• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Comments |
Iramba District Council
Iramba District Council

The United Republic of Tanzania Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Iramba District Council

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Emmanuel Luhahula amewaagiza Maafisa Tarafa na Maafisa Elimu Kata kuwakamata wazazi ambao hawajapeleka watoto shule.

Posted on: March 13th, 2020

Hemedi Munga, Irambadc

tehama@irambadc.go.tz

Iramba. Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Emmanuel Luhahula amewaagiza Maafisa Tarafa na Maafisa Elimu Kata kuwakamata wazazi ambao hawajapeleka watoto shule.

Agizo hilo amelitoa leo Ijumaa Machi 13, 2020 wakati akiongea katika kikao cha Baraza la Madiwani Ukumbi Mdogo wa Halmashauri hiyo mjini hapa.

“ Kamata wazazi ambao hawataki kupeleka watoto wao shule, tunataka Iramba yetu isonge mbele na haiwezi kusonga mbele kama watoto wetu hawapati elimu,” amesisitiza Luhahula

 

Pia amewataka Madiwani hao kuendelea kuhamasisha wananchi kutoka maeneo ya mabonde huku akiwapongeza kwa namna ambavyo wanavyosimamia miradi ya maendeleo.

“ Niwaombe tuendelee kuonesha uadilifu katika kusimamia miradi ya maendeleo na kukifanya kituo cha Afya Shelui kuwa kituo bora,” amesisitiza Luhahula

Halikadhalika amewataka Madiwani hao kuhamasisha kulima mazao yanayokabiliana na hali ya mvua inayoendelea kunyesha.

Akiongea katika kikao hicho Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo, Simion Tyosela amemuhakikishia Diwani wa Kata ya Shelui, Kinota Hamisi kuwa Halmashauri hiyo itakuwa pamoja katika ujenzi wa kituo cha Afya Shelui.

Tyosela amewataka Madiwani hao kuendesha kampeni ya kupinga mimba na utoro  kwa wanafunzi waliopo katika maeneo yao.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo, Linno Mwageni amewashukuru Madiwani hao kwa ushirikiano wao katika kujadili mambo mbalimbali ikiwemo ukusanyaji wa mapato kwa mustakabali wa maendeleo ya Wilaya ya Iramba.

Naye kaimu Afisa Ardhi na Maliasili wa Halmashauri hiyo, Lugano Sanga amewaomba Madiwani wa Baraza hilo kufahamu kuwa wataalamu wanapokwenda kupima mipaka ya maeneo mbalimbali hawampendelei yoyote bali wanafuata ramani.

MWISHO

kaimu Afisa Ardhi na Maliasili wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba, Lugano Sanga akifafanua mambo yanayohusu ardhi na mipaka yake wakati wa Baraza la Madiwani. Picha na Hemedi Munga


Announcements

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU January 02, 2026
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI June 05, 2025
  • View All

Latest News

  • MAONESHO YA MATUMIZI YA PEMBEJEO ZA KILIMO (MBEGU, MBOLEA NA VIUATILIFU) HALMASHAURI YA WILAYA YA IRAMBA DISEMBA 29-30, 2025

    December 28, 2025
  • HERI YA SIKUKUU YA KRISMASI NA MWAKA MPYA 2026

    December 25, 2025
  • DC MWENDA AWATAKA WALIMU IRAMBA KUONGEZA UBUNIFU NA BIDII KUINUA UFAULU

    December 09, 2025
  • HERI YA MIAKA 64 YA UHURU WA TANZANIA BARA

    December 09, 2025
  • View All

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
More Videos

Quick Links

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Related Links

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    KIOMBOI, IRAMBA

    Postal Address: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Telephone: 026 - 2532253

    Mobile: 026 - 2533001

    Email: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.