• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Mkuu wa wilaya ya Iramba mkoani Singida, Suleiman Mwenda amewaagiza wamiliki wa mabucha, wachinjaji na wauzaji wa nyama kuuza kilo ya nyama mchaganyiko kwa Tsh 7000 na kilo ya nyama isiyokuwa na mifupa kwa Tsh 8000.

Posted on: April 7th, 2022

Na Hemedi Munga

tehama@irambadc.go.tz


Singida - Iramba. Mkuu wa wilaya ya Iramba mkoani Singida, Suleiman Mwenda amewaagiza wamiliki wa mabucha, wachinjaji na wauzaji wa nyama kuuza kilo ya nyama mchaganyiko kwa Tsh 7000 na kilo ya nyama isiyokuwa na mifupa kwa Tsh 8000.

Mwenda ametoa agizo hilo leo Jumatano Aprili 6, 2022 wakati alipokuwa akiongea na wamiliki wa mabucha, wachinjaji na wauzaji wa nyama katika ukumbi mdogo wa mikutano wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba.

Agizo hilo linakuja ikiwa ni siku chache baada ya Mkuu huyo wa wilaya kufanya uchunguzi wa bei za kuuza nyama kwa kilo moja katika wilaya za Ikungi, Singida Manispaa na Mkalama ambako kote huko wamekuwa wakiuza kilo moja  ya nyama kwa Tsh 7000.

Wakati wilayani Iramba hali ikiwa ni tofauti ambapo katika eneo la Mtekente kilo moja ya nyama ikiuzwa kwa  Tsh 7000, Shelui Tsh 7000, Misigiri Tsh 7000, Oldi Kiomboi 7000 na Mjini Kiomboi ikiuzwa katika baadhi ya bucha kwa Tsh 8000, 9000 hadi 10,000 kwa kilo moja.

Ndani ya wilaya moja bidhaa moja ina bei tofauti tofauti kitu ambacho sio rafiki hata kama tuko katika soko huria, hivyo ipo haja ya kuwa na bei ya juu elekezi kwa wilaya nzima.

“Ni jambo la ajabu kabisa katika Jiji la Mwanza kilo moja ya nyama inauzwa Tsh 7000 halafu hapa Kiomboi kilo moja ya nyama inauzwa kwa Tsh 9000 mpaka 10000, hivyo tunakubaliana kuwa kiwango cha bei ya juu ya kilo moja ya nyama itakuwa Tsh 7000.” Alisisitiza Mkuu huyo wa wilaya nakuongeza kuwa

“Bei elekezi kwa sasa ni Tsh 7000 na hatutegemei kukuta bucha katika wilaya yetu inauza kilo moja ya nyama kwa bei zaidi ya Tsh 7000.”

Aidha, Mwenda alisema kuwa wanahitaji kuona katika wilaya hiyo katika siku za usoni wanapata machinjiyo ya kisasa ambayo yatakuwa yakiwezesha wanyama kuchinjwa hapo na kufungasha kwa ajili ya kuunza ndani ya wilaya, mkoa, Tanzania nzima na nje ya nchi.

Pia, alionesha kusikitika baada ya kuona ongezeko kubwa la bei ya nyama wakati anafika akiwa mkuu wa wilaya hiyo, kilo ya nyama ilikuwa ikiuzwa kwa Tsh 6000.

Halikadhalika, Mwenda amemuelekeza Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo kuhakikisha katika bajeti ya mwaka wa fedha 2023/2024 wanatenga fedha kwa ajili ya kujenga machinjio ya kisasa katika kila tarafa ikiwa ni pamoja na kuhakikisha kila nyama inapimwa na daktari ili kuthibitisha usalama na ubora wake.

Katika kuhakikisha nyanja ya mifugo inachangia katika mapato ya Halmashauri, Mkuu wa Wilaya hiyo kwa kushirikiana na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo, Mhandisi Michael Matomora walifanikiwa kuinua mapato yanayotokana na kuuza mifugo katika minada kutoka kwenye Tsh 16 hadi 18 milioni kwa makusanyo ya  jumla ambapo kwa sasa imefikia Tsh  40 hadi 50 milioni.

Akiongea katika kikao hicho Mkuu wa jeshi la Polisi wilayani hapa Henry Makwasa amewataka wafanyabiarasha hao kutoa taarifa ya watu wanaouza nyama mitaani ili jeshi la polisi liwachukulie hatu kwa sababu hao ndio wanaodaiwa kuwa na tabia ya kuiba mifugo na kuchinja bila ya kufuata utaratibu.

Makwasa alimshauri Mkuu wa Idara ya Mifugo Dkt Dotto Thomas kuendesha oparesheni ya kuchanja mifugo ili mifugo hiyo iweze kunenepa na kuepukana na minyoo kwa sababu kufanya hivyo kutasaidia Iramba kuwa na ng’ombe wenye afya na ubora mkubwa.

Kwa upande wake mmoja wa wauzaji wa  nyama wilayani hapa, Zakaria Shila alithibitisha kuwa wao katika maeneo yao wanauza kilo ya nyama kwa Tsh 6000 hadi 7000 kwa sababu wakiuza zaidi ya Tsh 7000 ua 8000 hakuna atakayenunua.

Naye Asha Juma mfanyabiasha ya mamantilie alimshukuru mkuu huyo wa wilaya kwa agizo la kupunguza bei ya kilo ya nyama iuzwe Tsh 7000 kwa sababu hapo awali walikuwa wakipata changamoto ya kununua kilo moja ya nyama kwa Tsh 8000, 9000 hadi 10000 kwa baadhi ya bucha mjini Kiomboi.

MWISHO

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • KIDATO CHA KWANZA KURIPOTI SHULE January 13, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • MAAFISA ELIMU KATA 136 MKOANI SINGIDA WAPATIWA MAFUNZO KUHUSU USIMAMIZI WA SHULE NA UJAZAJI TAKWIMU KATIKA MFUMO WA "SIS"

    March 24, 2025
  • DC MWENDA AWASISITIZA WALIPA KODI KUFANYA MAKADIRIO YA KODI KABLA YA MACHI 31, 2025

    March 20, 2025
  • DC MWENDA NA WAZIRI MWIGULU NCHEMBA WACHANGIA JUMLA YA MADAWATI 98 SHULE YA MSINGI MSANSAO ILIYOPO KATA YA MTEKENTE

    March 10, 2025
  • WALIMU WAKUU 108 WA SHULE ZA MSINGI NA MAAFISA ELIMU KATA 20 WILAYANI IRAMBA WAPEWA MAFUNZO ENDELEVU YA USIMAMIZI WA UFUNDISHAJI NA UJIFUNZAJI FANISI KUPITIA JUMUIYA ZA KUJIFUNZA ZA WALIMU WAKUU NA MAAFISA ELIMU KATA

    March 19, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.