• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Emmanuel Luhahula amegawa ndoo 150 na sabuni lita 664 kwa watoto wa kituo cha huduma ya mtoto Shiloh Student Center Kinampanda Wilayani Iramba kuendelea kujikinga na corona.

Posted on: June 6th, 2020

Hemedi Munga, Irambadc

tehama@irambadc.go.tz

Iramba. Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Emmanuel Luhahula amegawa ndoo za maji tiririka 150 na sabuni za maji lita 664 kwa familia 244 zenye Watoto katika kituo cha huduma ya mtoto Shiloh Student  Center kwa ajili kusaidia kupambana na maambukizi ya homa kali ya mapafu inayosabishwa na virusi vya corona.

 Mkuu huyo wa Wilaya amegawa vifaa hivyo leo Juni 4, 2020 wakati alipokua katika kanisa la TAG Shiloh Kinampanda Wilayani Iramba.

Ameziagiza familia hizo kwenda kutumia vifaa hivyo na sio kuziweka kuwa mapambo.

“Nendeni mkatumie vizuri na msiviweke kuwa mapambo ili kuendelea kujikinga na maambukizi ya virusi vya corona,” amesema Luhahula na kuongeza

 

“Matumizi hayo si tu yanawakinga na virusi vya corona bali yanawakinga na magonjwa yatokanayo na uchafu kama vile kipindupindu.”

Pia, amewatoa hofu Wananchi wa Kinampanda na kuwataka kuendelea kukitumia kituo cha Afya cha kinampanda kupata huduma za Afya kwa kua kipo salama.

“Ni kweli tulipendekeza Kituo cha Afya kinampanda ikiwa mgonjwa angepatikana angeletwa hapo, lakini mpaka leo tunavyoongea hakuna mgonjwa yeyote wa corona aliyeletwa kwenye kituo hicho,” ametilia mkazo Luhahula nakuongeza

“Kwa maana hiyo Iramba tuko salama hatujawahi kupata mgonjwa na si kwa ujanja wetu bali ni kwa uwezo wa Mwenyezi Mungu, hivyo tuendelee kumuomba Mungu na kuchukua tahadhari  kama wanavyoendelea kutuambia wataalam wa Afya.”

Halikadhalika, Mkuu huyo wa Wilaya ameahidi kutoa mifuko 20 ya simenti ikiwa ni sadaka yake ya kuendeleza ujenzi wa kanisa hilo.

Mapema akiwasilisha taarifa ya kituo cha huduma ya mtoto Shiloh Student Center chenye namba ya usajili TZ152, Mchungaji wa Kanisa la TAG, Noel Lameck amesema vifaa hivyo vimegarimu zaidi ya Tsh 2.26milioni ili kuiunga mkono Serikali katika mapambano ya kudhibiti maambukizi ya homa kali ya mapafu inayosababishwa na virusi vya corona.

Amesema kituo hicho kinawahudumia Watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu takribani 244 ambapo wasichana ni 128 na wavulana ni 116 ambao wanajipatia mafunzo ya elimu, kimwili, kijamii na kiroho.

Amefafanua kua kituo huwapatia vifaa vyote vinavyomsaidia mtoto mazingira ya kujifunza kama vile sare za shule, madaftari na kalamu na hugaramia matibabu pindi watoto wanapougua.

Halikadhalika, kituo kimeanzisha miradi ya ufugaji wa kuku kwa kaya 25, vikundi vya kuweka na kukopa kwa lengo la kujikwamua kiuchumi pamoja na kujenga nyumba mbili zilizokabidhiwa kwa walengwa.

Kwa upande wake mmoja wa wazazi mwenye mtoto katika kituo hicho baada ya kupokea msaada huo, Jane Timotheo amesema kuwa baadhi ya familia zilikua zinashindwa kununua ndoo, hivyo zikawa zinatengeneza vigaloni, kwa hiyo wanashukuru na wataendelea kufuata masharti kuhakikisha corona haita ingia kinampanda.

Naye mmoja wa watoto wanaopata huduma kituoni hapo, Samwel Richard amelishukuru Kanisa na kituo cha huduma cha mtoto kuwapatia ndoo na sabuni, hivyo wanaweza kunawa ili kujikinga na janga la corona.

“Msaada huo ni mkubwa maana wengine walikuwa hawana uwezo wa kununua ndoo na sabuni hivyo tunawaahidi kuwa tutavitumia vizuri ili kujikinga na corona,” amesema Richard

MWISHO

Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Emmanuel Luhahula akiwatoa hofu wananchi na waumini wa kanisa la TAG kinampanda kuendelea kupata huduma za Afya kituo cha Afya Kinampanda kwa sababu kipo salama. Picha na Hemedi Munga

Mchungaji wa Kanisa la TAG Tarafa ya Kinampanda Wilayani Iramba, Noel Lameck akifafanua namna wanavyo iunga mkono Serikali kupambana na maambukizi ya homa kali ya mapafu inayosababishwa na virusi vya corona kwa kutoa ndoo 150 na sabuni lita 664. Picha na Hemedi Munga

Afisa Tarafa wa Kinampanda Wilayani Iramba, Chotto Maingu akiongea na Waumini wa kanisa la TAG Tarafa ya Kinampanda Wilayani Iramba. Picha na Hemedi Munga

Baadhi ya ndoo na sabuni za maji zilizotolewa na kanisa la TAG Tarafa ya Kinampanda Wilayani Iramba chini ya Mchungaji Noel Lameck. Picha na Hemedi Munga

Tangazo

  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI June 05, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • DC MWENDA ATEMBELEA MRADI WA UJENZI WA SHULE MPYA YA SEKONDARI YA AMALI KITUKUTU

    May 08, 2025
  • KAMATI YA FEDHA, UONGOZI NA MIPANGO YA HALMASHAURI YA WILAYA YA IRAMBA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO

    May 06, 2025
  • DC MWENDA ATOA WITO KWA WALIMU WA SHULE ZA MSINGI KUIMARISHA UFUNDISHAJI KWA MADARASA YA MITIHANI

    May 06, 2025
  • JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI WILAYANI IRAMBA LATOA ELIMU YA KINGA DHIDI MAJANGA YA MOTO KWA MADIWANI NA WANANCHI

    May 02, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.