• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Emmanuel Luhahula aitia moyo timu ya karantini kuwa vifaa vyote vinavyohitajika katika kupambana na kuchukua tahadhari ya maambukizi ya ugonjwa wa corona havitapungua.

Posted on: April 22nd, 2020

Hemedi Munga, Irambadc

tehama@irambadc.go.tz

Iramba. Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Emmanuel Luhahula ameihakikishia timu ya Karantini, Wataalam na Wajumbe wa Kamati ya Usalama ya Wilaya ya Iramba kuwa vifaa vyote vinavyohitajika katika kupambana na kuchukua tahadhari ya maambukizi ya ugonjwa wa corona havitapungua.

Luhahula ameyasema hayo leo Jumaa tano Aprili 22, 2020 wakati akiongea na timu ya karantini kuwatia moyo katika Ukumbi Mdogo wa Halmashauri hiyo mjini hapa.

Mkuu wa Wilaya hiyo amewaagiza  wataalam kuainisha vifaa vyote vinavyohitajika.

 “ Tutafanya kila kinachowezekana kuhakikisha kuwa vifaa ambavyo ni vya timu yetu iliyo mstari wa mbele havitapungua” amesisitiza Luhahula

Katika hatua nyingine, Luhahula amewashukuru watu wa Afya kwa ubunifu wa kutengeneza barakola kwa ajili ya jamii.

Pia amemuagiza  Mkurugenzi Mtendaji na Katibu Tawala wa Wilaya hiyo kutoa maelekezo kwa taasisi zilizo chini yao  kutengeneza vitu vya kunawia ambavyo havishikiwi na mkono.

“Ninaiomba timu ya karantini kuwekeza zaidi kwenye kinga kwa kuwa ndio usalama wetu ulipo, hivyo ninawatia moyo na tuendelee kumtegemea mungu,” amesema Luhahula na kuongeza

“ Ninaamini kuwa tukishikamana katika haya mapambano Mungu wetu atatusimamia.”

Halikadhalika amewataka viongozi wa timu hiyo kuratibu mambo yote mapema huku akiwatahadharisha wale wote watakao kua kikwazo au kuzembea kwa ajili ya wapiganaji hao kumchukulia hatua za kinidhamu mara moja.

“ Ndugu zangu nawatia moyo twendeni tukafanye kazi na tuwe na moyo mkuu,” amesisitiza Luhahula

Akiongea katika kikao hicho, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo, Linno Mwageni amewasisitiza Watendaji wa Kata na Vijiji kuendelea kuzibaini familia ambazo zinaingia katika maeneo mbalimbali ya Wilaya yetu kutoka mikoa mbalimbali.

“ Ninawakumbusha Watendaji wa Kata na Vijiji kuwa na takwimu za watu wanaokuja ili likitokea jambo iwe rahisi kufuatilia,” amesema Mwageni

Mapema akiwasilisha taarifa fupi mbele ya Mkuu wa Wilaya hiyo, Mganga Mkuu wa Wilaya hiyo, Daktari Hussein Sepoko amemuhakikishia Mkuu huyo kuwa mpaka leo hii Wilaya ya Iramba haijapata  muhisiwa wa ugonjwa wa corona ambaye amechukuliwa sampuli.

Sepoko amesema kupitia mikakati walioiweka katika timu ya karantini wameweza kupata Themo scana 5 ambazo zinatumika huku Idara ya Afya ikinunua spriers 8 kwa ajili ya upuliziaji.

Kuendelea kufikisha elimu ya ugonjwa wa corona katika maeneo hatarishi kama vile sehemu za bodaboda, minadani, machimboni, Doromoni kwenye uvuvi wa samaki, nyumba za ibada na kwenye Misiba.

“ Pia, tumefanya oparesheni katika stendi zetu za mabasi na kukuta wameweka sanitaiza na kufanya uchunguzi (screening) pindi mabasi yanapoingia toka mikoani,” amesema Sepoko

Naye Mjumbe wa Timu ya Karantini ya Wilaya hiyo, Afisa Muuguzi wa Hospitali ya Kiomboi,  Noela Vicent ameshauri kuwa watu wote wanaokuja kuona wagonjwa wawe wamevaa barakola.

Kwa upande wake  Mratibu wa uimarishaji ubora  wa huduma za Afya wa Wilaya hiyo, Daniel Paulo ameishauri kamati hiyo kuwafanyia uchunguzi wageni wote watokao mikoa yenye maambukizo.

Pia ameitaka jamii kuendelea kunawa kwa kutumia maji yanayotiririka na sabuni sahihi.

MWISHO

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba, Linno Mwageni akifafanua jambo wakati akiongea na timu ya karantini ya Wilaya hiyo. Picha na Hemedi Munga

Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba, Daktari Hussein Sepoko akitoa taarifa ya utekelezaji wa timu ya karantini ya Wilaya hiyo Mbele ya Mkuu wa Wilaya hiyo. Picha na  Hemedi Munga

Afisa Muuguzi wa Hospitali ya Kiomboi, Noel Vicent, akichangia mada katika kikao cha timu ya karantini kilichofanyika ukumbi Mdogo wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba. Picha na Hemedi Munga

Mratibu wa Uimarishaji Ubora wa Huduma za Afya wa Wilaya ya Iramba akichangia mada katika kikao cha timu ya karantini kilichofanyika ukumbi Mdogo wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba. Picha na Hemedi Munga

Wajumbe mbalimbali wa timu ya karantini wakifuatilia uchangiaji taarifa ya timu hiyo ukumbi Mdogo wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba. Picha na Hemedi Munga

Mfano mzuri wa chombo cha kanawia bila ya kushika kwa mikono. Picha na Hemedi Munga

Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Emmanuel Luhahula akinawa maji yanayotiririka toka katika chombo kinachobonyezwa kwa mguu kutoa maji na upande mwingine kutoa sabuni. Picha na Hemedi Munga

Katibu Tawala wa Wilaya ya Iramba, Pius Songoma akinawa maji yanayotiririka toka katika chombo kinachobonyezwa kwa mguu kutoa maji na upande mwingine kutoa sabuni. Picha na Hemedi Munga

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba, Linno Mwageni akinawa maji yanayotiririka toka katika chombo kinachobonyezwa kwa mguu kutoa maji na upande mwingine kutoa sabuni. Picha na Hemedi Munga

Mganga Mkuu wa Halamashauri ya Wilaya ya Iramba, Daktari Hussein Sepoko akinawa maji yanayotiririka toka katika chombo kinachotumiwa kwa mguu kutoa maji na upande mwingine kutoa sabuni. Picha na Hemedi Munga


Tangazo

  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI June 05, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • DC MWENDA ATEMBELEA MRADI WA UJENZI WA SHULE MPYA YA SEKONDARI YA AMALI KITUKUTU

    May 08, 2025
  • KAMATI YA FEDHA, UONGOZI NA MIPANGO YA HALMASHAURI YA WILAYA YA IRAMBA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO

    May 06, 2025
  • DC MWENDA ATOA WITO KWA WALIMU WA SHULE ZA MSINGI KUIMARISHA UFUNDISHAJI KWA MADARASA YA MITIHANI

    May 06, 2025
  • JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI WILAYANI IRAMBA LATOA ELIMU YA KINGA DHIDI MAJANGA YA MOTO KWA MADIWANI NA WANANCHI

    May 02, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.