• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Comments |
Iramba District Council
Iramba District Council

The United Republic of Tanzania Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Iramba District Council

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Emmanuel Luhahula amepiga marufuku mikusanyiko ya mikutano ya kisiasa, warsha, makongamano, semina na mafunzo Wilayani Iramba.

Posted on: March 18th, 2020

Hemedi Munga, Irambadc

tehama@irambadc.go.tz

Iramba. Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Emmanuel Luhahula amepiga marufuku mikusanyiko yote isiyo ya lazima ikiwa ni pamoja na mikutano ya kisiasa, warsha, makongamano, semina na  mafunzo wilayani Iramba.

                                     

Luhahula  ametoa katazo hilo  leo Jumatano Machi 18, 2020 wakati akiongea na wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama pamoja na viongozi wadini mbalimbali katika ukumbi wa Mkuu wa Wilaya mjini hapa.

Akiongea katika kikao hicho, Mkuu wa Wilaya amepiga marufuku vilabu vyote vinavyouza pombe za kienyeji, mabanda yote yanayoonesha video, michezo yote ya pool table na ile inayokusanya watu zaidi ya watano.

Amesema kuwa wagonjwa waliolazwa hospitali wataruhusiwa  kuonwa na kuhudumiwa na ndugu mmoja tu.

Katika kujilinda na ugonjwa wa virusi vya Corona Wilayani Iramba, Taasisi zote za umma na binafsi zichukue tahadhari ambayo imeelekezwa na Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Ummy Mwalimu.

“ Ninaelekeza Taasisi zote, maeneo yote ya biashara na maeneo yatakayokuwa na ulazima wa kusababisha mikusanyiko ikiwa ni pamoja na migahawa, hotel, maduka daladala na vyombo vyote vya usafiri kuwa na utaratibu wa kuhakikisha wateja wao wananawa mikono kwa maji yanayotiririka huku wakitumia sabuni,” amesisitiza Mkuu wa Wilaya

Naye Mkuu wa Magereza   Wilayani humo, SSP. Frank Mwakijungu amewaomba viongozi wa dini kuwafikishia taarifa wananchi kuwa hawaruhusiwi kuja Magereza kwa lengo la kuwatembelea ndugu zao.

Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba, Hussein Sepoko amewataka wananchi kufahamu dalili za ugonjwa wa  Covid-19 kuwa ni homa na mafua makali, kuumwa na kichwa, mwili kuchoka, kikohozi, kubanwa na mbavu, maumivu ya misuli, vidonda vya koo na kupumua kwa shida.

Sepoko amewataka wananchi hao kujikinga na maambukizi ya ugonjwa huo kwa kuzingatia kanuni za Afya na usafi ikiwa ni pamoja na kukaa mbali na mtu mwenye dalili za mafua na historia ya kusafiri katika maeneo yaliokumbwa na mlipuko wa ugonjwa huo.

Halikadhalika, kufunika mdomo na pua wakati wa kukohoa kwa kitambaa safi au nguo ulioivaa sehemu za mikono, kuepuka kugusana na mgonjwa mwenye dalili za magonjwa ya njia ya hewa na kuzingatia usafi binafsi ikiwemo kunawa mikono kwa maji tiririka na sabuni.

Pia, kuwahi kwenye vituo vya kutolea huduma za Afya endapo utakua na dalili zilizoainishwa na kutoa taarifa kwenye kituo cha kutolea huduma za Afya karibu uonapo mtu mwenye dalili za ugonjwa huo.

Halmashauri ya Wilaya ya Iramba imetenga jengo la macho liliopo  hospitali ya Wilaya na kituo cha Afya Kinampanda kwa ajili ya mgonjwa yoyote atakaye kuwa na dalili za viruri vya Covid-19.

MWISHO

Announcements

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU January 02, 2026
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI June 05, 2025
  • View All

Latest News

  • MAONESHO YA MATUMIZI YA PEMBEJEO ZA KILIMO (MBEGU, MBOLEA NA VIUATILIFU) HALMASHAURI YA WILAYA YA IRAMBA DISEMBA 29-30, 2025

    December 28, 2025
  • HERI YA SIKUKUU YA KRISMASI NA MWAKA MPYA 2026

    December 25, 2025
  • DC MWENDA AWATAKA WALIMU IRAMBA KUONGEZA UBUNIFU NA BIDII KUINUA UFAULU

    December 09, 2025
  • HERI YA MIAKA 64 YA UHURU WA TANZANIA BARA

    December 09, 2025
  • View All

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
More Videos

Quick Links

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Related Links

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    KIOMBOI, IRAMBA

    Postal Address: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Telephone: 026 - 2532253

    Mobile: 026 - 2533001

    Email: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.