• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Emmanuel Luhahula amefanya ziara kwenye kampuni ya SUN SHINE na Mgodini kuelimisha namna ya kujikinga na COVID 19.

Posted on: March 23rd, 2020

Hemedi Munga, Irambadc

tehama@irambadc.go.tz

Iramba. Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Emmanuel Luhahula amefanya ziara katika kampuni ya SUN SHINE iliyopo kijiji cha Konkilangi kata ya Ntwike Tarafa ya Shelui kutoa elimu ya kuchukua tahadhari kujikinga na maambukizi ya virusi vya korona.

Elimu hiyo ameitoa leo Jumatatu Machi 23, 2020 alipofanya ziara hiyo akiwa na kamati ya Usalama ya Wilaya katika kampuni hiyo inayojishughulisha na uchimbaji wa madini ya dhahabu.

Mkuu wa Wilaya hiyo amewataka wafanyakazi wa kampuni hiyo kufahamu kuwa mripuko wa ugonjwa huo umekua tishio katika mataifa mbalimbali duniani hivyo  kuwataka kuwa na vitakasa mikono kwa ajili ya kupaka mikononi ili kuua vijidudu vya ugonjwa huo.

Pia, amemuagiza meneja wa kampuni hiyo, ndugu Chen kuweka maji ya kuoshea mikono katika milango ya kuingilia na maeneo mbalimbali ya kampuni hiyo.

“ Ndugu zangu simamieni hayo maana afya ni zenu pia  ni zetu akiumia Mtanzania hapa Serikali tunapata hasara, Mheshimiwa Rais aliporuhusu wawekezaji kama hawa tunategemea tuone faida,” amesema Luhahula na kuongeza

“ Mhakikishe mnasimamia kutimiza  wajibu wenu.”

Akitaka kujua mmoja wa wafanyakazi wa kampuni hiyo, Hemedi Heri kuwa ndani ya kampuni hiyo kuna vitendea kazi kama nyundo na chepe ambavyo vinashikwa na kila mmoja kuhusu kujikinga na maambukuzi hayo watafanyaje.


Akijibu swali hilo, Mratibu wa uimarishaji ubora wa huduma za Afya Wilayani Iramba, Daniel Paul amesema kuwa vitakasa mikono vinapaswa kuwapo kila eneo kwa ajili ya kupaka kabla na baada ya kushika vifaa hivyo.

Paul amewatahadharisha  wananchi hao juu ya ugonjwa wa korona unaoambukizwa kwa maji maji yanayosambaa kwa  njia ya hewa  kutoka  kwa mtu mwenye maambukizi hayo anapokua anakohoa au kupiga chafya.

Halikadhalika, kugusa maji  maji yanayotoka puani (kamasi), kugusa kitambaa au nguo na vitu vingine vilivyokua vinatumika na mtu mwenye maambukizi ya ugonjwa wa korona.

Pia, amewataka kuzijua dalili za ugonjwa huo kua ni homa na mafua makali, kuumwa na kichwa, mwili kuchoka, kikohozi, kubanwa na mbavu, maumivu ya misuli, vidonda vya koo na kupumua kwa shida, hivyo waonapo dalili hizo kutoa taarifa kupitia namba za bure za 0800110124, 0800110125 na 0800110037 na kufika katika vituo vilivyotengwa kwa wagonjwa hao ili kupata matibabu haraka.

Amewashauri wananchi hao kuzifahamu mbinu za kujikinga na ugonjwa huo kuwa ni kukaa mbali mbali angalau kwa mita mbili, kuacha kupeana mikono, kukumbatiana au kubusiana, kufunika mdomo na pua wakati wa kukohoa au kupiga chafya kwa kitambaa safi au kwa kutumia kiwiko cha mkono, kukaa mbali na mtu yoyote  mwenye dalili za kifua au kikohozi na kunawa mikono mara kwa mara.

Naye katibu Tawala wa Wilaya hiyo, Pius Songoma amewataka wananchi hao kufahamu kuwa serikali inapita kuhakikisha kuwa wananchi wanafuata yale ambayo Serikali inataka.

“ Mhakikishe kuwa hamgusani, hamshikani mikono, hamkumbatiani, hambusiani, pia  mnakua na ndoo za kunawa maji yanayotiririka kwa sabuni pia kuwa na  sanitaiza.” amesema Songoma

Mkuu wa Wilaya hiyo ameambatana na kamati ya Usalama ya Wilaya na Wataalamu wa Afya kutoa elimu ya kujikinga na ugonjwa wa Korona.

Ziara hiyo imetembelea na kutoa elimu katika kampuni ya SUN SHINE, Mgodi  wa Sekenke kijiji cha Konkilangi

Kata ya Ntwike.

Pia imefika Mgodi wa Zambia uliopo kata ya Mgongo Tarafa ya Shelui.

MWISHO

Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Emmanuel Luhahula akiwaelimisha wananchi wa Mgodini Sekenke kijiji cha Konkilangi kata ya Ntwike Tarafa ya Shelui  namna ya kujikinga na ugonjwa wa Korona. Picha na Hemedi Munga

Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Emmanuel Luhahula akiwaelimisha wananchi wa Mgodi wa  Zambia  kata ya Mgongo  Tarafa ya Shelui  namna ya kujikinga na ugonjwa wa Korona. Picha na Hemedi Munga

Mratibu wa uimarishaji ubora wa huduma za Afya wilayani Iramba, Daiel Paul akielezea dalili mbalimbali na njia za kujikinga na ugonjwa wa korona Mgodini Sekenke kijiji cha Konkilangi kata ya Ntwike Tarafa ya Shelui. Picha na Hemedi Munga

Katibu Tawala wa Wilaya ya Iramba, Pius Songoma akinawa maji yanayotiririka na sabuni wakati alipotembelea akiwa na Mkuu wa Wilaya hiyo, Emmanuel Luhahula pamoja na kamati ya Usalama ya Wilaya hiyo kutoa elimu ya namna ya kujikinga na maambukizi ya ugonjwa wa korona Mgodini Sekenke kijiji cha Konkilangi kata ya Ntwike  Tarafa ya Shelui Wilyani Iramba. Picha na Hemedi Munga.

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • KIDATO CHA KWANZA KURIPOTI SHULE January 13, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • MAAFISA ELIMU KATA 136 MKOANI SINGIDA WAPATIWA MAFUNZO KUHUSU USIMAMIZI WA SHULE NA UJAZAJI TAKWIMU KATIKA MFUMO WA "SIS"

    March 24, 2025
  • DC MWENDA AWASISITIZA WALIPA KODI KUFANYA MAKADIRIO YA KODI KABLA YA MACHI 31, 2025

    March 20, 2025
  • DC MWENDA NA WAZIRI MWIGULU NCHEMBA WACHANGIA JUMLA YA MADAWATI 98 SHULE YA MSINGI MSANSAO ILIYOPO KATA YA MTEKENTE

    March 10, 2025
  • WALIMU WAKUU 108 WA SHULE ZA MSINGI NA MAAFISA ELIMU KATA 20 WILAYANI IRAMBA WAPEWA MAFUNZO ENDELEVU YA USIMAMIZI WA UFUNDISHAJI NA UJIFUNZAJI FANISI KUPITIA JUMUIYA ZA KUJIFUNZA ZA WALIMU WAKUU NA MAAFISA ELIMU KATA

    March 19, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.