• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Emmanuel Luhahula amezindua mfumo wa Stakabadhi Ghalani kwa mazao ya Choroko, dengu, mbaazi, soya na ufuta Wilayani Iramba.

Posted on: April 29th, 2020

Hemedi Munga, Irambadc

tehama@irambadc.go.tz

Iramba. Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Emmanuel Luhahula amewaagiza viongozi wa AMCOS kuwa waadilifu na kutoa elimu kwa wakulima wa mazao ya choroko, dengu, mbaazi, soya na ufuta kuhusu mfumo wa stakabadhi ghalani Wilayani Iramba.

Luhahula ametoa maagizo hayo kwa AMCOS leo Jumatano Aprili 29, 2020 wakati akizindua mfumo wa stakabadhi ghalani Wilayani Iramba.

Amewataka viongozi hao kutochezea mizani ya kupimia mazao hayo na kuhakikisha wanakua waadilifu katika kutekeleza mfumo huu.

“Niwaombe viongozi wote wa ngazi ya Halmashauri na wale mnaosimamia Ushirika kuwa makini ili tusiwapoteze Wakulima na matokeo yake wakawa wakiitukana Serikali,” amesema Luhahula

Halikadhalika, amewataka viongozi hao kuhakikisha wanasimamia Ushirika vizuri ili Halmashauri isipoteze mapato yake.

Mfumo wa Stakabadhi Ghalani kwa mazao ya dengu, choroko na mengineo yanayotokana na maagizo ya Serikali kuhusu mfumo wa ununuzi wa mazao hayo kwa Mikoa inayolima mazao hayo kuanzia mwaka 2020.

Akisoma tangazo kwa umma lililotangazwa na gazeti la Habari Leo la Februari 20, 2020, Mrajisi Msaidizi Mkoa wa Singida, Thomasi Nyamba amesema kuwa Serikali inataka mazao yanayozalishwa na Mkulima kuuzwa kupitia Mfumo wa Ushirika kwa lengo la kuhakikisha mazao ya jamii ya mikunde na mbegu kama vile choroko, dengu, mbaazi, soya na ufuta yanazalishwa na kuuzwa kwa tija na ubora unaotakiwa ili kumuwezesha Mkulima wa mazao hayo kupata soko la uhakika na lenye bei ya ushindani.

Kufuatia tangazo hilo, Nyamba ameufahamisha umma na wadau wote wa mazao hayo nchini  kwamba kuanzia mwaka 2020 yatazalishwa na kuuzwa kupitia Mfumo wa Ushirika.

Pia, kutokana na mamlaka ya Wizara ya Kilimo na kwa kuzingatia sheria ya Vyama vya Ushirika Na. 6 ya mwaka 2013 imetoa maelekezo 17 Wakulima na Wanunuzi wa mazao hayo kuyazingatia.

 Akichangia mada katika kikao cha uzinduzi wa Mfumo wa Stakabadhi Ghalani, Katibu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) wa Wilaya hiyo, Ibrahimu Mjanaheri amemuagiza Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo Linno Mwageni, kutengeneza programu maalumu ambayo haitachukua wiki moja kuanzia sasa itakayomuwezesha Afisa Ushirika kupita kwa viongozi wa  vijiji na vitongoji ambao watafikisha elimu ya mfumo wa Stakabadhi Ghalani  kwa wananchi wao.

“Halmashauri imuwezeshe Afisa Ushirika Wilaya kwenda kukutana na hao watu, maana mpango huu utatupa matokeo makubwa sana,” ameagiza Mjanaheri

“Ninaomba tuwekeze Ndago, Shelui na Kidaru ambapo tunaweza kupata mazao mengi maana  tutapata fedha nyingi sana kwenye kilimo,” amesema

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo, Simion Tyosela amewataka viongozi hao wa AMCOS  kuanza Ushirika  mpya.

“Tuhakikishe tunauboresha Ushirika ambao utaleta tija katika maisha yetu, Ushirika ni Maisha,” amesema Tyosela

 

“Embu tuupeleke Ushirika huu, maana tukifanya vizuri mtaona namna ambavyo watu watamiminika, hivyo Ushirika kuwa na tija na kufanya maendeleo makubwa ikiwemo kuongeza mapato ya Halmashauri yetu,” ameongeza  Tyosela

Katika kuhakikisha viongozi wa AMCOS wanaelewa malengo ya Serikali kwa Wakulima wa mazao hayo mada mbalimbali zimewasilishwa.

Naye Mkuu wa Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika wa Wilaya hiyo, Marietha Kasongo amesema kuwa mfumo utakua na vituo vya kukusanyia mazao ambavyo vitakua katika AMCOS za Umoja-Mtoa, Jembe nimali-Ndago, Nsimbo AMCOS-Urughu, Malendi AMCOS-Mgongo, Lunsanga AMCOS-Mtekente, Ngusamu AMCOS-Ntwike na Maluga AMCOS-Maluga.

Amefafanua kuwa vituo vya masoko vinatarajiwa kuwa viwili ambapo ni Ghala la Nselembwe kata ya Shelui, Mtoa, Mgongo na Ntwike huku kijiji cha nguvumali kikihudumia kata ya Mukulu, Mtekente, Mbelekese, Kaselya, Maluga, Ulemo na Kyengege.

Kasongo amewataka Wakulima kufahamu kuwa wanatakiwa kuuzia mazao yao katika vituo vya ununuzi wa mazao.

Amesema Wafanya biashara watatakiwa kuomba kibali cha ununuzi wa mazao kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ambapo Mkurugenzi Mtendaji atampatia mnunuzi kituo cha kwenda kununua mazao au zao analolitaka.

Pia, Kasongo amewaonya wakulima wa mazao hayo kuwa hawaruhusiwi kuuza mazao yakiwa shambani au nyumbani, hivyo faini kubwa itatolewa kwa mnunuzi na Mkulima anayeuza mazao bila kutumia kituo maalumu.

MWISHO  

 Katibu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Iramba, Ibrahimu Mjanaheri amemuagiza Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo, Linno Mwageni kumuwezesha Afisa Ushirika wa Wilaya hiyo kwenda kutoa elimu ya mfumo wa stakabadhi ghalani kwa mazao ya choroko, dengu, mbaazi, soya na ufuta kwa wananchi vijijini. Picha na Hemedi Munga


Mkuu wa Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika wa Wilaya ya Iramba, Marietha Kasongo akiwaonya wakulima wa mazao ya choroko, dengu, mbaazi, soya na ufuta kuwa hawaruhusiwi kuuza mazao yakiwa shambani au nyumbani, hivyo faini kubwa itatolewa kwa mnunuzi na Mkulima anayeuza mazao bila kutumia kituo maalumu. Picha na Hemedi Munga

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba, Simion Tyosela akiwataka viongozi wa AMCOS   kuanza Ushirika  mpya utakaokua na tija na kuifanya Halmashauri hiyo ikusanye mapato yake. Picha na Hemedi Munga

                          

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • KIDATO CHA KWANZA KURIPOTI SHULE January 13, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • MAAFISA ELIMU KATA 136 MKOANI SINGIDA WAPATIWA MAFUNZO KUHUSU USIMAMIZI WA SHULE NA UJAZAJI TAKWIMU KATIKA MFUMO WA "SIS"

    March 24, 2025
  • DC MWENDA AWASISITIZA WALIPA KODI KUFANYA MAKADIRIO YA KODI KABLA YA MACHI 31, 2025

    March 20, 2025
  • DC MWENDA NA WAZIRI MWIGULU NCHEMBA WACHANGIA JUMLA YA MADAWATI 98 SHULE YA MSINGI MSANSAO ILIYOPO KATA YA MTEKENTE

    March 10, 2025
  • WALIMU WAKUU 108 WA SHULE ZA MSINGI NA MAAFISA ELIMU KATA 20 WILAYANI IRAMBA WAPEWA MAFUNZO ENDELEVU YA USIMAMIZI WA UFUNDISHAJI NA UJIFUNZAJI FANISI KUPITIA JUMUIYA ZA KUJIFUNZA ZA WALIMU WAKUU NA MAAFISA ELIMU KATA

    March 19, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.