• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Mkuu wa wilaya ya Iramba mkoani Singida, Suleiman Mwenda amewasihi wananchi wa kijiji cha Ndulungu kuwa na subira wakati serikali ikiendelea kupanga na kutekeleza mikakati ya kuwaletea wananchi hao miradi ya maendeleo.

Posted on: January 23rd, 2022

Na Hemedi Munga

tehama@irambadc.go.tz

Singida - Iramba. Mkuu wa wilaya ya Iramba mkoani Singida, Suleiman Mwenda amewasihi wananchi wa kijiji cha Ndulungu kuwa na subira wakati serikali ikiendelea kupanga na kutekeleza mikakati ya kuwaletea wananchi hao miradi ya maendeleo.

Mwenda ameyasema hayo mwishoni mwa juma hili wakati alipokutana na wananchi wa kijiji cha Ndulungu wilayani hapa.

Usia huo unatokana na agizo alilolitoa Mkuu huyo wa wilaya wiki moja iliyopita kuitaka Kamati ya Maendeleo ya Kata ya Ndulungu kukubaliana kuchagua kati ya takribani Tsh 350 milioni zinazotarajiwa kutengeneza barabara kijiji cha Ndulungu na takriban Tsh 250 milioni kwa ajili ya kujenga kituo cha afya kijiji cha Mwandugyembe ndani ya kata hiyo.

Miradi hii ilidaiwa kuzua mgogoro kati ya wananchi wa kijiji cha Mwandugyembe kunakotarajiwa kujengwa kituo cha afya huku kijiji cha Ndulungu itengenezwa barabara, jambo ambalo wananchi wa kijiji cha Ndulungu hawakukubaliana nalo wakidai kuwa miradi mingi inapelekwa katika kijiji cha Mwandugyembe.

Akieleza maamuzi ambayo yalifikiwa na Chama cha Mapinduzi (CCM) ngazi ya kata hiyo, Kijiji cha Ndulungu na Kamati ya Maendeleo ya kata hiyo, Mwenda alisema CCM waliamaua kituo hicho cha afya kijengwe Mwandugyembe kwa sababu ndio maelekezo ya muongozo toka serikali kuu. Huku muhtasari wa kijiji cha Ndulungu wakiamua kuwa kituo hicho kijengwe Ndulungu wakati muhtasari wa Kamati ya Maendeleo ya Kata wakiamuwa kuwa kituo hicho kijengwe kijiji cha Mwandugyembe.

“Hivyo ndugu zangu ni dhahiri serikali kuu walizingatia sababu nyingi za kujenga kituo cha afya Mwandugyembe, hata maamuzi ya CCM pamoja na Kamati ya Maendeleo ya kata yamehitaji kituo hicho kijengwe Mwandugyembe, hivyo niwaombe wananchi wa Ndulungu kuwa na subira serikali itajenga kituo cha afya Ndulungu kadri uwezo utakavyoruhusu.” Aliomba Mwenda

Aidha, aliongeza kuwa serikali itafikisha huduma ya afya katika kila kijiji ndani ya kata huku akitolea mfano wa huduma ya umeme ambayo kwa wilaya ya iramba yenye vijiji 74 ambapo vijiji 60 vinaumeme na vijiji 14 tayari mkandarasi ameisha patikana kufikisha umeme katika vijiji hivyo.

Akitoa shukrani mbele ya mkuu huyo wa wilaya Mwenyekiti wa Chama cha Mpinduzi (CCM) wa kata hiyo, Said Hassan aliomba kuwa jambo hili liendelee kuelezewa vizuri zaidi.

“Nikushukuru Mkuu wa wilaya na timu yako kwa namna ambavyo umejitahidi kulielezea na kutatua mgogoro huu, hivyo tunaomba kadri uwezo utakavyokuwa ukipatikana basi tuelekeze maendeleo kijiji cha Ndulungu.” Alisema

Kwa upande wake mmoja wa wananchi wa kijiji hicho, Mwanaidi Nyauli alisema kuwa yote yalioongelewa na Mkuu huyo wa wilaya yamezidi kuwatia uchungu.

“Kwa kweli tunamachungu kwa sababu mnada umepelekwa Mwandugyembe, sekondari imejengwa Mwandugyembe na sasa kituo cha afya kinajengwa Mwandugyembe, Jamani serikali tunaomba mtuonee huruma na sisi wa Ndulungu mtufanyie hima tupate kituo cha afya.” Alisema

Naye Jafari Kamoko akasema kuwa kituo cha afya kilipaswa kijengwe Ndulungu kwa sababu Mwandugyembe tayari wamepata mnada na shule ya sekondari.

Aidha, alieleza kuwa swala la kila kitu kinapelekwa Mwandugyembe kinafanya wananchi waone kuwa kuna upendeleo.

MWISHO

Tangazo

  • WAHI NAFASI YA AJIRA August 19, 2021
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2018 HALMASHAURI YA WILAYA IRAMBA January 05, 2019
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA KIDATO CHA PILI (FTNA) 2018 January 05, 2019
  • TANGAZO LA KULIPA KODI YA ARDHI. February 26, 2018
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • DC Mwenda aahidi ufadhili masomo nchini China matokeo mazuri kidato cha 6 Iramba

    May 09, 2022
  • Waumini Iramba wamuombea Dua ya Kheri na Mafanikio Rais Samia kumi la mwisho Ramadhani

    May 01, 2022
  • DC Mwenda awapongeza viongozi ukamilishaji kuweka vibao anwani za makazi Iramba

    May 01, 2022
  • DC Mwenda awajaza matumaini watumishi Rais Samia kutamka neema Mei Mosi

    April 29, 2022
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.