• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Mkuu wa wilaya ya Iramba mkoani Singida, Suleiman Mwenda amewaomba waandishi wa historia kuendelea kuenzi na kuthamini mchango uliotolewa na wanawake kabla na baada ya Tanzania kupata uhuru.

Posted on: March 9th, 2022

Na Hemedi Munga

tehama@irambadc.go.tz

Singida - Iramba. Mkuu wa wilaya ya Iramba mkoani Singida, Suleiman Mwenda amewaomba waandishi wa historia kuendelea kuenzi na kuthamini mchango uliotolewa na wanawake kabla na baada ya Tanzania kupata uhuru.

Mwenda ametoa ombi hilo leo Jumanne Machi 08, 2022 wakati akihutubia maelfu ya wananchi waliohudhuria katika maadhimisho ya siku ya wanawake duniani yaliofanyika kiwilaya katika viwanja vya Shule ya Wasichana Tumaini mjini hapa.

“Ni bahati mbaya sana kutotaja mchango uliofanywa na mwana mama shupavu kabla na baada ya uhuru wa Taifa letu Hadija Kamba ambaye aliwahi kusema na kudai kizazi cha haki na usawa kwa maendeleo endelevu.” Alisema Mwenda

Aidha, aliongeza kuwa kauli mbiu hii “Kizazi cha haki na usawa kwa maendeleo endelevu” ambayo leo tunajivunia ni kauli ya kishupavu na ukomavu iliyosemwa na mwana Mama Hadija Kamba ambaye ni mmoja wa waasisi wa Taifa la Tanzania na Chama cha Mapinduzi (CCM) ambacho kinaongoza nchi yetu.

Kwa mara ya kwanza Hadija Kamba alisikika akitajwa mwaka 1985 na Mwalimu Julius K. Nyerere wakati akiwahutubia wajumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM katika ukumbi wa Diamond Jubilee akiwa anawaaga na kuwatangazia rasmi kuwa anangatuka katika nafasi ya urais na kubaki kuwa Mwenyekiti wa CCM.

Mwalimu Nyerere alisema kuwa katika miaka 24 ya urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuna mwanamama ambaye alikuwa akimshangaza kwa sababu ni mwanamama ambaye alipambana enzi za ukoloni ili kulipatia Taifa uhuru.

“Katika kina mama waliokuwa mstari wa mbele katika mapambano enzi za Ukoloni katika siku ngumu na za hatari ni Hadija Kamba.” Alisema Mwalimu Nyerere

Baada ya kupata uhuru Mwalimu Nyerere alimwita Hadija Kamba nakutaka kumpa cheo ingawa alikataa na kuyasema maneno ya kishujaa ambayo leo siye tunajivunia.

“Lengo la kushiriki na kuingia katika mapambano ya kuondoa Ukoloni ilikuwa ni kuhakikisha tunapata jamii ya haki na usawa, hivyo nimeridhika kabisa kwa sababu lengo langu limetimia kwa sababu sasa Waafrika wanathaminiwa katika nchi zao na hawatawaliwi tena.” Alisema Kamba

Kauli hiyo ilimfanya Mwalimu nyerere kusema kuwa sio watu wengi walioshiriki mapambano hayo na hawakuwa wanalenga kupata madaraka ispokuwa ni wa chache akiwemo Hadija Kamba.

“Kwa bahati mbaya sana historia yetu kipindi cha Ukoloni, mapambano dhidi ya Ukoloni na hata katika kupata uhuru wetu hawatajwi wanawake hawa muhimu walioshiriki kwa namna moja au nyinginge kuhakikisha tunapata uhuru wetu.” Alikumbusha Mwenda na kuongeza kuwa

“Historia yetu imetaja sana wanaume kama vile wakati wanaume wakipambana hawakuwa na akina mama hawa, hivyo ni wakati sasa kwa waandishi wetu kuenzi na kuthamini michango iliyofanywa na wanawake hawa katika kulijenga Taifa letu” Alisisitiza

Akiongelea michango muhimu inayofanywa na Wananwake nchini, Mwenda alisema kuwa tunaye Mama ambaye ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan ambaye kwa kipindi cha miezi michache amefanya mambo makubwa ambayo hayajawahi tokea katika historia ya nchi yetu.

Aidha, alifafanua kuwa katika kipindi cha awamu ya kwanza ya urais hadi ya tano kwa wilaya ya Iramba kulikuwa na vituo vya afya vitatu laniki katika kipindi cha Rais Samia tayari Iramba inajenga vituo vya afya vitano na maendeleo haya ni katika wilaya zote za nchi yetu.

Kwa upande wa barabara kwa mara yakwanza katika kipindi hichi cha Rais Samia Iramba ilipata Tsh 6.5 bilioni kwa ajili ya ujenzi wa barabara huku fedha nyingi yakwanza kuja wilaya ya Iramba tangu kupata uhuru ni Tsh 800 milioni.

Pia, katika nishati ya umeme tayari Mkandarasi ameishapatikana ambaye atamalizia vijiji 14 vilivyokuwa havina umeme, hivyo ni dhahiri sasa Iramba itakuwa haina kijiji ambacho hakina umeme.

Halikadhalika, kwa upande wa madarasa kwa ajili ya wanafunzi Iramba ilifanikiwa kupata fedha na kujenga madarasa 67 huku madarasa zaidi ya elfu kumi na tano (15,000) kwa Tanzania nzima.

Katika kuhakikisha mama anatuliwa ndoo kichwani na maji yanapatikana kwa urahisi takribani Tsh 4.8 bilioni zinatekeleza miradi mbalimbali ya maji nakuifanya Iramba kufikia asilimia 52 ambapo wakati Rais Samia anaingia madarakani Iramba ilikuwa na asilimia 26.

“Kwa kweli kwa ushahidi na takwimu hizi ninashawishika kusema kuwa tukiwaamini wanawake katika nafasi za uongozi tutapata matokeo chanya.” Alisema

Kwa upande wake Mjumbe wa Kamati Tendaji Taifa ya Chama cha Walimu (CWT), Mwl. Ulumbi Shani alisema kuwa ukimuelimisha mama utakuwa umelielimisha Taifa. Hivyo tunaendelea kumuunga mkono Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan kwa sababu ni Mama ambaye anaendelea kututangazia kwamba kinana mama tunaweza katika nyanya zote.

“Ni hakika kwamba Mama ni chanzo cha kila fani na nichanzo cha mafanikio ya kiuchumi, kijamii na kisiasa katika familia na Taifa kwa ujumla.” Alisema Shani

Naye Sara Mitula Mkazi wa Kinampanda wilayani hapa alimuomba Mkuu huyo wa Wilaya kuendelea kutokomeza unyanyasaji wa jinsia ambao wamekuwa wakikutana nao katika mazingira tofauti tofauti hasa katika makabila ambayo bado yanatekeleza mfumo dume.

Aidha, Sara ameitaka jamii kutambuwa kuwa maendeleo endelevu ni lazima yahusishe jinsia zote kwa kuzingatia haki na usawa ili kukuza uchumi wa jamii na Taifa.

MWISHO.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba, Mhandisi Michael Matomora akiwa na Mwnyekiti wa Halmashauri hiyo Innocent Msengi wakicheza mziki kuwaunga mkono wakina mama katika maadhimisho ya siku ya wanawake duniani yaliofanyika katika viwanja vya shule ya wasichana Tumaini kata ya Kinampanda Wilayani Iramba Mkoa wa Singida. Picha na Hemedi Munga

Hivi ndivyo wanawake walivyopendeza katika picha ya pamoja wakati wa maadhimisho ya siku ya wanawake duniani yaliofanyika katika viwanja vya shule ya wasichana Tumaini kata ya Kinampanda Wilayani Iramba Mkoa wa Singida. Picha na Hemedi Munga



Tangazo

  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI June 05, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • DC MWENDA ATEMBELEA MRADI WA UJENZI WA SHULE MPYA YA SEKONDARI YA AMALI KITUKUTU

    May 08, 2025
  • KAMATI YA FEDHA, UONGOZI NA MIPANGO YA HALMASHAURI YA WILAYA YA IRAMBA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO

    May 06, 2025
  • DC MWENDA ATOA WITO KWA WALIMU WA SHULE ZA MSINGI KUIMARISHA UFUNDISHAJI KWA MADARASA YA MITIHANI

    May 06, 2025
  • JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI WILAYANI IRAMBA LATOA ELIMU YA KINGA DHIDI MAJANGA YA MOTO KWA MADIWANI NA WANANCHI

    May 02, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.