• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Emmanuel Luhahula amezinduwa mradi wa maji Gereza la Ushora.Picha na Hemedi Munga

Posted on: January 3rd, 2020

Hemedi Munga, Irambadc

tehama@irambadc.go.tz

Iramba.Mkuu wa Wilaya ya Iramba Emmanuel Luhahula amezindua mradi wa maji Gereza la Ushora.

Luhahula amezindua mradi huo leo Ijumaa Januari 03, 2020 katika Gereza la Ushora lililopo Tarafa ya Ndago Wilayani Iramba.

Akiongea katika hafla hiyo, luhahula amempogeza Rais wa  wa Tanzania , Dtk. John Magufuli kwa kutoa Bilioni 1 na milioni mia tano kumi na nne kwa wilaya ya Iramba pekee kwa kipindi cha miaka mine kutekeleza miradi ya maji.

Huku akieleza mafanikio ya upatikanaji wa maji kufikia 53.6%   ukilinganisha na wakati anaignia madarakani upatikanaji wa maji ulikuwa asilimia 43%.

Akibainisha malengo ya serikali katika kutimiza  ilani ya Chama cha Mapinduzi (CCM)  kumtua mama ndoo kichwani kwa kuweka vituo vya kutolea maji  (DP) kila umbali wa mita 400.

Aidha amemuagiza Mkuu wa Magereza Mkoa wa Singda, Msekwa Omari kuhakikisha wanapanda miti kulinda uwoto wa asili wa vyanzo vya maji ushora.

Akimkaribisha mwekezaji Profesa Giuseppe kutoka Italia, mwakilishi wa wizara ya maji, Lidya Joseph amemshukuru mwekezaji huyo kwa kutatuwa tatizo la maji katika jamii ya watu wa Ushora.

Akiongea katika hafla hiyo profesa Giuseppe amesema kusherehekea kukamilika mradi huo ni kusherehekea maisha huku akiwataka kufahamu kuwa 90% ya mwili wa mwadamu umeumbwa na maji.

“ Tunatokea kwenye maji, kiumbe cha kwaza kugundulika ilikuwa ni bakteria kutoka kwenye maji na tunapojifunza sayari zilizoko karibu nasisi tunaangalia uwepo wa maji kuona uwezekano wa maisha” Alisisitiza Giuseppe

Mapema akisoma taarifa ya mradi wa maji Gereza la Ushora meneja wa maji RUWASA wilayani humo, Ezra Mwacha amesema mradi umegharimu 89.1 milioni, huku akifafanuwa kuwa 78.2 milioni zinatoka kwa wadau wa maendeleo “Rotary Club Rho” wa Italia na 10.8 milioni kutoka Magereza, Ofisi ya katibu Tawala Mkoa wa Singida na Halmashauri ya wilaya ya  Iramba.

Fedha hizo ziliwezesha kufanya utafiti wa maji ardhini na uchimbaji wa kisima kirefu cha mita 115 chenye uwezo wa kuzalisha wingi  wa maji wa lita 5,600 kwa saa.

Mwacha ameeleza miundombinu iliyojengwa kuwa ni ujenzi wa vituo 8 vya kuchotea maji (DP), ujenzi wa mnara wa mita sita, kununua na kuweka tanki la plastiki lenye ujazo wa lita 10,000, ujenzi wa fensi na jengo moja la mitambo ya kuendeshea pampu, kulaza, kuunganisha na kufikia mtandao wa mabomba wenye urefu wa mita 2,575.

Kufanikiwa kwa mradi huo kumefunguwa nafasi ya ketekeleza maagizo ya Rais wa Tanzania, Dtk. John  Magufuli ya kuwataka magereza kuzalisha chakula kwa wingi.

Naye Mkuu wa Magereza Mkoa wa Singida, Msekwa Omari ameeleza kuwa Gereza la Ushora ndio gereza linalotegemewa kwa chakula na  magereza yote Mkoa wa Singida.

“ Baada ya maji kupatikana nguvu kazi ya wafungwa itatumika katika shughuli za uzajishaji,” alisibitisha Omari

Huku akiahidi kuulinda mradi huo ili udumu kwa muda mrefu kuendelea kupata matunda yake.

Kwa upande wake katibu wa Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Iramba, Ibrahimu Mjanaheri amempogeza Profesa Giuseppe kwa kusogeza huduma ya maji ambayo ndio chanzo cha kuondoa magonjwa yanayoweza kusababishwa na ukosefu wa maji safi na salama.

“ Unapoleta maji mahala unaondoa magonjwa ambayo yanaonyemelewa na ukosefu wa maji,” alisema Mjanaheri

Kwa upande wake mnufaika wa maji yatokanayo na mradi huo Mwalimu Mkuu wa Shule ya Utemini, Mwanaisha Mfaume amesema mradi huo umewarahisishia kuyapata maji karibu na kuwafanya wawe safi na afya njema.

Mradi wa maji wa Gereza la kilimo na Mifugo Ushora uliibuliwa mwaka 2017 kupitia Mkuu wa Magereza Mkoa wa Singida kwa kuwasilisha kwa katibu Tawala wa Mkoa.

Mradi huo umeweza kutatua changamoto ya ukosefu wa huduma ya  maji katika eneo la Gereza la Ushora na shule ya Msingi Utemini.                                                                                                                                                                         

Mkurugenzi wa Mazingira Wizara ya Maji akimtaka Meneja wa RUWASA wilayani Iramba kuhakikisha mradi wa maji Ushora  unadumu na unaleta manufaa kwa jamii ya wanaushora, Kushoto kwake  ni Mkuu wa Wilaya ya Iramba Emmanuel Luhahula na kulia kwake ni Profesa Giuseppe kutoka Italia. Picha na Hemedi Munga                                                                                                                                                                                                                                                         

Mkuu wa Wilaya ya Iramba Emmanuel Luhahula akiwa na viongozi mbalimbali eneo la Gereza la Ushora Wilayani Iramba. Kushoto kwake ni Msekwa Omari Mkuu wa Magereza Mkoa wa Singida akifuatiwa na katibu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Iramba, Ibrahimu Mjanaheri na kulia kwa Mkuu wa Wilaya ni Mkurugenzi wa Mazingira Wizara ya maji Lidya Joseph akifuatiwa na Profesa Giuseppe kutoka Italia. Picha na Hemedi Munga

Tangazo

  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI June 05, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • DC MWENDA ATEMBELEA MRADI WA UJENZI WA SHULE MPYA YA SEKONDARI YA AMALI KITUKUTU

    May 08, 2025
  • KAMATI YA FEDHA, UONGOZI NA MIPANGO YA HALMASHAURI YA WILAYA YA IRAMBA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO

    May 06, 2025
  • DC MWENDA ATOA WITO KWA WALIMU WA SHULE ZA MSINGI KUIMARISHA UFUNDISHAJI KWA MADARASA YA MITIHANI

    May 06, 2025
  • JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI WILAYANI IRAMBA LATOA ELIMU YA KINGA DHIDI MAJANGA YA MOTO KWA MADIWANI NA WANANCHI

    May 02, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.