• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Emmanuel Luhahula, amewashukuru wadau wote kutoa Tsh 14.6milioni kuchangia upatikanaji wa vifaa vya kujikinga na maambukizi ya homa kali ya mapafu inayosababishwa na virusi vya corona.

Posted on: June 11th, 2020

Hemedi Munga, Irambadc

tehama@irambadc.go.tz

Iramba. Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Emmanuel Luhahula amewashukuru Wadau wote kwa kuchangia takriban Tsh 14.6milioni kwa ajili ya kununua vifaa vya kuchukua tahadhari ya maambukizi ya homa kali inayosababishwa na virusi vya corona Wilayani Iramba.

Shukrani hizo amezitoa leo Juni 10, 2020 wakati alipokutana na baadhi ya Wadau katika viwanja vya Mkuu wa Wilaya hiyo mjini hapa.

“Niwashukuru Wadau wote kwa kuitikia wito, hivyo mmeonesha namna gani wananchi wa Iramba mnavyojali, ninawaomba wakazi na wasiowakazi wa Iramba kukumbuka kuwa Iramba ni yakwenu hivyo nilazima tuwekeze,” amesema Luhahula na kuongeza

“Ninawaomba wakazi wote wa Iramba na wale wasio wakazi wa Iramba ambao wako tayari kuwekeza wakaribie eneo la Salala kuna hekari 113 za kujenga matawi ya vyuo vikuu.”

Eneo la Salala lililopo njia kuu ya kuelekea Misigiri barabara kuu itokayo Singida mjini kuelekea jijini Mwanza lipo wazi kwa ajili ya mpango mahususi wa kuufanya mji wa Iramba kuwa Mji wa kisasa maana maeneo hayo tutaweka vituo vya Afya, Sheli na shule huku akiwataka wale wenye ndugu nje za nchi kuwaambia ndugu zao kuja kuwekeza Iramba.

Halikadhalika, amemuagiza Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo, Linno Mwageni kuhakikisha kitanda cha kujifungulia kilichototewa na ndugu Amoni aliyewakilishwa na ndugu yake, Winjuka kinapelekwa Zahanati ya Misigiri ili kukidhi utashi wa mfadhili.

Akiongea baada ya kukabidhiwa vifaa vya kuchukua tahadhari ya maambukizi ya homa kali ya mapafu inayosababishwa na virusi vya corona, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo, Linno Mwageni amewashukuru Wananchi kwa kuwa na muamko wa kuchangia kuiunga mkono Serikali inayoongonzwa na Rais wetu, Dkt John Magufuli.

Aidha amempongeza sana ndugu Winjuka kwa kuwakumbuka wakinamama kutoa kitanda ambacho watatumia wakati wa kujifungua.

“Nikushukuru sana dada Winjuka kwa kuwakumbuka wakinamama wanavyopata tabu maana ukimlinda mama tayari unakua umeilinda jamii,” amesema Mwageni

Kwa upande wake mmoja wa Wadau hao, Ndugu Winjuka akitoa shukrani kwa niaba ya Wadau wote amesema wanaishukuru Serikali kwa kukubali wao kuwa sehemu ya kuunga mkono juhudi za Mhe, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Magufuli.

Winjuka amesema kwa niaba ya ndugu yake aliyopo nje ya Tanzania wameweza kuchangia takriban Tsh 2.6milioni ambazo zimeweza kununua kitanda cha kujifungulia (delivery bed), PPE na vitakasa mikono (sanitizer).

MWISHO

Ndugu Winjuka akimkabidhi Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Emmanuel Luhahula baadhi ya vifaa alivyochangia kuunga mkono juhudi za Mhe, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Magufuli dhidi ya mapambano ya maambukizi ya homa kali ya mapafu inayosababishwa na virusi vya corona. Picha na Hemedi Munga

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba, Linno Mwageni akishika kitanda cha kujifungulia kilichotolewa na ndugu Winjuka kwa ajili ya Zahanati ya Misigiri ili kuwawezesha akina mama kujifungua kwa usalama. Picha na Hemedi Munga

Afisa Elimu kata ya Ulemo na Mratibu wa andiko lililosababisha kupatikana kwa vifaa hivi wakwanza kushoto, Nickson Mmanyi akishirikiana na Ndugu Winjuka kumkabidhi Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Emmanuel Luhahula kitanda na kipima joto (thermo scanner) kwa ajili yakusaidia huduma za afya na mapambano ya kuchukua tahadhari ya maambukizi ya homa kali ya mapafu inayosababishwa na virusi vya corona. Picha na Hemedi Munga

Katibu Tawala wa Wilaya ya Iramba, Pius Songoma akikagua vifaa vilivyotolewa na Mdau Winjuka. Picha na Hemedi Munga


Tangazo

  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI June 05, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • DC MWENDA ATEMBELEA MRADI WA UJENZI WA SHULE MPYA YA SEKONDARI YA AMALI KITUKUTU

    May 08, 2025
  • KAMATI YA FEDHA, UONGOZI NA MIPANGO YA HALMASHAURI YA WILAYA YA IRAMBA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO

    May 06, 2025
  • DC MWENDA ATOA WITO KWA WALIMU WA SHULE ZA MSINGI KUIMARISHA UFUNDISHAJI KWA MADARASA YA MITIHANI

    May 06, 2025
  • JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI WILAYANI IRAMBA LATOA ELIMU YA KINGA DHIDI MAJANGA YA MOTO KWA MADIWANI NA WANANCHI

    May 02, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.