• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Mkuu wa Wilaya ya Iramba mkoani Singida, Suleiman Mwenda amempongeza Mkurugenzi Mtendaji, Mhandisi Michael Matomora kwa kutilia mkazo suala la mapato na kutamani kuona bajeti ya Iramba inavuka Tsh 1.4 bilioni.

Posted on: January 28th, 2022

Na Hemedi Munga

tehama@irambadc.go.tz

Singida - Iramba. Mkuu wa Wilaya ya Iramba mkoani Singida, Suleiman Mwenda amempongeza Mkurugenzi Mtendaji, Mhandisi Michael Matomora kwa kutilia mkazo suala la mapato na kutamani kuona bajeti ya Iramba inavuka Tsh 1.4 bilioni.

Mwenda ametoa pongezi hizo leo Ijumaa Januari 28, 2022 wakati alipokuwa akiongea na Madiwani katika kikao cha Baraza la Madiwani kota ya pili ya mwaka wa fedha 2021/2022 katika ukumbi mdogo wa Halmashauri hiyo mjini hapa.

“Waheshimiwa Madiwani pamoja na wataalamu wote niwaombe tusimamie vyanzo vyetu vya mapato tunaouwezo wa kukusanya fedha nyingi sana katika Halmashauri yetu.” Alisema Mkuu huyo wa wilaya

Aidha, alifafanua vyanzo mbalimbali vya ukusanyaji wa mapato ikiwemo kuanzisha chanzo cha kuingiza mifugo katika hifadhi mbalimbali hasa wafugaji ambao wamehamia katika hifadhi hizo bila ya kufuata sheria na utaratibu.

Pia aliahidi kuwa katika kipindi cha uongozi wake atahakikisha chanzo cha madini ya dhahabu kinazalishwa kufikia gramu laki sita (600,000)   kwa mwaka ukilinganisha na kiwango cha gramu  laki tatu na kumi na tisa elfu ( 319,000)  ambazo zilikuwa zinazalishwa kwa mwaka katika miaka ya nyuma.

“Tukipata uzalishaji wa namna hiyo ni hakika gawio lake litakuwa kubwa, hivyo huenda nusu ya bajeti ya Iramba ikawa inatoka katika chanzo cha madini.” Alisema

Kufuatia maono hayo ya kuinua Iramba kuwa na bajeti kubwa, Mwenda amewaomba Madiwani wote kuhakikisha wanasimamia shughuli za maendeleo katika kata zao ikiwemo ukusanyaji wa mapato.

Halikadhalika, Mwenda amewataka watendaji wote kuhakikisha wanatimiza wajibu wao na kufanya utoaji wa huduma kwa wananchi zinakuwa nyepesi hatimaye wananchi wakiwemo wajasiriamali kutamani kufanya kazi na Halmashauri yao.

“Nitoe wito kwa watendaji wenzangu wa serikali tunapokuwa tunawasaidia wananchi kuhakikisha tunafuata sheria, kanuni na taratibu.” Alisema

Akiongea katika Baraza hilo Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo, Innocent Msengi alisema kuwa chanzo cha kuingiza mifugo ni kizuri, hivyo watakaa katika vikao vyao kuona namna bora ya kupitisha sheria ili kuweza kukusanya chanzo hicho.

Aidha, amewataka watendaji hao kuendelea kudumisha ushirikiano walionao ili kuhakikisha wanafikia malengo ya kuinyanyua Halmashauri hiyo katika ukusanyaji wa mapato.

“Niwaombe sana ndugu zangu vikao hivi vitakuwa vinatija ikiwa tutarudi katika vikao vijavyo halafu tukaona kunamabadiliko makubwa wa haya ambayo tumekubaliana.” Alisema Msengi

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo akiongea katika Baraza hilo, Mhandisi Michael Matomora alifafanua namna ambavyo anapambana kuhakikisha Halmashauri hiyo haipati hati yenye mashaka wala hati chafu katika Hesabu za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Serikali.

“Mheshimiwa Mwenyekiti naomba kutoa ufafanuzi kuwa ili madokezo yapite katika ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji lazima yafuate utaratibu na kanuni za matumizi ya fedha za serikali.”Alisema Matomora na kuongeza kuwa

“Ni lazima tukakusanye mapato kwa sababu hatuwezi kutumia fedha kama hatujakusanya.”

Halikadhalika, alibainisha kuwa fedha ya serikali uliyoiweka katika bajeti na ukaikusanya usipoitumia ni kutengeneza hoja ya ukaguzi.

“Mimi siwezi kuzuia fedha ya serikali isitumike kwa sababu itakuja hoja kuwa Mkurugenzi Mtendaji hatumii fedha na hiyo hoja mimi siwezi kuikubali.” Alisisitiza

Aidha, aliongeza kuwa ataendelea kusimamia matumizi ya fedha za serikali yaliokuwa halali kwa sababu ya kuhakikisha Halmashauri inapunguza hoja za ukaguzi.

Pia amewataka wananchi wote katika Halmashauri hiyo, kufikisha mapendekezo yao ambayo yanatakiwa kuingia katika bajeti ya mwaka 2022/2023.

“Huu ni wakati wa bajeti ya mwaka wa fedha 2022/2023, hivyo nitoe wito kwa wananchi wote kuwa kama kuna mwananchi anaushauri anaalikwa kutoa ushauri kuwa nini Halmashauri ifanye katika mwaka wa fedha.” Alitoa wito Matomora

Baraza la Madiwani limekaa kikao chake cha kota ya pili katika mwaka wa fedha 2021/2022.

MWISHO

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • KIDATO CHA KWANZA KURIPOTI SHULE January 13, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • MAAFISA ELIMU KATA 136 MKOANI SINGIDA WAPATIWA MAFUNZO KUHUSU USIMAMIZI WA SHULE NA UJAZAJI TAKWIMU KATIKA MFUMO WA "SIS"

    March 24, 2025
  • DC MWENDA AWASISITIZA WALIPA KODI KUFANYA MAKADIRIO YA KODI KABLA YA MACHI 31, 2025

    March 20, 2025
  • DC MWENDA NA WAZIRI MWIGULU NCHEMBA WACHANGIA JUMLA YA MADAWATI 98 SHULE YA MSINGI MSANSAO ILIYOPO KATA YA MTEKENTE

    March 10, 2025
  • WALIMU WAKUU 108 WA SHULE ZA MSINGI NA MAAFISA ELIMU KATA 20 WILAYANI IRAMBA WAPEWA MAFUNZO ENDELEVU YA USIMAMIZI WA UFUNDISHAJI NA UJIFUNZAJI FANISI KUPITIA JUMUIYA ZA KUJIFUNZA ZA WALIMU WAKUU NA MAAFISA ELIMU KATA

    March 19, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.