• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

MKUU WA WILAYA YA IRAMBA MHE.SULEMAN MWENDA AMEHADHIMISHO SIKU YA UKIMWI DUNIANI KATIKA KIJIJI CHA UJUNGU, LEO TAREHE 1 DISEMBA, 2021

Posted on: December 1st, 2021

Mkuu wa wilaya ya Iramba Mhe.suleiman Mwenda amehadhimisho siku ya ukimwi duniani katika kijiji cha ujungu, leo tarehe 1 Desemba, 2021 akiongea na Wananchi Mhe, Mwenda amewashukuru viongozi na wananchi wa Wilaya ya Iramba kwa kubeba jukumu la kuwa mwenyeji wa Maadhimisho haya ya Siku ya UKIMWI Duniani kwa Mwaka huu wa 2021 “nitoe shukrani za pekee kwa Viongozi, Wadau na wananchi wote wa Wilaya ya Iramba kwa kukubali kubeba jukumu la kuwa mwenyeji wa Maadhimisho haya ya Siku ya UKIMWI Duniani kwa Mwaka huu wa 2021, yanayofanyika Kiwilaya hapa Ujungu. Napenda pia kuwashukuru nyote kwa kunipa heshima ya kuwa Mgeni Rasmi katika maadhimisho haya. Ahsanteni sana.

Aidha, niwapongeze vikundi vyote kwa burudani mbalimbali na ushuhuda kutoka kwa watu wanaoishi na Virusi vya UKIMWI. Nimefarijika na yote niliyoyaona na kusikia.

Umoja wa Mataifa uliamua siku ya tarehe 01 Desemba ya kila mwaka kuwa siku ya Kimataifa ya Maadhimisho ya UKIMWI Duniani. Lengo la Maadhimisho haya ni kupima na kutathmini kiasi cha utekelezaji wa malengo na maazimio mbalimbali kuhusu Mapambano dhidi ya VVU na UKIMWI. Aidha, siku hii hutumika kwa malengo MATATU yafuatayo:-

Kuhamasisha  na  kuelimisha  jamii  juu  ya  namna  ya  kujikinga  na maambukizi mapya ya VVU,

Matumizi sahihi ya dawa za ARV kwa watu wanaoishi na VVU pamoja na

Kupinga unyanyapaa na ubaguzi.

Kauli mbiu ya Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani kwa mwaka huu wa 2021 ni “ZINGATIA USAWA. TOKOMEZA UKIMWI.TOKOMEZA MAGONJWA YA MLIPUKO” Kaulimbiu hii inasisitiza ushiriki na ushirikishaji wa Kimataifa, Kitaifa na Jamii katika shughuli za udhibiti wa VVU na UKIMWI kuanzia kwenye upangaji mikakati, upatikanaji wa rasilimali na utoaji wa huduma za VVU na UKIMWI kwa makundi yote ya wanaume, wanawake, vijana walio katika umri wa balehe wenye umri wa miaka 15-24, akinamama wajawazito na wanaonyonyesha pamoja na watoto wao katika kuzingatia upimaji wa afya zao.

Wakati Dunia ikiadhimisha Siku hii ya UKIMWI ambayo leo ni Miaka 42 iliyopita tangu ugundulike rasmi duniani, kila mmoja wetu akumbuke kwamba VVU na UKIMWI bado upo, na achukue hatua za makusudi ya kupambana na janga hili, kwa kuwa hakuna dawa ya kuponya UKIMWI pia hakuna CHANJO. Hivyo kila moja wetu achukue tahadhari ili kupunguza maambukizi mapya  

Katika wilaya yetu maambukizi ya VVU na UKIMWI bado yapo, hii ni  kutokana na uwepo wa shughuli nyingi za mwingiliano wa kiuchumi kwa mfano uwepo wa machimbo ya madini, maeneo ya uvuvi, vituo vya magari makubwa n.k.Niwaombe viongozi wa kata zote kuweka Mikakati mahususi ya kudhibiti maambukizi mapya ya VVU.

Kushamiri wa maambukizi mapya ya Virusi vya UKIMWI miongoni mwa Wanaume, Wanawake na Vijana wenye umri kati ya miaka 15 – 49 ni mkubwa. Kwa mwaka 2021 yaani kuanzia (Januari – Oktoba) Waliopimwa ni watu 49,229 Wanaume 16,378 na wanawake 32,851 kati yao 814 waliogundulika kuwa na maambukizi ya VVU sawa na asilimia 1.6 wanaume walikuwa 300 sawa na asilimia 0.6   Na Wanawake walikuwa ni 514 sawa na asilimia 1.0.

Kwa  upande wa    vijana    kuanzia miaka 15-24 kwa kipindi cha Januari hadi Oktoba, 2021 waliopimwa 20,296 wanaume 7,349 na wanawake 12,947waliogudulika kuwa na maambukizi mapya VVU  ni 151 sawa na asilimia 0.7 kati yao wanaume  35  na wanawake  116. Katika suala zima la upimaji wa hiari, idadi kubwa ya wanaopima ni wanawake ukilinganisha na wanaume. Kama takwimu zinavyoonyesha hapo juu.

Kwenye Huduma ya Matunzo na Tiba, jumla ya watu wanaoishi na Virusi vya UKIMWI walioandikishwa hadi kufikia Oktoba 2021 ni 11,342 ambapo kati ya hawa waliopo kwenye dawa ni 5,338 na waliobaki wamehama na wengine ni watoro. Hali hii si ishara nzuri katika mapambano dhidi ya UKIMWI, kwa sababu hiyo, naomba sana wataalam wa afya waendelee kutoa elimu ya ufuasi mzuri wa dawa.

Kama sehemu ya Mapambano hayo WAVIU pia hupima wingi wa Virusi, kwa hiyo, hadi Oktoba, 2021 Jumla ya WAVIU 3,062  wamepata huduma ya kupima wingi wa Virus vya UKIMWI na kati yao 2,935  sawa na asilimia 96 wamepata ufubavu wa VVU. Hii ni ishara nzuri kwani inaonyesha  kuwa  afya  zao  zinaendelea  vizuri.  Niwasihi sana  WAVIU wasibweteke na kufubazwa kwa VVU na kuanza mienendo isiyofaa hivyo ni lazima tuendelee kufuata maelekezo ya wataalam ili kulinda afya zetu

Vijana ni kundi linalokabiliwa sana na changamoto ya maambukizi mapya ya VVU nchini. Takwimu za maambukizi mapya ya VVU zinaonesha kwamba asilimia 40 ya maambukizi hutokea kwa vijana na katika hao asilimia 80 ni vijana wa kike.

Kwa mujibu wa takwimu hizi, ni dhahiri kuwa kundi la vijana na hasa wa kike lipo kwenye hatari kubwa zaidi ya kupata maambukizi mapya. Uchambuzi wa kimazingira kuhusu takwimu hizi unaonesha kuwa sababu za vijana kuwa katika hatari ya maambukizi mapya ya VVU ni pamoja na:

  • Kuanza ngono katika umri mdogo.Hali hii husababisha mhusika kuwa na mahusiano yamapenzi na watu wengi hadi anapofikia utu uzima. Hivyo, kujiweka katika hatari ya kupata maambukizi ya VVU. Nawaasa vijana, msijihusishe na mapenzi katika umri mdogo. Ili vijana muweze kutimiza ndoto au malengo yenu katika Maisha; lazima kuwa na Subira
  • Vijana wadogo wa kike kuwa na mahusiano ya kingono na wanaume wenye umri mkubwa kwa kuvutika na vishawishi kama vile pesa na zawadi ndogo ndogo.
  • Ulevi wa kupindukia na matumizi ya dawa za kulevya hususan kuchangia sindano wakati wakujidunga huchochea vijana kuambukizwa VVU kirahisi; na
  • Unyanyasaji wa kijinsia na ukatili dhidi ya watoto unaombatana na matendo ya ubakaji, udhalilishaji na vipigo.

 

Hizo ni baadhi ya sababu au vichocheo vya kuongezeka kwa maambukizo mapya ya VVU miongoni mwa vijana. Aidha, natoa wito kwa vijana wajitambue na kuthamini maisha yao kwa kujikinga na maambukizi mapya ya VVU kwa kuwa ninyi ni nguvu kazi na Taifa linawategemea. Na wale wanaoishi na VVU waendelee kutumia dawa za ARV kwa ufuasi sahihi bila kuacha ili kufubaza VVU na kuimarisha afya zao.

Katika juhudi za Mapambano dhidi ya VVU na UKIMWI, Mkoa ulizindua Kampeni ya “FURAHA YANGU” mwaka 2018. Lengo la uzinduzi

wa kampeni hii ambayo kauli mbiu yake ilikuwa ni ‘PIMA, JITAMBUE, ISHI’ ni kuona wananchi wa Mkoa wa Singida wanatambua hali zao za maambukizi ya VVU, hususani wanaume na makundi mengine ambayo ni Wasichana walio katika umri wa balehe, Wanawake vijana wenye umri wa miaka 15-24, akinamama wajawazito na wanaonyonyesha pamoja na watoto wao.

Wilaya kwa kushirikiana na wadau mbalimbali waliopo ndani na nje ilifanya mapitio ya Mpango Mkakati wa UKIMWI wa mwaka 2015 hadi 2020. Lengo la mkakati huu ni kupunguza na kuondoa viashiria vinavyosababisha maambukizi ya VVU Maambukizi ya VVU.  

 

Pamoja na mafanikio makubwa tuliyoyapata, bado kuna mambo mengi yanayohitaji kufanyika ili tuweze kufikia adhima yetu ya kumaliza kabisa janga la UKIMWI. Hii ni pamoja na kuzuia maambukizi mapya sambamba na kuzuia vifo vinavyotokana na UKIMWI na hatimaye tuanze kuona gharama za kudhibiti VVU na UKIMWI nchini zikipungua.

 

Wilaya yetu imefanikiwa kufikia malengo ya 95 TATU (95:95:95) hasa katika 95 ya pili na ya tatu. Kwa kujikumbusha tu ni kwamba 

95% ya kwanza  inalenga kuhakikisha kuwa asilimia 95 ya WAVIU wanajua hali zao;

 95% ya Pili wanaojua hali zao wanaanza kutumia dawa za kufubaza makali ya VVU mapema na

 95% ya Tatu walioanza dawa za kufubaza VVU kinga zao za mwili zinaimarika.

Natoa wito kwa wadau wote katika mapambano dhidi ya VVU na UKIMWI, tuongeze jitihada sana katika kuhamasisha upimaji wa VVU ili tufikie lengo katika 95 ya kwanza. Vilevile, tuendelee kujitathmini katika maeneo yote matatu ili palipo na changamoto tuweze kurekebisha na kuimarisha na penye mafanikio tuongeze nguvu zaidi. Aidha mipango yetu ya baadaye ionyeshe wazi jinsi tutakavyofikia Tanzania isiyokuwa na maambukizi mapya UKIMWI ifikapo mwaka 2030.

 

Sote tunafahamu kwamba unyanyapaa umekuwa ni kikwazo kikubwa katika kutekeleza mipango tuliyojiwekea wenyewe katika kutokomeza UKIMWI. Serikali kwa upande wake, imeendelea kuchukua hatua mbalimbali ikiwa ni pamoja na kufanya kampeni za kuelimisha kuhusu madhara ya unyanyapaa na ubaguzi kupitia vyombo vya habari na majukwaa mbalimbali. Hata sasa kuna kampeni zinaendelea kupitia wasanii, mitandao ya kijamii pamoja na hotuba za viongozi. Huo ni mtizamo potofu na unahitaji kukomeshwa.

Nawasihi Watanzania wenzangu, tuache kabisa tabia za unyanyapaa na ubaguzi. Elimu iendelee kutolewa kwa njia mbalimbali kuanzia ngazi ya familia ili watu wajue ukweli kuhusu VVU/UKIMWI pamoja na kujua jinsi ya kuwahudumia watu wanaoishi na VVU ili kuondoa mtazamo hasi.

Aidha,Niwasihi Viongozi wa Dini, Wanasiasa na Viongozi wa Serikali katika ngazi zote, endeleeni kusemea na kukemea unyanyapaa na ubaguzi dhidi ya WAVIU na kuhimiza upendo na huruma miongoni mwao.

 

Katika kufikia mafanikio hayo niliyokwisha yataja, hatukuwa peke yetu. Wapo wadau mbalimbali ambao wamekuwa bega kwa bega na Serikali katika kuhakikisha tunashinda vita hivi dhidi ya VVU na UKIMWI. Hivyo basi, nitumie fursa hii kutoa shukrani za dhati kwao

Napenda kuhitimisha kwa kuwakumbusha kwamba UKIMWI bado ni Janga la Taifa na Kimataifa na la KIDUNIA, hivyo ni vyema kila mmoja kuwa na wajibu wa kuchukua tahadhari stahiki na kuendeleza mapambano dhidi ya Maambukizi ya Virusi vya UKIMWI. Sambamba na hilo niendelee kuwakumbusha wananchi kuchukua tahadhari dhidi ya UVIKO 19 na kwenda kupata chanjo dhidi ya UVIKO 19  katika vituo vya Afya

 Mwisho ninawashukuru tena kwa maandalizi mazuri na ushirikiano wenu mlionesha katika maadhimisho haya. Ninaomba Mungu aendelee kutulinda. “ZINGATIA USAWA. TOKOMEZA UKIMWI.TOKOMEZA MAGONJWA YA MLIPUKO”

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • KIDATO CHA KWANZA KURIPOTI SHULE January 13, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • MAAFISA ELIMU KATA 136 MKOANI SINGIDA WAPATIWA MAFUNZO KUHUSU USIMAMIZI WA SHULE NA UJAZAJI TAKWIMU KATIKA MFUMO WA "SIS"

    March 24, 2025
  • DC MWENDA AWASISITIZA WALIPA KODI KUFANYA MAKADIRIO YA KODI KABLA YA MACHI 31, 2025

    March 20, 2025
  • DC MWENDA NA WAZIRI MWIGULU NCHEMBA WACHANGIA JUMLA YA MADAWATI 98 SHULE YA MSINGI MSANSAO ILIYOPO KATA YA MTEKENTE

    March 10, 2025
  • WALIMU WAKUU 108 WA SHULE ZA MSINGI NA MAAFISA ELIMU KATA 20 WILAYANI IRAMBA WAPEWA MAFUNZO ENDELEVU YA USIMAMIZI WA UFUNDISHAJI NA UJIFUNZAJI FANISI KUPITIA JUMUIYA ZA KUJIFUNZA ZA WALIMU WAKUU NA MAAFISA ELIMU KATA

    March 19, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.