• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

MKUU wa wilaya ya Iramba mkoani Singida, Suleiman Mwenda amemshukuru na kumpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan kwa fedha alizoipatia Wilaya ya Iramba kutekeleza miradi ya maendeleo.

Posted on: January 16th, 2022

Na Hemedi Munga

tehama@irambadc.go.tz

Singida - Iramba. MKUU wa wilaya ya Iramba mkoani Singida, Suleiman Mwenda amemshukuru na kumpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan kwa fedha alizoipatia Wilaya ya Iramba kutekeleza miradi ya maendeleo.

Mwenda ametoa pongezi hizo leo Jumapili 16, 2022 wakati akisoma taarifa ya utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi (CCM) ya mwaka 2020/2025 kwa kipindi cha kuanzia julai hadi Disemba katika ukumbi mkubwa wa Halmashauri hiyo mjini hapa.

“Takribani 20 bilioni zimeletwa katika Wilaya hii kwa ajili ya kutekeleza miradi ya maendeleo, kiwango hichi ni kikubwa sana, hivyo tunayo sababu ya kumshukuru Rais wetu Samia Suluhu Hassan.” Alisema komredi Mwenda na kuongeza kuwa

“Kwa kweli ni mara ya kwanza tena kota ya kwanza kwa mwaka wa fedha 2021/2022 TARURA wamepata 6.5 bilioni kwa ajili ya barabara huku bilioni 5.2 kwa ajili ya miradi ya maji na nyingine nyingi katika sekta ya afya na elimu.”

Kufuatia kupata fedha hizo nyingi, Komderi Mwenda amewataka viongozi wote ngazi mbalimbali wilayani hapa kuhakikisha wanasimamia kutekeleza miradi ya maendeleo kwa ufanisi na kiwango kinachohitajika.

“Sisi serikali tunayodhima kuhakikisha tunaisimamia fedha hii iliyoletwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzani, Samia Suluhu Hassan ili ifanye kazi iliyokusudiwa na kukamilika kwa kiwango stahiki.” Alisema

Pia amewataka wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Wilaya wa Chama cha Mapinduzi (CCM) kushirikiana na serikali katika mambo mbalimbali kwa sababu umoja wao ni ushindi katika kila jambo.

“Nitowe wito kwa viongozi wenzangu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) niwaombe tushirikiane ili kutimiza matakwa ya ilani ya Chama chetu hatimaye kuboresha maisha ya wananchi ambao wamekichagua chama hichi na kukipa serikali.”

Aidha akiongelea kuhusu maisha yake ndani ya Chama cha Mapinduzi (CCM)  Komredi Mwenda alisema kuwa anamshukuru Rais Samia kwa kumteua na kumuamini kuwa Mkuu wa wilaya hiyo, kazi ambayo itamfanya kuendelea kuvaa vazi la kijani ambalo analipenda tangu akiwa chipukizi katika chama hicho.

“Niseme kweli moja ya kitu kilichonifanya kuipenda CCM na kuingia katika kundi la chipukizi la chama hicho nikiwa darasa la pili ni nyimbo ambazo zilizokuwa zikiimbwa na Komredi Kaptain John Komba aliyekuwa Mbunge wa Mbinga Magharibi na muimbaji mkuu wa nyimbo za siasa nchini Tanzania.” Alisema

Akiongea katika mkutano huo kwa niamba ya wajumbe wote wa Halmashauri Kuu ya chama hicho, Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) wilayani humo, Ashel Joel ameipongeza serikali ya amwamu ya sita inayoongozwa na Rais Samia kwa kuipatia fedha nyingi wilaya hiyo.

“Nimpongeze Rais wetu kwa kweli haijawahi tokea kupokea fedha nyingi kiasi hichi katika wilaya yetu ya Iramba kwa ajili ya miradi mbalimbali.” Alipongeza na kuongeza kuwa

“Tuko pamoja na mama na tutaendelea kuwa pamoja naye, tunaendelea kumpongeza kwa kazi kubwa anayoifanya ya kuliongoza taifa letu, mungu ampe afya njema ili aendelee kututumikia sawa na mapenzi yake.”

Kwa upande wake mmoja wa wajumbe wa Halmashauri Kuu ya chama hicho, Diwani wa kata ya Ntwike, Albert Makwala akiongea kwa niaba ya wajumbe hao alisema kuwa wameipokea taarifa ya utekelezaji wa Chama cha Mapinduzi (CCM) na hivyo wapo tayari kuijadili na kutoa maagizo kwa wataalamu.

Aidha anaishukuru serikali kwa kuitengea kata hiyo 460 milioni kwa ajili ya kufungua barabara ya kutoka Kiomboi kwenda Ntwike na kushauri kuwa wataalamu wa TARURA wangeanza na kivuko.

Naye Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama hicho kata ya Kiomboi, Israel Shimba akashauri kuhusu kumalizia Zahanati ambayo ilijengwa katika kata hiyo ili kuwasaidia akinamama wajawazito kupata huduma kwa haraka katika kituo hicho badala ya kupelekwa hospitali ya kiomboi ambayo inadaiwa kuwa mbali na wakazi hao.

MWISHO

Tangazo

  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI June 05, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • DC MWENDA ATEMBELEA MRADI WA UJENZI WA SHULE MPYA YA SEKONDARI YA AMALI KITUKUTU

    May 08, 2025
  • KAMATI YA FEDHA, UONGOZI NA MIPANGO YA HALMASHAURI YA WILAYA YA IRAMBA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO

    May 06, 2025
  • DC MWENDA ATOA WITO KWA WALIMU WA SHULE ZA MSINGI KUIMARISHA UFUNDISHAJI KWA MADARASA YA MITIHANI

    May 06, 2025
  • JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI WILAYANI IRAMBA LATOA ELIMU YA KINGA DHIDI MAJANGA YA MOTO KWA MADIWANI NA WANANCHI

    May 02, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.