• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Comments |
Iramba District Council
Iramba District Council

The United Republic of Tanzania Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Iramba District Council

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

MKUU wa wilaya ya Iramba mkoani Singida, Suleiman Mwenda ameiagiza Kamati ya Maendeleo ya Kijiji cha Ndulungu kukubaliana kimaandishi kuomba kijiji hicho kuwa kata au kuiomba TAMISEMI kubadilisha matumizi ya Tsh 250 milioni zije kijiji cha Ndulungu na Tsh

Posted on: January 16th, 2022

Na Hemedi Munga

tehama@irambadc.go.tz

Singida - Iramba. MKUU wa wilaya ya Iramba mkoani Singida, Suleiman Mwenda ameiagiza Kamati ya Maendeleo ya Kijiji cha Ndulungu kukubaliana kimaandishi kuomba kijiji hicho kuwa kata au kuiomba TAMISEMI kubadilisha matumizi ya Tsh 250 milioni zije kijiji cha Ndulungu na Tsh 355 milioni zipelekwe kijiji cha Mwandugyembe.

Mwenda ametoa agizo hilo leo Ijumaa Januari 14, 2022 wakati alipokutana na wananchi wa kijiji cha Ndulungu wilayani hapa baada ya kudaiwa kuibuka mgogoro wa wananchi wa kijiji cha Ndulungu kutokubaliana na ujenzi wa kituo cha Afya kijiji cha Mwandugyembe katika kata hiyo.

Akiongea na wananchi hao, Mwenda amewataka kuwa na subira kipindi ambacho amewapa nafasi ya kuandika muhtasari wa kubadilisha matumizi ya fedha ambazo wameletewa kwa ajili ya kutengenza barabara kijijini hapo.

“Ndugu za kuna njia mbili ya kutatua mgogoro huu ambapo moja ni kuiandikia TAMISEMI kuwaomba kufuata ushauri wa wananchi wakubadilisha matumizi ya Tsh 355 za kutengeneza barabara katika kijiji cha Ndulungu  zipelekwe kijiji cha Mwandugyembe huku Tsh 250 za ujezi wa kituo cha Afya kijiji cha  Mwandugyembe ziletwe kijiji cha Ndulungu.” Alisema Mkuu huyo wa Wilaya na kuongeza kuwa

“Namna ya pili ni kuandaa muhtasari wa kuomba kata ambapo tukipata kata tutapata huduma ya shule, kituo cha afya na huduma nyingine za msingi zinazostahili kuwepo katani.”

Aidha aliwataka kuwa makini wakati wakuchagua kati ya hayo waliyokubaliana ili baada ya mchakato huo kusiwepo tena malalamiko.

“Niagize kuwa jambo hili muhakikishe mnashirikisha kijiji cha Mwandugyembe, Mahola, Kipuma pamoja na Ndulungu ili kupata maamuzi yasiyokuwa na manunguniko tena.” Alisema

Katika hatua nyingine amewataka wananchi hao kuhakikisha wanalinda amani kwa sababu ndio msingi wa maisha bora na kupata maendeleo yao.

“Niwaombe ndugu zangu tunakila sababu ya kumshukuru Mbunge wetu ambaye ni Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Nchemba ambaye amekuwa akipambana kuhakikisha fedha hizi zinatufikia kupitia wizara ya TAMISEMI, hivyo tutunze amani yetu katika kutekeleza miradi hii.”

Awali akiongea katika kikao hicho, Diwani wa kata ya Ndulungu, Ndugu Jilole alisema kuwa Kamati ya Maendeleo ya Kata ya wakati wa Diwani Iddi Muyonga walikubaliana kuwa kijiji cha Mwandugyembe na Mahola pajengwe Sekondari huku kijiji cha Kipuma na Ndulungu kujengwe kituo cha Afya.

Suala ya kujenga kituo cha afya kijiji cha Mwandugyembe kilipelekea baadhi ya wananchi wa kijiji cha Mahola na Ndulungu kugomea shughuli za maendeleo na hivyo kufika kwa mkuu wa wilaya kwa ajili ya utatuzi.

Kwa upande wake mmoja wa wananchi wa kijiji cha Ndulungu akifikisha kero yake kwa mkuu huyo wa wilaya, Iddi Nyauli  alisema kuwa kama mkuu huyo wa wilaya asinge fika kutatua mgogoro huo basi wangekwenda kushitaki kwa mkuu wa mkoa huo.

“Nikushukuru sana kwa hekima zako kwa utatuzi wa mgogoro huu kwa sababu usinge utatua huu mgogoro tungeufikisha mpaka kwa Mhe Rais Samia.” Alisema na kuongeza kuwa

“Kama ungozi wa wilaya ungeliona kuwa kijiji cha Ndulungu hakipo wilaya ya Iramba basi tupelekwe wilaya ya Ikungi.”

Naye Zakiya Kapande mkazi wa kijiji hicho akawasilisha kero yake mbele ya mkuu huyo wa wilaya na kumuomba kuwasaidia akina mama ambao wanaumia kwa michango mbalimbali wanayoitoa kufuatia shughuli za maendeleo.

“Nikombe Mkuu wa wilaya utusaidie sisi akina mama kwa sababu yapo magumu tunayoyapitia kutoka katika serikali yetu ya kijiji.”

MWISHO

Announcements

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU January 02, 2026
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI June 05, 2025
  • View All

Latest News

  • MAONESHO YA MATUMIZI YA PEMBEJEO ZA KILIMO (MBEGU, MBOLEA NA VIUATILIFU) HALMASHAURI YA WILAYA YA IRAMBA DISEMBA 29-30, 2025

    December 28, 2025
  • HERI YA SIKUKUU YA KRISMASI NA MWAKA MPYA 2026

    December 25, 2025
  • DC MWENDA AWATAKA WALIMU IRAMBA KUONGEZA UBUNIFU NA BIDII KUINUA UFAULU

    December 09, 2025
  • HERI YA MIAKA 64 YA UHURU WA TANZANIA BARA

    December 09, 2025
  • View All

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
More Videos

Quick Links

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Related Links

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    KIOMBOI, IRAMBA

    Postal Address: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Telephone: 026 - 2532253

    Mobile: 026 - 2533001

    Email: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.