• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Mkuu wa wilaya ya Iramba mkoani Singida, Suleiman Mwenda ameiagiza Idara ya Afya kufikisha chanjo ya polio katika taasisi mbalimbali ikiwemo Magereza.

Posted on: April 26th, 2022

Na Hemedi Munga

tehama@irambadc.go.tz


Singida-Iramba. Mkuu wa wilaya ya Iramba mkoani Singida, Suleiman Mwenda ameiagiza Idara ya Afya kufikisha chanjo ya polio katika taasisi mbalimbali ikiwemo Magereza.

Mwenda ametoa agizo hilo leo Jumatatu Arili 25, 2022 wakati wa mafunzo ya chanjo ya polio kwa Kamati ya Msingi ngazi ya jamii yaliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ofisi ya Mkuu wa wilaya hiyo mjini hapa.

“Sasa nitoe maelekezo rasmi kuwa zoezi la chanjo lifike katika maeneo muhimu hasa katika kila tukio litakalokusanya watu, watu wa Idara ya afya mfike kutoa elimu ili watu wapate chanjo.” aliagiza na kuongeza kuwa

 “Ninatoa maagizo maalumu kwa Idara ya afya kutembelea Magereza kukagua kama kuna watoto na kuhakikisha watoto hao wanapata huduma muhimu za afya ikiwemo chanjo ya polio.”

Halikadhalika, Mkuu huyo wa wilaya aliitaka kamati hiyo kuifikia jamii ili kuipa elimu na kuisisitiza kuendelea kuchukua tahadhari ya maambukizi dhidi ya virusi vya UKWIMI hasa katika maeneo ya barabara kuu itokayo Singida kuelekea jijini Mwanza, Migodini na Ziwa Kitangiri.

“Ndugu zangu ni wajibu wetu sisi tuchukue tahadhari, pia tutoe elimu kwa jamii inayotuzunguka.” Alisistiza

Aidha, aliongeza kuwa upo ugonjwa wa Homa ya Inni ambao unaonekana kuwa hatari sana katika afya ya mwanadamu, hivyo ni vyema wananchi na watumishi wakachukua tahadhari na kuchanja.

“Nitoe wito kwa watumishi wote na kuwahamasisha wananchi kuchoma chanjo ya Homa ya Inni ambayo hushambulia zaidi Inni, habari njema nikwamba chanjo hiyo ipo.”

Akiongelea kuhusu ugonjwa wa malaria, Mkuu huyo wa wilaya aliendelea kuitaka kamati hiyo kuchukua tahadhari na kuielimisha jamii kujikinga na ugonjwa wa malaria.

“Tunatamani na ndio lengo letu ifike wakati wilaya ya Iramba na nchi kwa ujumla tunakuwa na zero malaria, hivyo tuendelee kuwahamasisha wananchi wafukie madimbwi, kutumia neti na kusafisha kila penye mazalia ya mbu.”

Pia, aliitaka kamati hiyo kuendelea kuhamasisha watu kujitolea katika zoezi la kuchangia damu ili kukidhi haja ya hitajio la damu pale inapotokea wagonjwa wanahitaji damu.

Katika kuhakikisha elimu ya chanjo inawafikia watu wengi katika jamii, Mkuu huyo wa wilaya aliitaka kamati kuongeza wigo wa kushirikisha viongozi kuanzia ngazi ya kijiji.

Hatua hiyo itasaidia jamii kupata elimu sahihi ya chanjo na kuepukana na upotoshaji na tamaduni za kuwafunga watoto mvuje na hirizi wakidaiwa kuamini kuwa ni kinga kuliko chanjo hizi za kitaalamu.

“Ndugu zangu tukifanikiwa kushirikisha viongozi kuanzia ngazi ya kijiji elimu itafika kwa jamii na tutafanikiwa kupunguza vifo vya watoto.”

Akiongea katika kikao hicho Mkuu wa Idara ya Afya, Dkt Hussein Sepoko alisema kuwa kampeni ya chanjo ya polio itaanza Aprili 28, 2022, hivyo aliwaomba wanakamti hao kuwa mabalozi wa kufikisha elimu sahihi ya chanjo.

“Ndugu viongozi! Niwaombe tufahamu kuwa chanjo hii ya polio lengo lake ni kuwaongezea kinga watoto na si vinginevyo.”

Kwa upande wake mmoja wa washiriki katika mafunzo hayo Mkuu wa Gereza la Kiomboi Iramba, Denis Njegite aliiomba Idara ya Afya kutoa nakala ya mafunzo hayo ili kuwawezesha wao kufikisha ujumbe huo katika tasisi wanazoziongoza.

Naye katibu tawala wa wilaya hiyo, Pius Songoma alishauri timu hiyo kuelekeza nguvu katika maeneo ya machimboni, wafugaji na ziwani ili kufikisha chanjo hiyo kwa lengo lakutimiza zoezi la kitaifa.

MWISHO

Tangazo

  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI June 05, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • AFISA MWANDIKISHAJI JIMBO LA IRAMBA MAGHARIBI AWATAKA WAENDESHA VIFAA VYA BVR NA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI KUFANYA KAZI KWA WELEDI ILI KUFANIKISHA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI

    May 14, 2025
  • KAMATI YA AFYA YA MSINGI (PHC) IRAMBA YAJADILI MIKAKATI YA CHANJO YA POLIO SINDANO YA PILI

    May 09, 2025
  • DC MWENDA ATEMBELEA MRADI WA UJENZI WA SHULE MPYA YA SEKONDARI YA AMALI KITUKUTU

    May 08, 2025
  • KAMATI YA FEDHA, UONGOZI NA MIPANGO YA HALMASHAURI YA WILAYA YA IRAMBA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO

    May 06, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.