• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Emmanuel Luhahula amempongeza Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba, Linno Mwageni kwa kulipa deni la ujenzi wa Zahanati ya Ushora. Picha na Hemedi Munga

Posted on: November 29th, 2019

By Hemedi Munga, Irambadc

tehama@irambadc.go.tz

Iramba. Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Emmanuel Luhahula amempongeza Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba, Linno Mwageni kwa kulipa deni la ujenzi wa Zahanati ya Ushora.

Luhahula ameyaongea hayo leo Ijumaa Novemba 29, 2019  katika Ukumbi Mkubwa wa Halmashauri hiyo wakati wakiwa katika kikao cha tathimini ya mbio za Mwenge wa Uhuru wilayani humo 2019.

Akiongea katika kikao hicho Mkuu wa Wilaya hiyo, amewataka wanakamati wa mbio za Mwenge wa Uhuru 2019 kuendelea kujifunza kwa kuwa wamefanya kazi kubwa mpaka Mwenge wa Uhuru ukapita salama bila ya kuacha majeraha kwa watumishi.

Huku akibainisha kuwa kufanya tathimini ni kutathimini majukumu ambayo tulipewa na  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt.  John Pombe Joseph Magufuli ambapo balada yakuja yeye anatuma Mwenge wa Uhuru kupita katika kila Halmashauri kukaguwa kama wale waliopewa majukumu wanawajibika ipasavyo.

Mkuu wa Wilaya hiyo ametumia kikao hicho kumpongeza Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo  kwa kupeleka 3.6 milioni kulipa deni la ujezi wa Zahanati ya Ushora.

Akitoa taarifa ya matokeo ya Mwenge wa Uhuru 2019, Mratibu wa Mwenge wa Uhuru Wilayani  Iramba, Romwald Mwendi amesema Iramba imeshika nafasi ya kwanza kimkoa katika uraghabishaji wa falsafa ya mbio za Mwenge wa Uhuru  kwa wananchi.

Mwendi amesema matokeo ya jumla kimkoa, Iramba imeshika nafasi ya sita wakati Wilaya ya Mkalama ikishika nafasi ya mwisho huku nafasi ya kwanza ikishikwa na Wilaya ya Itigi, nafasi ya pili Wilaya ya Manyoni, nafasi ya tatu Singida  Vijijni , nafasi ya nne Wilaya ya Ikungi  wakati nafasi ya tano ikishikwa na Singida Manispaa.

Hata hivyo amebainisha nafasi iliyoshika kitaifa ambapo  Iramba imekuwa ya 174 wakati Wilaya ya Mkalama imekuwa ya  184 huku Wilaya ya Itigi ikishika nafasi 93.

 

Akichangia katika tathimini hiyo Afisa wa kuzuwia  na kupambana na rushwa (TAKUKURU), Benjamini Masyaga amewakumbusha wanakamati wote wa Mwenge wa Uhuru 2019  kuwa wanapopewa majukumu wanapaswa kujiongeza na kuhakisha wanakuwa na mawasiliano yakutosha.

 

Kwa upande wake Mkuu wa Magereza Wilayani humo, Mwakijungu ameshauri taarifa ya fedha kutaja malengo ya kila kijiji au kata yaliotakiwa kufikiwa huku akiwataka wenyeviti wakamati zote kuwepo kikao kijacho ili wajadili kwa pamoja.

Mwenge wa Uhuru 2019 Wilayani Iramba ulikimbizwa  kilometa 142.5 hadi eneo la makabidhiano Wilayani Igunga , ulipitia  katika Tarafa 3 , kata 7 na vijiji 14 huku ukipitia miradi 4 na shughuli sita ambapo miradi yote na shughulizi zote zilikuwa najumla ya garama ya 1.1 bilion.

Mbio za Mwenge wa Uhuru zilifikia kilele Oktoba 14, 2019 siku ya kumbukumbu ya Baba wa Taifa Hayati Mwl. Julius Kambarage Nyerere  na Wiki ya Vijana zilizofanyika uwanja wa Ilulu Mjini Lindi.                                                                        

Baadhi ya wajumbe wa kamati za Mwenge wa Uhuru 2019 wakifuatilia tathimini ya Mwenge ukumbi mkubwa wa Halmashuri ya wilaya ya Iramba. Picha na Hemedi Munga

Tangazo

  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI June 05, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • DC MWENDA ATEMBELEA MRADI WA UJENZI WA SHULE MPYA YA SEKONDARI YA AMALI KITUKUTU

    May 08, 2025
  • KAMATI YA FEDHA, UONGOZI NA MIPANGO YA HALMASHAURI YA WILAYA YA IRAMBA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO

    May 06, 2025
  • DC MWENDA ATOA WITO KWA WALIMU WA SHULE ZA MSINGI KUIMARISHA UFUNDISHAJI KWA MADARASA YA MITIHANI

    May 06, 2025
  • JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI WILAYANI IRAMBA LATOA ELIMU YA KINGA DHIDI MAJANGA YA MOTO KWA MADIWANI NA WANANCHI

    May 02, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.