• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Mkuu wa wilaya ya Iramba mkoani Mhe. Emmanuel Luhahula akikabidhiwa miche ya miti 3000 na vitabu vya ziada na kiada 547 kutoka shirika la NDUGU foundation.

Posted on: January 9th, 2019

Mkuu wa wilaya ya Iramba mkoani Mhe. Emmanuel Luhahula akikabidhiwa miche ya miti 3000 ya aina mbalimbali kwa ajili ya kuboresha mazingira katika shule ya sekondari Kizaga na shule za msingi kutoka shirika la NDUGU Foundation.

Mkuu wa wilaya ya Iramba Mhe. Emmanuel Luhahula akikabidhiwa vitabu vya ziada na kiada 547 kwa ajili ya shule ya sekondari kizaga kutoka shirika la NDUGU Foundation.

Mkuu wa wilaya ya Iramba mkoani Singida Mhe. Emmanuel Luhahula, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Iramba na Viongozi mbalimbali wakiwa kwenye picha ya pamoja na wanafunzi wa shule ya sekondari Kizaga


SHIRIKA lisilo la Kiserikali linalojishughulisha na shughuli za kijamii, Ndugu Foundation lenye makao yake Makuu nchini Sweeden limetoa msaada ya vitabu vya ziada na kiada zaidi ya 3000 kwa ajili ya Shule ya Sekondari Kizaga Wilayani Iramba ,Mkoa wa Singida.

Kitengo cha mawasiliano wilayani Iramba  kimeshuhudia hafla fupi juzi iliyofanyika kwenye ukumbi shule ya Sekondari Kizaga ya kukabidhi vitabu 547 vya Sekondari kwa Mkuu wa Wilaya ya Iramba Mhe: Emmanuel Luhahula lengo likiwa kuwasaidia watoto wa shule hiyo kitaaluma na kuongeza ufaulu.

Akipokea msaada huo Mhe: Luhahula alimshukuru Mratibu Mkuu wa Shirika la Ndugu Foundation Winjuka Mkumbo ambaye ni mkazi wa kijiji cha Kizaga ambapo Mkuu huyo wa Wilaya alimsifu kwa kujali nyumbani alikozaliwa kwani ni watu wachache wenye moyo wa kusaidia wakiwa nje ya nchi kukumbuka nyumbani na kutoa msaada kama huu.

Pamoja na kutoa msaada wa vitabu pia shirika hilo limetoa msaada wa miche ya miti mbalimbali 3000 kwa ajili ya kumuunga mkono Makamu wa Rais Mhe: Samia suluhu Hassan kutunza na kuhifadhi mazingira nchini.

Pamoja na shukrani zake Mkuu huyo wa Wilaya alitoa wito kwa wazazi wote kuhakikisha watoto wote waliofaulu kwenda Sekondari wanaenda shule kwa tarehe iliyopangwa bila kisingizio chochote.

‘’ Natoa wito kwa wananchi wote , watendaji wa vijiji na kata wenyeviti wa vitongoji na vijiji kuhakisha ifikapo Januari 31 mwaka huu watoto wote waliofaulu kuingia kidato cha kwanza wawe wameripoti shuleni na ikifika Februari Mosi mwaka huu operesheni ya kuwakamata wazazi ambao hawajawapeleka watoto wao shule, kwa kipindi hiki watoto wanaweza kuripoti shule bila sare za shule wakati wazazi wakijiandaa kushona sare ’’alisisitiza Mhe Luhahula.

Hata hivyo aliwapongeza watendaji wa kata ya Ulemo kwa kutekeleza maagizo yaliyotolewa na Serikali kwa kuandikisha darasa la awali kwa asilimias 117 na darasa la kwanza asilimia 102.

Kwa upande wake Mratibu Mkuu wa Shirika la Ndugu Foundation Winjuka Mkumbo alisema Shirika hilo limeanza kazi ya kushughulikia jamii tangu mwaka 2002 ambapo shirika hilo linajishughulisha na Afya , Elimu, Mazingira na Ustawi wa jamii.

‘’ Mheshimiwa Mkuu wa Wilaya , leo hii Shirika la Ndugu Foundation linakabidhi vitabu vya ziada na kiada 547 kwa ajili ya shule hii na miche ya miti mbalimbali 3000 kwa ajili ya uhifadhi na utunzaji mazingira ambapo Shule sita za Msingi za kata ya ulemo na shule ya Sekondari Kizaga zitahusika na upandaji wa miti ili kuboresha mazingira ya kata yetu lakini ukijumlisha msaasda wa vitabu tangu tuanze tumeshasaidia zaidi ya vitabu 3000 vya ziada na kiada’’ alisema Mratibu Mkumbo

Mratibu huyo alisema toka shirika hilo lianze mwaka 2002 tayari limejenga nyumba ya mganga ya moja kwa mbili kwa ajili ya Zahanati ya Misigiri, limetoa vifaa tiba kwa ajili ya zahanati hiyo.

‘’ Pamoja na shughuli nyingine za kijamii pia tumesaidia chakula magunia 120 ya mahindi kwa ajili ya chakula kwa shule 10 za Msingi na 2 za Sekondari za Mukulu na Kizaga, lakini pia shirika letu linatoa Elimu ya Wajasiriamali , na utoaji Elimu ya Ukimwi kwa jamii na uhifadhi wa mazingira’’

 Shirika la Ndugu Foundation lilianzishwa na Amon Gyunda ambaye ni mzaliwa wa kijiji cha Kizaga Wilayani Iramba anayeishi Sweden na Mwenyekiti wa Shirika hilo ni Martin Gastered ambaye pia mkazi wa nchini Sweden


Tangazo

  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI June 05, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • DC MWENDA ATEMBELEA MRADI WA UJENZI WA SHULE MPYA YA SEKONDARI YA AMALI KITUKUTU

    May 08, 2025
  • KAMATI YA FEDHA, UONGOZI NA MIPANGO YA HALMASHAURI YA WILAYA YA IRAMBA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO

    May 06, 2025
  • DC MWENDA ATOA WITO KWA WALIMU WA SHULE ZA MSINGI KUIMARISHA UFUNDISHAJI KWA MADARASA YA MITIHANI

    May 06, 2025
  • JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI WILAYANI IRAMBA LATOA ELIMU YA KINGA DHIDI MAJANGA YA MOTO KWA MADIWANI NA WANANCHI

    May 02, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.