbali za masomo na katu tusiwakatize ndoto zao,” ameomba Mbigu na kuongeza kuwa

“Niwaombe mfahamu kuwa watoto hawa ni mali ya Taifa na watakuwa na uwezo wa kulinda Taifa letu kwa kutumia maarifa wanayoyapata na watakayo yapata katika elimu ya juu.”

MWISHO

Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Emmanuel Luhahula agawa  mataili ya pikipiki 40  kwa Maafisa Elimu Kata na kuwataka kwenda kusimamia taaluma kwa ukaribu ili kuinua taaluma na ufaulu Wilayani Iramba Mkoa wa Singida. Wakwanza kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Emmanuel Luhahula, wakatikati ni Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba, Linno Mwageni na wamwisho kushoto ni Afisa Elimu Msingi wa Halmashuri hiyo, Chacha Kehogo.Picha na Hemedi Munga

Afisa Elimu Msingi, Chacha Kehogo akifafanua wanafunzi waliopangiwa shule mbalimbali Nchini,  ambapo mwanafunzi Raphael Maganza amepangiwa Tabora Boys, Benedict Isaya amepangiwa Kibaha, Vailet Jackosn amepangiwa Tabora Girls, Gwakisa Mwakijungu amepangiwa Mzumbe na Sixbert Sabigoro amepangiwa Ilboru. Wakati Yunusu Swalehe amepangiwa Iyunga Technical, Mary Mkumbo amepangiwa Msalato, Benson Makule amepangiwa Ifunda Technical, Gift Kileo amepangiwa Mtwara Technical na Saada  Mnyinga amepangiwa Balangdalalu. Picha na Hemedi Munga

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba, Linno Mwageni akiwaasa wanafunzi waliochaguliwa kwenda shule mbalimbali Nchini kuto iga tabia za wale watakaokutana nao, vitu vyao na kuridhika na kile watakachokuwa wanapewa na wazazi wao. Alio kaa ni Afisa Elimu Msingi Chacha Kehogo. Picha na Hemedi Munga

Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Emmanuel Luhahula akiwa katika picha ya pamoja na wanafunzi mbalimbali waliochaguliwa katika shule mbalmbali Nchini. Picha na Hemedi Munga

Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Emmanuel Luhahula akiwa katika picha ya pamoja na Maafisa Elimu Kata. Picha na Hemedi Munga


Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • KIDATO CHA KWANZA KURIPOTI SHULE January 13, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • MAAFISA ELIMU KATA 136 MKOANI SINGIDA WAPATIWA MAFUNZO KUHUSU USIMAMIZI WA SHULE NA UJAZAJI TAKWIMU KATIKA MFUMO WA "SIS"

    March 24, 2025
  • DC MWENDA AWASISITIZA WALIPA KODI KUFANYA MAKADIRIO YA KODI KABLA YA MACHI 31, 2025

    March 20, 2025
  • DC MWENDA NA WAZIRI MWIGULU NCHEMBA WACHANGIA JUMLA YA MADAWATI 98 SHULE YA MSINGI MSANSAO ILIYOPO KATA YA MTEKENTE

    March 10, 2025
  • WALIMU WAKUU 108 WA SHULE ZA MSINGI NA MAAFISA ELIMU KATA 20 WILAYANI IRAMBA WAPEWA MAFUNZO ENDELEVU YA USIMAMIZI WA UFUNDISHAJI NA UJIFUNZAJI FANISI KUPITIA JUMUIYA ZA KUJIFUNZA ZA WALIMU WAKUU NA MAAFISA ELIMU KATA

    March 19, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.