• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Mkuu wa Wilaya ya Iramba Emmanuel Luhahula amewaomba viongozi wa dini kuendelea kuelimisha jamii kujikinga na kuchukua tahadhari ya maambukizi ya homa kali ya mapafu inayosababishwa na virusi vya corona.

Posted on: April 24th, 2020

Hemedi Munga, Irambadc

tehama@irambadc.go.tz

Iramba. Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Emmanuel Luhahula amewaomba viongozi wa madhehebu ya dini mbalimbali kutengeneza vifaa vya kunawia vinavyokanyagwa kwa mguu, ambacho ukikanyaga kwa mguu mara moja kinatoa sabuni na ukikanyaga mara nyingine kinatoa maji.

Maombi hayo yametolewa leo Ijumaa Aprili 24, 2020 na Mkuu wa Wilaya wakati akiongea na Viongozi wa Dini wa wilaya ya Iramba Mkoani Singida.

“Sisi na nyinyi ni viyoo vya jamii, hivyo niwaombe Watumishi wa Mungu kutengeneza hivi vifaa kwa kuwa mnamikusanyiko mikubwa,” amesema Luhahula

Pia, amewaomba Viongozi hao kupunguza muda wa ibada na kutoa nafasi kwa waumini wachache ili kuepukana na maambukizi ya homa kali ya mapafu inayosababishwa na virusi vya corona.

Halikadhalika, amewakumbusha Viongozi hao kuwa madrasa na Sunday school zisiwepo kama alivyoelekeza Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa  Tanzania, Kassim Majaliwa.

Akiongea katika kikao hicho Mganga Mkuu wa Wilaya hiyo, Daktari Hussein Sepoko amesema kuwa wameandaa sehemu ya  jengo lililopo Hospitali ya Wilaya kwa wale wote watakao hisiwa kuwa na maradhi hayo na Kinampanda kwa wale watakaobainika kuwa na maradhi hayo kwa ajili ya kupatiwa matibabu.

Sepoko amesema kwa upande wa Doromoni kwenye Ziwa Kitangiri ambapo uvuvi wa samaki unaendelea kume kuwa na daftari la kuwasajili wote wanaoingia katika eneo hilo huku akiwataka Watendaji wa Kata na Vijiji kutoa taarifa ya mtu yoyote mwenye dalili ya homa kali ya mapafu inayosababishwa na virusi vya corona.

Pia, amesema tayari wameanza kuwapima joto abiria wote wanaoingia katika wilaya ya Iramba kwa kuweka kiziwizi eneo la Maluga.

Sepoko amesema wamekuwa wakiongeza uelewa na kutoa elimu kwa jamii kupitia vyombo mbalimbali vya habari ikiwemo Standard FM, Iramba Website (www.irambadc.go.tz) na mitandao ya kijamii ya facebook (Irambadc), Instagram (Irambadckiomboi) na Twitter (Irambadc) ya Wilaya ya Iramba.

Katika kuhakikisha Wilaya inadhibiti maambukizi ya homa kali ya mapafu inayosababishwa na virusi vya corona, Kamanda Mkuu wa Wilaya hiyo, P.C. Lusesa amewaomba Viongozi hao wa kiroho kuwahubiria bodaboda kuacha kubeba mshikaki.

“Sheikh Omari! ukizungumza pale Msikitini kuwa ni jambo lisilofaa, akalielewa kwa mtazamo wa kiroho anaweza asilifanye akitoka pale Msikitini,” amesema Lusesa na kuongeza

“kwa hiyo tuwaambie bodaboda hao kwa upande wa kiroho wanaweza kuelewa.”

Lusesa amewaomba Viongozi hao kuwaelimsha wananchi wao huku akiwataka kutoa taarifa kwa timu ya kufuatilia maambukizi ya virusi hivyo (Rapid Response Team).

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Usalama Barabarani, Alhaji Omari amesema kuwa tayari wametekeleza maagizo ya serikali kwa kusali huku wakiachiana nafasi kati ya mtu mmoja na mwingine na kwa muda mfupi.

Katika hatua nyingine, Hakimu Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya hiyo, Makwaya Charles amekiomba kikao hicho  kujifunza kufanya tathimini kuhusu ugonjwa wa COVID-19.

“Tunapo kuja kwenye kikao chapili tunafanya tathimini ili kuwa na mbinu na mienendo ya kukabiliana na ugonjwa huu kulingana na wakati,” amesema Hakimu Charles

Kwa kuwa Viongozi wa Dini wanapata nafasi ya kukutana na watu, Hakimu Charles amewaomba viongozi hao kupunguza safari na mienendo ya familia kutoka kwenda kwenye mahitaji.

“Niwaombe Viongozi wa Dini kwa sababu mnapata nafasi ya kukutana na watu wenye familia, kuzielekeza familia hizo kupunguza idadi ya watu wanao safiri au kutoka kwenda kwenye mahitaji,” amesema

Pia, amewaomba Viongozi hao kuzielekeza familia kupunguza msongamano wa kutuma watoto sokoni, hivyo msongamano utapungua sokoni na namna ya kujikinga itakua nzuri.

Halikadhalika amewaomba kuwasisitiza wazazi kuwa makini na watoto wao ili kuwalinda na mimba za mapema kwa wanafunzi.

“Niwaombe Viongozi wa Kiroho kuendelea kuwasisitiza wazazi kuwa makini maana wakisahau jukumu hilo, ni kweli baada ya ugonjwa huu kuisha na shule kufunguliwa huenda tukawa na wazazi na sio wanafunzi tena,” amesisitiza Hakimu Charlrs

Pia, amewaomba Viongozi hao kuendelea kuwaelimisha watu kuwa karibu na vyombo vya habari kwa sababu vyombo hivyo vinamatangazo ya kila aina ya namna ya ugonjwa huu unavyosambaa duniani, hivyo itasaidia kama familia kujikinga na ugonjwa huo.

Naye Mchungaji Robert Kijanga wa Kanisa la Evangelist Assembies of God, ameishauri jamii kukaa katika hali ya upweke kati ya ndugu, jamaa na marafiki huku akiwataka kufahamu kuwa wamenunua kifaa cha kupima joto kwa kila muumini atakaye kuwa anaingia kanisani ili kukabiliana na maambukizi ya homa kali ya mapafu inayosababishwa na virusi vya  corona.

Kikao cha Viongozi wa madhehebu ya Dini mbalimbali kimefanyika leo ikiwa ni siku moja tu, Mkuu wa Wilaya alipokutana na timu ya karantini kwa ajili ya kuwatia moyo katika kupambana na kuchukua tahadhari ya maambukizi ya homa kali ya mapafu inayosababishwa na virusi vya corona.

MWISHO

Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba, Daktari Hussein Sepoko akitoa taarifa ya mikakati waliojiwekea kupambana na maambukizi ya homa kali ya mapafu inayosababishwa na virusi vya corona. Picha na Hemedi Munga

Kamanda Mkuu wa Wilaya ya Iramba, P.C. Lusesa ameendelea kupiga marufuku bodaboda kubeba mshikaki ili kuepukana na maambukizi ya homa kali ya mapafu inayosababishwa na virusi vya corona. Picha na Hemedi Munga

Hakimu Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya ya Iramba, Makwaya Charles akiwaomba Viongozi wa Dini kuendelea kuwasisitiza wazazi kuwa makini na wanafunzi katika kipindi hichi waliopo nyumbani. Picha na Hemedi Munga

Viongozi wa madhehebu ya Dini mbalimbali wakisikiliza taarifa ya namna ya kuchukua tahadhari ya kupambana na maambukizi ya homa kali inayosababishwa na virusi vya corona. Picha na Hemedi Munga


Tangazo

  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI June 05, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • DC MWENDA ATEMBELEA MRADI WA UJENZI WA SHULE MPYA YA SEKONDARI YA AMALI KITUKUTU

    May 08, 2025
  • KAMATI YA FEDHA, UONGOZI NA MIPANGO YA HALMASHAURI YA WILAYA YA IRAMBA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO

    May 06, 2025
  • DC MWENDA ATOA WITO KWA WALIMU WA SHULE ZA MSINGI KUIMARISHA UFUNDISHAJI KWA MADARASA YA MITIHANI

    May 06, 2025
  • JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI WILAYANI IRAMBA LATOA ELIMU YA KINGA DHIDI MAJANGA YA MOTO KWA MADIWANI NA WANANCHI

    May 02, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.