• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Mkuu wa Wilaya ya Iramba mkoani Singida, Suleiman Mwenda amemuagiza Afisa Ardhi wilaya ya Iramba, Valerian Msigala kulipima eneo la Maluga linalodaiwa kuwa na mgogoro tangu kutoka katika siasa za vijiji na ujamaa ili kujua ukubwa wa eneo hilo na kutatua m

Posted on: January 26th, 2022

Na Hemedi Munga

tehama@irambadc.go.tz

Singida - Iramba. Mkuu wa Wilaya ya Iramba mkoani Singida, Suleiman Mwenda amemuagiza Afisa Ardhi wilaya ya Iramba, Valerian Msigala kulipima eneo la Maluga linalodaiwa kuwa na mgogoro tangu kutoka katika siasa za vijiji na ujamaa ili kujua ukubwa wa eneo hilo na kutatua mgogoro huo.

Mwenda ametoa agizo hilo leo Jumatano Januari 26, 2022 wakati alipokuwa akiongea na wananchi wa kijiji cha Maluga wilayani hapa.

Akiongea na wananchi hao mkuu huyo wa wilaya amewaeleza kuwa kila mmoja atapata haki yake kwa kuhakikisha kuwa baada ya kutoa hekari 50 zinazodaiwa kumilikwa na mzee Amosi Shigimbi ambaye kwa sasa ni marehemu na mgogoro huo kuibuliwa na wajukuu wake.

“Niwahakikishie ndugu zangu kuwa wiki hii wataalam wa ardhi watakuja kutuonesha mipaka ya eneo hilo ili kufahamu eneo linalobaki ili kila mmoja apate ardhi aendeshe maisha yake kwa utulivu.” Alisema Mwenda

Aidha, aliongeza kuwa tunapaswa kuwaheshimu wazee wetu kwa sababu wanapotuombea dua ndio tunaweza kupata baraka.

Akiongelea kuhusu makaburi yaliopo katika ardhi hiyo, Mwenda amewataka wananchi hao kuheshimu ndugu ambao wametangulia mbele ya haki.

“Sisi sote ni wanakijiji ni lazima tuishi katika namna ya kupendana,kusaidiana na kushirikiana kwa sababu hayo makaburi wamehifadhiwa binaadamu ambao ni wazee wa wenzako.” Alisema

Pia aliwaomba wananchi hao, kufahamu kuwa waliohifadhiwa hapo ni wazee wa wenzao na binaadamu wenzao ni vyema wangeendelea kuheshimiwa.

Kufuatia hali hiyo Mwenda amewataka wananchi hao kuheshimu makaburi ya wanaadamu ambao walifariki na kuzikwa hapo.

Awali akiwasilisha malalamiko hayo kwa mkuu wa wilaya hiyo, Elizabeth Israel alishukuru hatua zilizochukuliwa na mkuu huyo wa wilaya kwa kutatua mgogoro huo ambao umekuwa wa muda mrefu.

“Mgogoro huo uliibuka baada ya tamko la Mwl. Julius K. Nyerere kusema kuwa watu warudi katika mahame yao, hivyo walivyorudi ndio ulipatikana mwanya wa watu kumiliki ardhi ambayo isiokuwa yakwao kutokana na oparesheni ya mwaka 1974 hadi 1976.” Alisema Israel

Halikadhalika, aliongeza kuwa ndio nafasi ambayo Mzee Amosi shigimbi alirudi katika ardhi yake kama walivyorudi watu wengine katika miaka hiyo.

Kwa upande wake mmoja wa wazee waliokuepo katika miaka hiyo ya siasa ya vijiji na ujamaa, Elias Mpwai alisema kuwa eneo la kujenga nyumba miguu 70 alipewa na Amosi Shigimbi wakati huo.

“Mzee Shigimbi alinipa eneo hilo kwa sababu nilikuwa nikichunga mifugo yake, hivyo nikawa nalima eneo hilo mpaka wajukuu wangu waliponisaidia kujenga nyumba na baadae kuibomoa kutokana na mamlaka ya wakati huo.” Alisema Mpwai

Kufuatia hali hiyo, Mpwai alimueleza mkuu huyo wa wilaya kwa sasa anapata tabu kwa sababu hana sehemu ya kulima kwa lengo la kujipatia chakula, hivyo amebaki anatanga tanga.

MWISHO

Tangazo

  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI June 05, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • AFISA MWANDIKISHAJI JIMBO LA IRAMBA MAGHARIBI AWATAKA WAENDESHA VIFAA VYA BVR NA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI KUFANYA KAZI KWA WELEDI ILI KUFANIKISHA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI

    May 14, 2025
  • KAMATI YA AFYA YA MSINGI (PHC) IRAMBA YAJADILI MIKAKATI YA CHANJO YA POLIO SINDANO YA PILI

    May 09, 2025
  • DC MWENDA ATEMBELEA MRADI WA UJENZI WA SHULE MPYA YA SEKONDARI YA AMALI KITUKUTU

    May 08, 2025
  • KAMATI YA FEDHA, UONGOZI NA MIPANGO YA HALMASHAURI YA WILAYA YA IRAMBA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO

    May 06, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.