• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

MKUU wa wilaya ya Iramba mkoani Singida, Suleiman Mwenda amepiga marufuku wananchi kufanya shughuli mbalimbali kando mwa vyanzo vya maji.

Posted on: November 11th, 2021

NA HEMEDI MUNGA

tehama@irambadc.go.tz

Iramba. MKUU wa wilaya ya Iramba mkoani Singida, Suleiman Mwenda amepiga marufuku wananchi kufanya shughuli mbalimbali kando mwa vyanzo vya maji.

Mwemda ameeleza hayo leo Jumatano Okotoba 10, 2021 akiwa na Kamati ya Ulinzi na Usalama katika ziara ya ukaguzi wa miradi ya maji kata ya Maluga Wilayani ya hapa.

Amemtaka Mhandisi wa Maji, Ezra Mwacha kuhakikisha miradi hiyo inakamilika kwa wakati na iwe na viwango vinavyofanana na fedha iliyotolewa.

Katika hatua nyingine amezitaka Serikali za Vijiji kuhakikisha vinalinda vyanzo vya maji ambapo Serikali imewekeza fedha nyingi ili huduma hiyo itatuwe changamoto ya kupatikana maji kwa muda mrefu.

“Niwaagize Wenyeviti wa Vijiji vyote ambavyo miradi ya maji inatekelezwa kulinda miradi ambayo Serikali inajenga kwa fedha nyingi na kutouza maeneyo ya vyanzo vya maji.” Ameagiza na kuongeza kuwa

“Hakikisheni mmepanda miti katika vyanzo vyote vya maji ili kulinda vyanzo hivyo kwa masilahi yetu wote.”

Halikadhalika, amemtaka Mhandisi wa Maji, Mafundi Sanifu na Venyeviti wa Vijiji katika maeneo mbalimbali yanayotekeleza miradi hiyo kuijenga kwa kiwango bora ili kutimiza makusudio ya Mhe, Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan ya kuhakikisha maji yanapatikana kila eneo na muda wote ili kumtua mama ndoo ya maji.

Akiongea na hadhira iliyopo katika ziara hiyo mmoja wa wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ambaye ni Mkuu wa Jeshi la Wananchi Wilayani hapo, SSP. Peter Lusesa amewataka wenyeviti wa vijiji kuhakikisha wanatumia sheria ndogo kulinda vyanzo vya maji hali ambayo itawaepusha na migogoro ya hapa na pale.

Awali akitoa tarifa fupi ya utekelezaji wa miradi ya maji mbele ya Mkuu huyo wa Wilaya, Meneja wa Maji Wilayani hapo, Mhandisi Ezra Mwacha alisema kuwa kazi zinazoendelea katika maeneo yote ambayo miradi inatekelezwa ni ujenzi wa matenki ya kuhifazia maji mita 12 na yenye ujazo wa lita 50,000, nyumba za  kuhifadhia mashine (vyanzo vya maji), uchimbaji wa mitaro na DP nane katika kila mradi.  

Aidha amefafanua kuwa miradi mitatu aliyoitembelea Mkuu wa Wilaya inatakribani 1.2 Bilioni na kumuhakikishia kuwa ifikapo Machi 2022 miradi itakuwa imekamilika.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kijiji cha Zinziligi Tarafa ya Ndago Wilayani hapa, Anthony Kitalu amemshukuru Rais Samia kwa kuwaletea miradi ya maji ambayo inatatua changamoto ya kupata maji waliyokuwa nayo kwa kipindi kirefu.

“Mhe Mkuu wa Wilaya ! Wananchi hawa wameipokea miradi hii kwa mikono miwili na kukuomba wewe uwafikishie salamu kwa Rais Samia kwa huruma yake ya kuwaletea maji.” Alisema Kitalu

MWISHO

Ujenzi wa tanki la kuhifadhia maji lenye urefu wa mita 12 na lenye ujazo wa lita 50,000 likijengwa kata ya Maluga wilayani Iramba Mkoa wa Singida. Picha na Hemedi Munga

Mkuu wa Wilaya ya Iramba Mkoani Singida, Suleimani Mwenda akiwa na wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama wa wilaya hiyo wakisikiliza taarifa ya Ujenzi wa tanki la kuhifadhia maji lenye urefu wa mita 12 na lenye ujazo wa lita 50,000 likijengwa kijiji cha Zinziligi wilayani Iramba Mkoa wa Singida. Picha na Hemedi Munga

Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA IRAMBA November 03, 2023
  • KUITWA KAZINI November 29, 2023
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2018 HALMASHAURI YA WILAYA IRAMBA January 05, 2019
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA KIDATO CHA PILI (FTNA) 2018 January 05, 2019
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • Wajumbe wa Kamati ya Fedha, Utawala na Mipango ya Halmashauri ya Wilaya ya Iramba wamefanya ziara ya Ukaguzi wa Miradi mbalimbali ya Maendeleo inayotekelezwa Wilayani Iramba

    October 24, 2023
  • RAIS DKT. SAMIA AHITIMISHA ZIARA YAKE MKOANI SINGIDA KWA KISHINDO, WANANCHI WAMSHUKURU KWA MIRADI YA MAENDELEO

    October 17, 2023
  • MKUU wa Mkoa wa Singida Peter Serukamba amepokea rasmi Mbio za Mwenge wa Uhuru kutoka Mkoani Tabora na aliyekabidhi ni Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Balozi Batlida Briani.

    September 22, 2023
  • MKIMBIZA Mwenge wa Uhuru Kitaifa, Abdalla Shaibu Kaim amewataka Watanzania kuhakikisha wanakemea vitendo vya rushwa kwa maelezo kuwa rushwa inakwamisha maendeleo ya Mkoa pamoja na Taifa kwa ujumla

    September 22, 2023
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.