• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Mkuu wa wilaya ya Iramba mkoani Singida, Suleiman Mwenda amewataka wananchi kulinda na kuuenzi Muungano wa Tanzania ulioasisiwa na Hayati Mwal. Julius K. Nyerere Rais wakwanza wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Rais wa Zanzibari Mzee Abed Karume April

Posted on: April 26th, 2022

Na Hemedi Munga

tehama@irambadc.go.tz

Singida - Iramba. Mkuu wa wilaya ya Iramba mkoani Singida, Suleiman Mwenda amewataka wananchi kulinda na kuuenzi Muungano wa Tanzania ulioasisiwa na Hayati Mwal. Julius K. Nyerere Rais wakwanza wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Rais wa Zanzibari Mzee Abed Karume Aprili 26, 1964.

Mwenda ametoa wito huo leo Jumanne Aprili 26, 2022 wakati wa maadhimisho ya Muungano wa Tanzania akiongea na Wananchi na Watumushi punde baada ya kupanda miti katika viwanja vya Halmashauri ya Wilaya hiyo mjini hapa.

Alisema kuwa kitaifa maadhimisho hayo yanafanyika jijini Dodoma ambapo viongozi wamekusanyika kujadili nchi hii ilipotoka, ilipo na iendapo kwa lengo la kuimarisha na kudumisha Muungano wa Tanzania.

Akiongea kuhusu Muungano, Mwenda alisema mara kadhaa wamekuwepo maadui wakitamani Muungano huu kuvunjika.

“Ndugu zangu bado wapo watu ndani ya nchi na nje ya nchi wakitamani Muungano huu uvunjike kwa sababu mara kadhaa hoja zinazolenga kuvunjika Muungano katika vikao vya maamuzi katika nchi yetu zimeibuka.” Alisema

Alieleza kuwa mtetezi mkubwa wa Muungano ambaye ni Rais wa kwanza wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mwal. Nyerere alifikishiwa hoja ya kuvunja Muungano mara kwa mara.

Alifafanua kuwa Mwal. Nyerere aliitisha Baraza la Mawaziri kwa lengo la kujadili hoja iliyodaiwa kuwa Mzee Karume hautaki Muungano kipindi hicho.

“Taarifa hizi zilimuumiza sana Mwal. Nyerere na kuita Baraza la Mawaziri kujadili suala la Muungano.” Alisimulia na kuongeza kuwa

Mmoja kati ya wasaidizi wa Mwal. Nyerere alimshawishi Mwal. Nyerere kuwa yupo Katibu Mkuu wa ASP Mzee Thabit Kombo hapa Dar es Salaam ni vyema aitwe ili aulizwe madai haya ya hoja ya kuvunja Muungano.

Baada ya Mzee Thabit Kombo kufika mbele ya Mwal. Nyerere nakuelezwa madai haya, Mzee Kombo alisema kuwa jambo hili sio kweli kwa sababu Mzee Karume hawezi kuja na hoja ya kuvunja Muungano.

“Naomba nikuthibitishie niende nikamuulize Mzee Karume.”

Katika kuhakikisha Mzee Kombo anapata uhakika wa hoja hii, Mzee Kombo na Mmoja wa wasaidizi wa Mwal. Nyerere walikwenda kuonana na Mzee Karume.

Baada ya kukutana na Mzee Karume na kumueleza madai haya, Mzee Karume alisema kuwa hilo jambo halipo ni uongo kabisa na nijambo la kutengeneza na sijui ni nani kamuaminisha Mwal. Nyerere jambo hili.

Hatimaye Mzee Kombo na Mmoja wa wasaidizi wa Mwal. Wakarejesha majimbu kwa Mwal. Nyerere kuwa Mzee Karume alisema kuwa hilo jambo ni uongo na ni ufitini wa hali ya juu.

“Kwa kweli ni uongo, kwa sababu Mzee Karume alisema kuwa hajawahi, kutamka, kunongona, kuandika wala kufikiria juu ya kuvunja muungano huu.” Alimthibitishia Mwal. Nyerere Mzee Kombo

Hali hii ilimfanya Mwal. Nyerere kufurahi na kumkumbatia Mzee Thabit Kombo na kuwaruhurusu mawaziri kurejea nyumbani kwa sababu hakuna tena Baraza la Mawaziri.

“Sasa ni wjibu wetu kuulinda na kuuenzi Muungano wetu kwa sababu watu ambao wanaopinga Muungano bado wapo ndani ya nchi yetu na nje ya nchi ili waone tu Tanzania imevunjika.” Aliomba Mkuu huyo wa wilaya

Aidha, aliongeza kuwa Muungano ni nembo inayobeba uhai wa Taifa na kuchangia uhai wa wanadamu na viumbe vingine kupitia uwepo wa miti na uoto wa asili, hivyo tunapaswa kuendelea kutunza na kulinda uoto wa asili katika mazingira yetu.

Wananchi wa Iramba katika kuhakikisha wanatunza mazingira wameafinikiwa kupanda miti takribani 238 kati ya miche 500 iliyokusudiwa kupandwa.

Kufuatia hali hiyo, Mwenda aliwataka wananchi hao kuendelea kuhamasishana kulinda na kutunza maliasili na miti na kuwa wakali wa waharibifu wa miti na maliasili.

Alisema miaka 58 ya Muungano wa Tanzania kumekuwa na mabadiliko makubwa ya hali ya hewa ambayo kwa sehemu kubwa yanatokana na uharibifu wa mazingira.

Aidha, alitolea mfano wa Msitu wa Sekenke Tulya ambao miaka takribani 40 iliyopita kulikwa na wanyama wa kila aina mfano wa nyumbu, nyanti, tembo na faru ambapo kutokana na uharibu wa mazingira wanyama wote wamehama.

Akiongelea kuhusu hali ya hewa miaka ya nyuma Iramba watu walikuwa wakivaa makoti kwa sababu ya baridi lakini sasa haiwezekani.

Pia, alitolea mfano wa nchi ya China katika mji wa Bejin ambapo hufika msimu watu hawavai makoti wala shati kwa kuroa kutokana na nyuzi joto kufikia 42 mpaka 45, hali ambayo ilichangiwa na kutumia makaa yamawe kuendesha viwanda vyao.

“Niwaombe! Tulinde mazingira yetu.”

Akiongea katika hafla hiyo katibu wa jumuiya ya wazazi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wilayani Iramba, Mwal. Iddi Kijamba aliwataka watanzania kuendelea kuuenzi na kuulinda muungano wa Tanzania kwa gharama yoyote.

Alibainisha kuwa Muungano uliokusudiwa na waasisi wetu ulikuwa ni kuhakikisha uhusiano wa kiudugu, kisiasa, kilugha na kibiashara unatamalaki.

“Muungano huuo ndio unaotufanya sisi watanzania tuishi bila ya kubaguana na kuwa wamoja na kudumisha amani na utulivu.” Alisema Kijamba

Aidha, alisema kuwa tuwakatae kila ambaye ataleta chochoko za kutaka kuvunja muungano, kwa sababu watu hao hawana nafasi katika jamii ya watanzania.

Naye Afisa Mazingira wa wilaya hiyo, Yohana Dondi alimshukuru Mkuu wa wilaya hiyo kwa kufanikisha maadhimisho ya Muungano wa Tanzania kwa kupanda miti kwa namna taratibu na kanuni zinavyoelekeza.

“Kwa kweli tumefanya vizuri kwa sababu wananchi wameadhimisha muungano kwa kufanya usafi na kupanda miti ili kuifanya Iramba ya kijani.”

MWISHO

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • KIDATO CHA KWANZA KURIPOTI SHULE January 13, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • MAAFISA ELIMU KATA 136 MKOANI SINGIDA WAPATIWA MAFUNZO KUHUSU USIMAMIZI WA SHULE NA UJAZAJI TAKWIMU KATIKA MFUMO WA "SIS"

    March 24, 2025
  • DC MWENDA AWASISITIZA WALIPA KODI KUFANYA MAKADIRIO YA KODI KABLA YA MACHI 31, 2025

    March 20, 2025
  • DC MWENDA NA WAZIRI MWIGULU NCHEMBA WACHANGIA JUMLA YA MADAWATI 98 SHULE YA MSINGI MSANSAO ILIYOPO KATA YA MTEKENTE

    March 10, 2025
  • WALIMU WAKUU 108 WA SHULE ZA MSINGI NA MAAFISA ELIMU KATA 20 WILAYANI IRAMBA WAPEWA MAFUNZO ENDELEVU YA USIMAMIZI WA UFUNDISHAJI NA UJIFUNZAJI FANISI KUPITIA JUMUIYA ZA KUJIFUNZA ZA WALIMU WAKUU NA MAAFISA ELIMU KATA

    March 19, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.